Kwa kuwa baba yake na wadogo zake wakiume walimudu ile biashara ya kusambaza mayai na maziwa. Wakati mwingine kuku, Naya akajikuta yupo tu hosteli. Hana anachokifanya isipokuwa kusoma. Baba yake alikuwa akimtumia pesa kiasi cha matumizi. Akawa hana sababu yakulalamika tena. Maisha yakawa shule na hosteli kwenye kelele za Lulu na Malon.
Kila siku kulikuwa na jipya juu ya Lulu na Malon. Na Lulu naye aliyapamba hayo mahusiano, kama kujivunia tu na kufurahia.
Siku hiyo ya alhamisi akiwa ndio anatoka darasani, akapigiwa tena
simu na Madamu Vane akimtaka arudi kazini. Naya alifurahi sana. “Lakini bado siku chache
tuanze mitihani. Nitafanya weekend hii, halafu nitapumzika. Nikimaliza mitihani
nitarudi.” “Utakuwa umenisogeza. Si unajua Lulu naye ameacha? Nasikia amepata
mwanaume anayemtunza vizuri. Ameacha bila hata kuniaga! Nimeona tu hafiki, nikimpigia
simu, hapokei! Ndio rafiki zake wameniambia amepata mwanaume.” “Hamna shida.
Mimi nitajaza nafasi yake.” “Lakini nakutaka na usimamizi Naya. Napenda jinsi ulivyo mwaminifu
na unavyojituma. Zungumza na wasichana wa hapo. Waambie ipo kazi. Tuone wangapi
watakubali, kisha unijulishe.” “Sawa. Nitazungumza nao, kisha nitakujulisha
tumepata wangapi.” Wakaagana huku Naya akiumia na kufurahia.
Alirudi hosteli akaenda chumbani kwa Girls star, akakuta wamenunua
tv kubwa, spika nzuri na redio yenye CD, wanashangilia na wapambe wao. “Mambo
ya Lulu hayo!” Naya akacheka. “Hongereni. Mtatupunguzia kiwingu kwenye
tamthilia.” “Na kweli. Siku hizi tunakula kuku na kuangalia tamthilia vitandani
kwetu, tena kwenye flat screen!” Lulu akajisifia. “Haya mama, hongera. Sasa
kazi jumamosi, mpo?” “Kwani umerudi kazini!?” Wote wakashangaa. “Nimerudi ndio
natafuta watu wakufanya kazi.” “Mimi sitaweza. Jumamosi natoka na Malon.” Lulu
akajitoa kwa majivuno. “Haya, na nyinyi kina Hawa, Tuli na Tunu?” “Mama sisi
tupo. Tena utuandike wa kwanza. Sisi bado hatujawapata kina Malon.” Naya
akaandika majina yao, akatoka. Akawaacha wanashangilia utajiri.
Ni kweli maisha ya Lulu yalibadilika. Alibadili chumba chao.
Akaweka thamani za maana. Kazi akawa hafanyi tena. Ikawa ni shule na chumbani
akiangalia tv na kufurahia utajiri. Naya yeye akarudi kazini kwa nguvu zote. Jumamosi
hiyo alifanya kazi kwa bidii zote. Mitihani ikaanza. Akatulia kabisa shuleni.
Wakamaliza mitihani, wakafunga likizo ya mwezi wa sita. Akarudi nyumbani.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Akawekeza akili kwenye kazi, na tuition. Alikuwa kidato cha 4,
hapakuwa na mapumziko mengi. Shule ya ziada iliendelea wakati wenzao wapo
mapumzikoni. Na akili zilitulia kwa kuwa hapakuwa na habari za Lulu na Malon.
Alikuwa akikutana na wenzake mara kwa mara kujisomea katikati ya juma.
Hakukosa. Jumamosi kama kawaida akawa akienda kazini anakoitwa na Madamu Vane.
Akichelewa kutoka, anakwenda kulala nyumbani kwa bosi wake, Madamu Vane.
Ukaribu ukaongezeka. Naya akawa mtu wa karibu sana na bosi wake, kila mtu
akamuheshimu.
Likizo ilikwenda kwa haraka sababu ya shuguli nyingi. Shule, kazi
na majukumu ya nyumbani. Naya alikuwa mchapa kazi za mikono haswa. Hakuwa mzuri
kwenye mambo ya ndani ya nyumbani kama mtoto wakike. Lakini ukimuweka nje, hata
kuwapa kuku chakula tu, hakuwa na shida. Kwanza hakusubiri kutumwa. Kipindi
hicho cha likizo, wakawa wameshamjua. Akiamka tu asubuhi, kitu cha kwanza sio
kupika hata chai. Ni kwenye banda la kuku. Ataosha vyombo vyote vya kuku.
Ataweka maji safi na dawa. Ataweka chakula. Ataokota mayai, ndipo anatoka
kwenda kusoma. Kwanza hawakupenda apike. Walisema hajui kupika. Na yeye hakuwa
akijisumbua hata kusogea jikoni. Mdogo wao wa mwisho yeye ndio alikuwa akiosha
vyombo. Usingemkuta Naya jikoni. Mpaka mama yake alikuwa anasema Mungu
alitakiwa amfanye Bale ni Naya, Naya, Bale.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Alirudi hosteli siku ya jumapili jioni kwa kuwa jumamosi alikuwa
na kazi ya usiku. Alirudi kulala nyumbani kwao kwa kuwa alijua lazima siku
inayofuata arudi hosteli. Alijiandaa kuweka akili shuleni haswa, kwani ndio
ulikuwa muhula wa mwisho.
Shule ikaanza kwa kasi zote. Shuleni, hosteli na kazini. Safari za
nyumbani zikawa zimepungua sababu ya ubusy wa kujisomea. Mtoto huyo wa Mwalimu,
hakuhitaji kuhimizwa shule. Nyumbani kwao kila mtu alijua umuhimu wa kusoma.
Ulikuwa mwezi wa nane mwishoni. Birthday ya Naya. Hakuwa hata na
habari kwa sababu nyumbani kwao hawakuwa wakisherehekea vitu kama hivyo. Kwa
hiyo siku za birthday hazikuwa za ajabu. Ni kama siku nyingine zozote tu. Naya
alikuwa ndio anatimiza miaka 18. Ilikuwa siku ya jumatato. Alikwenda shule kama
kawaida. Akaunganisha kwenda kujisomea na wenzake. Akarudi hosteli kama kwenye
saa 12 na nusu jioni.
“Nimechoka, nakaribia kuanguka na usingizi.” “Kula ndio ulale.” Wahija
akamjibu akiwa na yeye anarudisha vitu kabatini kwake. Ndio alikuwa anarudi na
yeye kutoka chuo. “Mtu kama anampenda mdogo wake si angeenda kumletea tu maji
yakuoga!” Wengine wakacheka. “Umeanza Naya!” “Mimi mbona huwa nakuchotea maji, da
Wahija? Tena bila kunituma.” “Na kweli. Haya, anza kuvua nguo, naenda sasa
hivi. Na usilale.” “Najilaza kitandani kwako.” “Hapana naya bwana! Utaniwekea
jasho.” “Da Wahija, hata mimi?” Mara hodi.
“Mnataka nini chumbani kwetu?” Wahija akaongea bila kukaribisha,
Lulu akaingia. “Nina mzigo wa Naya.” Lulu alionekana kukosa raha sana usoni.
Alipooza kupita kiasi. Naya na Wahija wote wakageuka. Ulikuwa mfuko mkubwa sana
wa zawadi. Unakadi nyekundu kubwa iliyoweza kuonekana mpaka nje ya ule mfuko na
maua. Wakati anashangaa, Lulu akauweka ule mfuko chini kwa hasira kidogo,
akaondoka na kufunga mlango.
“Makubwa! Nani huyo?” Wahija akauliza huku akiokota ule mfuko,
akamkabidhi Naya. Akaanza kuufungua na maswali mengi mpaka usoni. Akatoa maua
kwanza. Wahija akavuta kadi na kuifungua kwa haraka. “Haaa!” Wakamsikia Wahija anashangaa kwa sauti.
“Inatoka wapi da Wahija?” Naya akauliza huku akifungua kijiboksi kidogo
kilichofungwa vizuri. Macho yakamtoka Naya. Ilikuwa cheni nzuri sana, nzito ya
dhahabu. Yenye kidani kidogo cha alama ya kopa kilichobeba herufi ya N. Naya akakunja uso na kumpokonya ile
kadi Wahija. “Kumbe leo ni birthday yako!?” Wahija akashangaa. Naya akasoma.
Haikuwa na maneno mengi zaidi ya kumtakia birthday njema, chini jina la Malon.
Naya akamtizama Wahija kwa mshangao.
Wote wakabaki kimya kwa muda. Ndipo na wenzao wakatoka vitandani
kwao na kusogelea vile vitu wakitaka kujua. “Vimetoka wapi?” “Eti kwa Malon!”
Wahija akajibu. “Sasa kwa nini ampe mwanamke wake alete!?” Mmoja wao akauliza
kwa mshangao. “Ndio ushangae na wewe!” “Ndio maana Lulu kaingia hapa amenuna!
Atakuwa amemlazimisha yeye ndio alete.” Mwingine akaeleza. “Huyu Malon si
mjinga. Atakuwa ameleta hivi vitu na ujumbe wa zaidi ya huo, ndio maana akataka
Lulu ndio alete.” “Sasa ni ujumbe gani huo kama sio kutukosanisha na Lulu tu?”
“Kwani wewe Lulu alikwambia Malon amemuoa?” Wahija akauliza, Naya akakunja uso.
“Wewe si ulibadilisha namba ya simu? Sasa unajuaje kama kumkubali
Lulu ndio ilikuwa njia yakuendelea kuwa karibu na wewe?” Naya akabaki kutoa
macho. “Wewe huyajui makubaliano ya Malon na Lulu. Unachujua ni kelele za Lulu
akitoka huko kwa Malon.” “Sio kwa Malon, anakuwa anatoka kwenye starehe na
mpenzi wake.” Naya akaongeza kwa wivu. “Kama angekuwa mpenzi wake angemtuma
akuletee wewe cheni, mwanamke uliyemuacha amekupigia magoti?” “Wala hakupiga
magoti! Wamemsingizia Malon.” “Leo ndio unataka kusema wakati sisi tulikuuliza
humu ndani ilikuaje, tena kwa kurudia rudia, ukasema hutaki kuongelea! Leo ndio
unajidai kusema hakupiga magoti!” Naya akaanza kucheka.
“Tula au Chezo mmoja wao aliongeza chumvi ili kunogesha stori.
Malon anipigie mimi magoti wakati watoto wazuri kama kina Lulu wapo! Anataka
nini kwangu na wakati wote tulikuwa tunatangaziwa hapa staili alizokuwa akipewa
huyo Malon?” “Nakuuliza kama angekuwa anapewa hayo yooote, kwa nini akuletee
cheni leo, tena amtume Lulu mwenyewe?” “Bwana mimi sijui! Sasa nitafanyaje da
Wahija?” “Asante.” “Akuu! Sitaki kumtafuta yule kaka.” “Ila cheni unataka?”
Naya akacheka sana.
“Dhahabu hii da Wahija!” “Tena dhahabu haswa.” “Mimi naiweka
bwana. Kwani nimemuomba? Si kaniletea mwenyewe.” Wahija na wenzake wakaanza
kucheka. “Naya wewe mtoto mkorofi wa chini chini.” “Kweli da Wahija. Mimi
sikumuomba. Kwanza hata nilikuwa sijui kama leo ni birthday yangu. Sijui
kaambiwa na nani. Kaniletea cheni...” “Tena yenye jina lako.” Wahija
akamkatisha na kumfanya acheke zaidi. “Si umeona mwenyewe da Wahija? Sasa yeye
anaitwa Malon. Mwanamke wake Lulu. Nikiwarudishia kidani chenye N, utakuwa utahira.” Wakacheka hapo, lakini Naya alifurahi sana.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Siku zikaendelea kwenda. Naya akiendelea kutafakari juu ya Malon.
Hakika hakuwa amemuelewa, ila alimfurahisha sana. Aliona ni kama amemkumbuka,
bado hajamsahau. Ilimgusa sana. Ila taratibu kelele za Lulu zikaanza kupungua.
Akawa ametulia sana tofauti na zamani. Week hiyo ikaisha, na ya pili. Lulu
akawa ametulia sana.
Naya akawa amepewa tena kazi. Ilikuwa mwezi wa 9 katikati. Madamu
Vane alimwambia ni mtu amenunua nyumba hapo jijini. Anafanya house warming.
Amealika rafiki zake, anataka wasichana wanne. Akamtaka na Naya awepo. Kama
kawaida, hakumsahau Hawa rafiki yake aliyemuunganishia kwenye hiyo kazi.
Akamfuata Tula na Tunu chumbani kwao. “Kuna kazi jamani. Safari hii nyumbani
kwa mtu. Madamu Vane amesema kuvaa nyeusi, sio lazima kiatu cha juu. Mnataka?”
Kimya. Akaona na wenyewe wamepooza. Naya alipoona kimya hakutaka maneno mengi
na wao, aliwajua wale wasichana. Akataka kutoka.
“We Naya.” Tula akamwita. “Nini? Naona mmeninyamazia, nikajua hamtaki.” “Na Lulu?” “Nimeambiwa watu wanne. Kwa kuwa siku hizi Lulu hachukui kazi, nimemtafuta Hawa. Ipo nafasi ya watu wawili. Sasa nyinyi chagueni wenyewe, kisha mniambie nani anakwenda. Tena sasa hivi ili nimtumie majina Madamu Vane.” Tula na Tunu wakatizamana. “Tuandike sisi.” “Sawa.” Naya akajibu na kuondoka.
Jumamosi.
K |
wa kuwa Naya
alishakuwa kiongozi wao, alijitahidi kuwahi kujiandaa. Wakaita usafiri, akaenda
kumfuata Tula na Tunu. Akashangaa kumkuta Lulu pale chumbani, hajatoka kama
kawaida yake, Naya hakutaka kumsemesha. “Mpo tayari warembo?” “Mbona sasa wewe
umevaa kawaida tu, umetuacha wenzio tumevalia?” Tunu akawa kama analalamika.
“Niliwaambia kabisa ni nyumbani kwa watu, Madamu amesema tuvae nyeusi sio
lazima viatu vya juu. Nyeusi niliyonayo na niliyoona inafaa nyumbani kwa mtu,
tena ufukwenu ndio hii na sendozi. Kama nyinyi mmependeza zaidi, tatizo liko
wapi!?” Wakanyamaza.
“Naombeni tuwahini. Mimi sitaweza kuchelewa zaidi.” “Umepanda cheo
ndio umesahau kama sisi tulikuwa tukikusubiria?” “Sijasahau hata kidogo. Lakini
nimepigiwa simu muda sio mrefu, natakiwa kuwahi kabla ya sherehe kuanza, ili
kukabidhiwa vitu. Nyinyi mnaweza kuchelewa kidogo, mimi siwezi. Kwa hiyo basi,
anayetaka kuongozana na mimi twende, ambaye bado, aite taksi au uber.” Naya
akatoka. Wakamfuata nyuma bila kuchelewa maana walimjua Naya hababaishwi na
haogopi mtu.
Alipiga simu kwa bosi wake, akampa dereva amuelekeze mpaka kwenye
hiyo nyumba. Basi wakatulia garini wakati wakipelekwa kazini. Eneo ilipokuwepo
hiyo nyumba ilikuwa Kunduchi beach kabisa. Ndogo tu, lakini nzuri sana. Wote
wakabaki wanashangaa. “Huyu atakuwa mzungu tu.” Tuli akanong’ona. “Kwa kukuta
magari yote haya, inamaana tumechelewa.” Naya akaongeza. Mlinzi akawaruhusu
waingie ndani, maana walishushwa nje ya geti. Wakasogea mpaka kwenye nyumba
yenyewe wakionyesha kubabaika. Naya akasogelea mlango na kubonyeza kengele.
Akaja mtu kufungua na kopo la Heneken mkononi. Mziki wa kawaida tu ulikuwa
ukiendelea.
“Tumetumwa kuja kusaidia kazi ya kugawa vinywaji na chakula.” Naya
alianza hivyo. “Chezo! Chezo!” Wote wakaangaliana. Wakasikia Chezo anaitika.
“Kuna wageni wako hapo mlangoni.” Chezo akafika pale akionekana alikuwa
akicheka. “Mmefika wakati muafaka, warembo. Tuli upo mama?” “Nipo Chezo.” Naya
akampisha Tuli aliyesalimiwa kwa kutajwa jina. “Karibuni ndani.” Chezo
akatangulia. Naya aliweza kutambua baadhi ya sura. Lakini mbali na wale vijana
waliokuwa nao kwenye baa ya Masaki, kulikuwa na wazee, watu wazima na kina
mama, wote walionekana kwenye wakati mzuri. Wakina Naya walisalimia, nakupitiliza
jikoni. Kabla yakuingia jikoni, kulikuwa na friji na Cooler boksi kubwa sana.
Waliambiwa humo ndipo vilipo vinywaji. Chezo aliwaambia hawategemei watu wengi
sana, lakini walitaka kitu kisiharibike na baada ya hapo, watataka msaada
wakukusanya chupa zote na sahani. Wasafishe ndipo kazi yao itakuwa imeisha.
Wakapelekwa na jikoni. Wakaonyweshwa kila kitu kilipo. Chezo yeye akaondoka.
Kwa kuwa walikuwa na uzoefu, walijua nini chakufanya. Wakachukua
masinia ya vinywaji matupu ili warudi kule walipowageni. Wachukue chupa tupu na
kuchukua oda mpya. Mpaka hapo, Hawa hakuwa amefika na Naya alipompigia simu
wakati wapo njiani hakuwa akipatikanika. Wasiwasi ulimwingia, lakini baada
yakujua kazi yenyewe, wasiwasi ukamtoka. Akawaambia kina Tula wasiwe na
wasiwasi, wao watatu watatosha tu. Akatoka Tula na sinia tupu mkononi. Akafuata
na Tunu. Wakati Naya anajiandaa kutoka, akageuka, akakuta Malon amemsimamia
nyuma yake.
Akashtuka sana. “Malon!” Akajikuta anamwita kwa sauti ya juu
kidogo. Malon akacheka tu. “Ume..” Naya akasita. “Karibuni.” Malon
akamkaribisha. “Asante. Lakini tumekuja kikazi. Na wewe umealikwa?” Naya
akauliza akionekana kupaniki. Malon akacheka huku akitingisha kichwa kukataa.
Naya akakunja uso na kuamua kutoka pale. Ngoja mimi nianze kazi.” Akampita
Malon pembeni, akaelekea walipo wageni.
Kulijaa vicheko humo ndani.
Kadiri muda ulivyozidi kwenda, ndivyo watu walivyoongezeka na kuzidi
kulewa. Kufika saa nne, hapakuwa na mgeni mpya, lakini wengi wao walikuwa
wakinywa tu, walishalewa. Naya na wenzake wakaendelea kuwahudumia. Ilipofika
saa 5 usiku, Malon akamfuata Naya jikoni. “Njoo.” “Nani, mimi?” Tula akajishika
kifuani. “Naya. Njoo uwasalimie baba na mama. Wanataka kuondoka.” Naya akakunja
uso. “Malon!” “Njoo bwana. Usiogope.” Hata hakujua kama wazazi wa Malon
walikuwa pale. Naya akamsogelea Malon. “Malon!” Naya akamvuta mkono kama arudi
wazungumze kwanza. Malon akarudi, akamshika mkono kwa nguvu na kumvutia sebuleni.
Kina Tula wakasogea kushuhudia.
“Mama na baba, huyu ndio Naya.” Naya alikuwa akitetemeka. Kila mtu
pale sebuleni akanyamaza kimya. “Shikamooni.” Naya akawasalimia kwa heshima na
kuwapa mkono. “Chezo alituambia ulikuja Morogoro. Tukajua ungekuja kutusalimia
nyumbani, nikaona kimya.” Naya akababaika kidogo. “Nitakuja wakati mwingine.”
Akajibu akimtizama Malon. “Basi jogoo wako anakusubiri.” Akaongeza baba yake
Malon. “Jogoo za Mzee, za upendeo pendeleo!” Chezo akalalamika, wote wakacheka.
“Mgeni siku ya kwanza. Ya pili kuku wa kienyeji. Siku ya tatu maharage.”
Akajibu baba yake Malon, wote wakacheka. “Sisi tunaondoka tunarudi Morogoro.
Usiku sana sasa hivi. Tushapaona hapa, inatosha. Siku nyingine tukiwa hapa
mjini, mtashtukia tupo mlangoni.” Aliongea baba yake Malon, akisimama na mkewe.
Naya hakujua hata ajibu nini. Akacheka tu huku akimtizama Malon kwa wasiwasi.
“Ngoja tuwasindikize mama.” Malon akamvuta Naya mkono mpaka
mlangoni wakafungua mlango. “Ushalewa nini, mama?” “Sijanywa sana bwana wee!” Akajibu
mama yake Malon. “Mbona sasa miguu hainyanyuki?” Malon akaendelea kumuuliza mama
yake huku akimwangalia miguu yake. “Uzee. Unataka nikimbie kama wewe?” “Haya
mama. Taratibu usijikwae kwenye meza hapo.” “Nilikuwa namwambia asinywe,
akaniona nataka kumnyima raha. Haya, taratibu usije vunja meno bure.” Baba yake
akaongeza. Malon akamfuata mama yake akamshika mkono.
“Au mlale tu. Eti mama?” “Acha wasiwasi wewe Malo! Nimekwambia
mimi mzima. Miguu tu ndio inasumbua.” “Imeanza lini?” “Muda tu. Baba yako
amesema tutaenda kumuona dakatri, naona zimebaki ahadi tu.” “Tutaenda bwana.
Mambo yamekuwa mengi.” Naya alikuwa amesimama mlongoni akisubiria Malon na mama
yake wafike. Wakatoka, akafuata baba yake aliyekuwa akiagana na wageni wengine
kwa kupeana mikono, kisha na yeye akatoka. Naya alibaki hajui kama afuate nyuma
au arudi jikoni. “Naya!” Akamsikia Malon akimwita. Akatoka kwa haraka.
Akamkuta Side yupo kwenye gari ileile iliyomrudisha Dar, akilia.
Akamsogelea. “Habari Side?” “Ooooh! Naya mwenyewe! Kumbe upo mama?” “Nipo,
sijakuona ndani.” “Ndio nimefika muda sio mrefu. Kuna kitu nilikuwa nafanya
mjini. Ndio nataka niwarudishe wazee nyumbani. Mzima lakini?” Naya akacheka.
Akakumbuka vile alivyokuwa akilia siku ile. “Mzima Side. Muwe na safari njema
mnaporudi Morogoro.” “Asante sana.” Naya akarudi alipokuwa amesimama Malon.
Akamfungia mama yake mlango, akarudi nyuma kidogo. “Taratibu Side.” “Bila
shaka.” Side akamjibu Malon, wakaagana, nakuondoka.
Wakabaki Malon na Naya wamesimama pale nje. Naya akacheka kidogo.
Malon akashika kile kidani pale shingoni kwa Naya. Alikuwa amevaa ile cheni
aliyokuwa amempa Lulu ampelekee siku ya birthday yake. Akakizungusha kidogo
huku akitabasamu kama anayefikiria kitu. “Asante kwa zawadi.” Akaona ashukuru.
“Nimefurahi sana kuona umeivaa.” Naya akacheka kidogo, na kugeuka akitaka
kurudi ndani. “Naya!” Malon akaita. “Abee!” Naya akageuka. “Naomba unisamehe.”
Naya akakunja uso. “Kwa nini tena?” Naya akauliza kwa sauti ya chini tu.
“Chochote nilichokuudhi.” Naya akainama akifikiria. Kimya.
“Hata na hicho
unachokifikiria sasa hivi pia, naomba unisamehe.” Naya akamwangalia. Akaona machozi
yanajaa machoni. Hata yeye hakutegemea. Akajifuta, na kugeuka. Akaondoka kurudi
ndani. Baada ya muda kidogo watu wengine wakaaga. Wazazi wa Chezo nao
wakaondoka pamoja na marafiki wengine. Wakabaki Malon, Chezo na marafiki zao
wengine. Mpaka hapo hawakuwa wakijua nyumba ni ya nani. Wakaendelea kusafisha.
Mpaka wanamaliza kusafisha nakurudisha kila kitu sehemu yake, wakawa wamebaki
watu wanne hivi. Mpishi alishamaliza, akalipwa na kuondoka.
Naya alipohakikisha kila kitu kipo sehemu yake, wakasogea pale sebuleni.
“Tumemaliza. Mnaweza kukagua kabla hatujaondoka.” Naya aliongea akimtizama
Chezo. “Patakuwa sawa tu. Si mkae sasa na nyinyi mpumzike.” Tula na Tunu
wakakaa kwa haraka. Naya akacheka. “Jamani mimi naomba niwaage. Nitangulie.”
“Kwa nini hutaki kukaa, Naya?” Chezo akauliza. Malon alibaki akimwangalia Naya.
“Kwanza nimeshaita Uber, atakuwa yupo hapo nje akinisubiri. Pili, nina mambo
yakufanya hosteli. Lazima nimalize leo. Nawaachieni hao warembo, muwe na wakati
mzuri.” Naya akamaliza kiustarabu, akatoka.
“Naya!” Akamsikia Malon
akimwita, akageuka. “Naweza kukurudisha.” “Naona Uber imeshafika. Asante.”
Wakabaki kimya kidogo kisha Naya akawa kama amekumbuka kitu. “Halafu Malon,
naomba usiwe unamtuma mpenzi wako aniletee vitu.” Malon akacheka. “Nani
amekwambia Lulu ni mpenzi wangu?” Naya akakunja uso na kushangaa. “Malon!”
“Nakusikiliza Naya.” “Basi bwana. Mimi naomba usiwe unamtuma mwanamke wako
kwangu. Unatuchonganisha na kutufanya tuwe maadui bila sababu.” “Kwani
amekufanyia chochote!?” “Hapana. Lakini..” “Ahaa! Nilifikiri amekufanyia fujo
au maneno ya kipuuzi, nimpasue kichwa.” Naya akashangaa sana.
“Mimi naomba nikapumzike Malon.” “Sasa nikitaka kukutumia zawadi nifanyaje?” “Naomba usilete zawadi Malon. Tafadhali sana. Nilikwambia pale hosteli tuna miiko tuliyojiwekea.” “Uliniambia, sijasahau na wala hutavunja sharti lolote lile. Na pia sitakuruhusu ufanye hivyo.” Naya akawa bado haelewi. “Mimi nahisi nimechoka Malon. Naenda kulala.” “Naomba namba yako ya simu, Naya.” Naya akageuka na kuondoka bila yakujibu.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Na Chezo akawa amemwambia Tula ambaye ni kama mwanamke wake kwa wakati huo, kuwa Malon alikuwa karibu na Lulu ili kuwa karibu na Naya. Ndio maana hata siku moja Malon hakuwahi kufika hapo ndani kwao akimfuata Lulu, lakini alikuwa akiingia mpaka ndani kumfuata Naya. Ikawa maneno mengi. Naya alikuwa akijisikilizia tu na kunyamaza. Watu wakageuka kuanza kumcheka Lulu na Girls star. Ikawa aibu tupu. Kuwa walikuwa na maneno mengi kumbe hata Malon mwenyewe hakuwa anamtaka Lulu. Kama aliyekuwa ameonywa, Lulu hakurudisha neno hata moja. Akawa kimya. Baada ya kama juma moja, Lulu akahama kabisa pale hosteli. Maisha ya Naya yakaendelea kama kawaida.
Majuma mawili mbeleni, siku ya ijumaa, Naya alimka tumbo likimuuma
sana. Akashindwa hata kwenda shuleni. Akabaki hosteli amelala siku nzima.
Wahija alitoka chuo, akamkuta anahangaika kitandani, akampa dawa, akarudi
kulala. Wahija akaamua kusomea hapohapo chumbani ili awe na Naya. Kila mtu
alimjua Naya ni mdogo wake Wahija. Na Naya anaweza kumsikiliza Wahija kwa
chochote atakachomshauri. Akasikia mlango unagongwa taratibu kisha Tunu
akaingia. “Una mgeni wako da Wahija.” “Nani?” Akauliza Wahija. “Wewe nenda utamuona
mwenyewe.” Akajibu Tunu na kuondoka. Wahija akatoka.
Akashangaa kumkuta Malon sebuleni akimsubiria. “Wewe si ndio
Malon!” “Ndiyo. Tunaweza kuzungumza?” “Kama nikuhusu Naya, nataka unijibu swali
langu kwanza.” Kila mtu alimjua Wahija kwa maneno. Malon akatulia. “Wewe
unamtaka Naya au Lulu? Maana unakazi ya kuchanganya akili za hawa watoto, Lulu
kakimbia hosteli hapa.” “Kwani wewe Lulu alikwambia yupo kwenye mahusiano na
mimi?” Malon akauliza akiwa ametulia tu. “Ndivyo alivyosema.” “Kwa hiyo na mimi
nikisema ni raisi wa Marekani utaniamini?” Wahija akanyamaza.
“Mimi nipo hapa kwa ajili ya Naya.” “Na Lulu?” Wahija akauliza.
“Mimi sijui umesikia nini juu ya Lulu, nashauri uzungumze naye vizuri, upate
ukweli kutoka kwake. Siwezi kujibu maswala ya Lulu. Ila tu, ujue Naya
amebadilisha namba ya simu. Kila ninayemuomba namba yake, hana. Naya ni mpenzi
wangu. Kila mtu au anajulikana na wanaonifahamu mimi. Mambo mengine mimi sijui.
Leo nimeambiwa ni mgonjwa, hakwenda shule. Ni kweli?” Wahija akanyamaza.
“Nimekuita wewe sio kwa bahati mbaya Wahija. Naya ni mgonjwa nataka kujua jinsi
yakumsaidia.” “Nimempa dawa, amelala.” “Amekula?” “Alikuwa anatapika.
Nimemnunulia chips yai, akimka ndio nitampa nione kama vitakaa tumboni. Ila
akitapika tena, ndio nilipanga kumpeleka hospitali.” “Naweza kumuona?” Wahija
akanyamaza.
“Nakuuliza kama naweza kumuona sio kwa sababu nashindwa kuingia
chumbani kwenu. Ni kwa sababu nataka uzungumze na Naya, akubali nimuhudumie
kipindi hiki mgonjwa. Nimeambiwa wewe anakusikiliza.” “Sasa unaomba au unataka
nikubembelezee kwa Naya?” Malon akacheka na kutingisha kichwa. “Nakuomba
uzungumze na Naya. Nampenda Naya na jibu la hapana kwa yeyote hata Naya
mwenyewe haliwezi kunifanya niache kumfuata. Nitafanya chochote niwe na Naya.
Wewe naomba unisaidie tu. Kwanza hakuna mtu atampenda Naya kama mimi.” Wahija
akaanza kucheka.
“Sasa kilichokupelekea kulala na Lulu ni nini?” “Sasa hivi Naya
ananihitaji mimi. Naomba hizo kesi ziwe za wakati mwingine. Nitatafuta muda
wakuzungumza na wewe, lakini naomba isiwe leo. Nimepata taarifa za ugonjwa
wake, nikapanda gari na kuja hapa. Naomba tu nimuone.” “Twende, lakini ujue
itakuwa ni juu yako wewe mwenyewe kama hataki kukuo...” “Sasa wewe ndipo
ninapotaka unisaidie. Zungumza naye.” Wahija akamtizama Malon, akaongoza njia
kurudi chumbani kwao alipokuwepo amelala Naya.
Wakaingia chumbani kwao. “Kitanda chake hicho hapo juu.”
Akamuonyeshea alipolala Naya. Malon akasogea nakuanza kumgusa kichwani
taratibu. Akamvuta mkono akaushikanisha viganja kwa kupitanisha vidole vyake
katikati ya vidole vya Naya. “Malon!” Naya akafungua macho na kushangaa vile
Malon amemshika na kumsimamia pembeni ya kitanda. “Vipi?” “Mwenzio naumwa.
Tokea asubuhi natapika!” “Pole.” “Asante. Umekuja kufanya nini?” “Chezo
ameniambia unaumwa sana, unatapika ndio maana nimekuja.” “Itakuwa ameambiwa na
Tula. Alinikuta nje asubuhi wakati nachota maji, natapika.” “Pole sana.”
“Asante kwa kuja kuniona.” Malon akatoa tabasamu.
“Umekula?” “Natapika Malon. Sijui kwa nini mwezi huu umekuja hivi!
Huwa sipati siku zangu na maumivu hivi.” “Twende ukapumzike.” “Morogoro!?”
“Hapana Naya. Siwezi kukupeleka mbali.” Naya akanyamaza. “Twende. Utapumzika.” “Umeniumiza
Malon. Umeniumiza sana.” “Nimekuomba msamaha Naya. Naomba nisamehe. Na ujue nimefanya kila
kitu kwa kuwa nakupenda. Sikukusudia kukuumiza. Nisamehe. Na hata kama huna
mpango wa kukunisamehe sasa hivi, basi naomba twende nikakuuguze nikuache ukiwa
mzima. Siwezi kukuacha ukiwa hivi mgonjwa. Utanifanya nihamie hapo juu
kitandani kwako.” “Malon!” “Sikutanii Naya. Muulize Wahija.” “Umeongea na dada Wahija!?”
“Yeye ndio ameniruhusu niingine nije kukuona.”
Naya akafurahi kusikia na Wahija ameruhusu. Bado alikuwa amejilaza
kitandani, Malon akipitisha kidole chake kimoja taratibu kwenye nyusi zake, na
kuzunguka nywele.
“Nakupenda Naya.” Naya akacheka taratibu. “Nisamehe siku ile niliondoka
kwa hasira.” Malon akacheka na kujilaza kichwa kwenye mbao ya kitanda
akimtizama. “Ulikuwa hata ukinikumbuka kweli?” Naya akanyamaza. “Naya?” “Nina
mambo mengi Malon.” “Safari hii nimejifunza. Nitakuwa mtoto mzuri.” Naya akacheka
taratibu kwa sauti ya ugonjwa na deko juu. “Twende. Nakuahidi mapumziko mazuri.
Utarudi ukiwa unajisikia vizuri.” Naya
akakaa. Akashangaa kumbe kila mtu alikuwepo mle chumbani wakiwasikiliza.
Akacheka na kujifunika na mto. “Bwana da Wahija!” “Wewe nenda.
Ukipata nafuu ndio urudi.” Naya akacheka. “Nikubebe?” Malon akauliza huku
akimtizama. “Sijazidiwa bwana! Kwanza dawa alizonipa da Wahija, zimenisaidia.
Sina hata haja ya kwenda.” “Naomba usibadili mawazo Naya. Tafadhali.
Nimeendesha muda wote huo nikiwa na wasiwasi na wewe.” Naya akashuka kitandani.
“Labda nioge kwanza Malon.” “Twende utaoga hukohuko.” Naya
akasita. “Vipi?” “Njoo nikunong’oneze.” Malon akainama kumpa sikio. “Naweza
kuchafua gari.” Naya akanong’ona. “Usijali. Twende.” Akakusanya vitu vichache.
Akawaaga pale na kutoka na Malon. Malon akamfungulia mlango wa gari, Naya akatandika
khanga ndipo akakaa. “Hatuendi mbali?” “Tunaelekea pale ulipokuja kwenye house
warming.” Naya akamtizama kama mwenye swali. “Vipi?” “Kwani na pale ni kwako?”
“Huoni na wazazi walikuja? Nilinunua kwenye mnada wa benki. Bei haikuwa mbaya
sana.” “Hongera Malon. Unajitahidi.” “Hivyo hivyo.” Wakatulia. Malon akiendelea
kuendesha.
“Unajisikiaje?” “Sasa hivi tumbo na kiuno vimetulia kidogo, sio
kama asubuhi.” “Unataka kula nini? Lazima tununue. Pale nimeweka walinzi tu.
Nikiondoka nafunga.” “Chochote utakachopenda wewe. Mimi nimetapika sana, nahisi
nimepoteza hamu ya kula.” “Basi nitakutengenezea uji.” “Asante Malo. Nashukuru
kwa kuja kuniona na kunichukua.” Malon akamwangalia na kuguna. “Unaniringia
Naya wewe!” “Sikuringii Malon. Najiona nina mambo mengi yakunizidi umri wangu.”
“Kwa kuwa unataka kuyabeba mwenyewe. Hutaki tushirikiane.” “Hutabiriki Malon.”
“Mimi sitabiriki tena? Leo ningekuwa hapa kama sitabiriki?” “Basi mimi
sikuelewi Malon.” “Kwa kuwa hutaki kunielewa Naya. Tunakwenda mbele, na kurudi
nyuma.” Naya akanyamaza.
“Vipi?” “Natamani kuoga tu
nilale. Najihisi kuchoka. Sijisikii vizuri Malon.” “Unauhakika ni tumbo tu,
hamna malaria au kitu kingine?” “Sijui. Ngoja nijipe siku ya kesho. Nikiendelea
hivi, ndio nifikirie kwenda hospitalini.” “Wazo zuri. Basi twende moja kwa moja
nyumbani. Wakati unaoga, mimi niwe nakutengenezea uji, ujaribu.” “Na wewe
chakula?” “Usijali. Nitajua tu kitu chakufanya ukisha tulia.” “Pole Malon.
Nakusumbua eeh?” “Hata kidogo. Ningesumbuka kama ungekuwa unaumwa halafu sipo
kukusaidia. Hiyo ingenisumbua.” Ikamgusa sana Naya. Akajifuta machozi. Malon
akamuona. “Nakupenda sana Naya. Kuliko nitakavyokwambia. Na sikukusudia
kukuudhi siku ile. Nilifanya kutaka kukulinda. Lakini nimejifunza. Nakuahidi
sitaingilia tena.” Naya akanyamaza.
Walifika nyumbani kwa Malon, akamsaidia kushuka. Naya alikwenda
moja kwa moja bafuni kuoga. Malon alimletea taulo kubwa. Akarudi jikoni kupika.
Baada ya kumaliza kuoga, akatoka na kumfuata Malon jikoni. “Vipi?” “Nasikia
kutapika Malon. Huo uji sidhani kama utapita.” “Maumivu?” “Nahisi kama dawa
zimeanza kuisha. Natamani kulala tu.” “Nikikupa dawa sasa hivi, hutatapika?”
“Sasa sijui nifanye nini!?” “Tujaribu dawa. Ukitapika, nakupeleka hospitalini
tuombe wakuchome sindano yakuzua kutapika na wakupime vitu vingine.” “Sawa.”
Malon akampa dawa. Naya akabaki amejiegemeza pale jikoni. “Twende kitandani
ukajilaze. Usipotapika, nakupa uji.” Wakaongozana mpaka chumbani. Kilikuwa
chumba kizuri sana. Naya akakipenda ila hali ilikuwa mbaya.
“Au nimpigie simu baba?” “Naya! Acha kupaniki bwana. Tumekubaliana
tusubiri. Naomba utulie. Usiogope. Mimi nipo hapa na wewe, ukizidiwa nakupeleka
hospitalini.” Naya akanyamaza. “Ni sawa?” “Nikifa je? Naweza kufa bila
kumuaga baba yangu. Na nisipomuaga...” “Naya! Naya! Naomba tulia na
unyamaze. Huwezi kufa bwana.” “Unajuaje?” “Jilaze hapa kwanza. Halafu niambie
kama bado maumivu yanaendelea.” “Yanaendelea.” “Naya! Wewe
muoga bwana.” “Sana.” Malon akaanza kucheka asiamini.
“Usicheke.” “Naomba tulia, tuzipe dawa muda wakufanya kazi.
Utakuwa sawa. Lala hapa.” Malon akamuwekea mto vizuri akapanda na
kumfunika. Akakaa hapo pembeni yake.
“Utaunguza uji.” “Upo sawa. Nimezimia jiko. Jitahidi kutulia.” Naya akafunga
macho kwa muda. Mara akamuona anakimbilia chooni. Alitapika vitu vichungu,
kuashiria dawa. Alitapika tena na tena. Malon akaona ampeleke tu hospitalini.
Alipofika hospitalini, akafanyiwa vipimo, akakutwa na Malaria. “Mpigie
simu baba yangu. Tafadhali Malon. Nitachanganyikiwa asipokuja.” Malon akachukua
simu ya Naya, cha kwanza akajipigia yeye na kumpigia simu baba yake Naya. “Naitwa Malon.
Nipo hospitalini na Naya. Anaumwa. Amesema nikutaarifu. Lakini usiwe na
wasiwasi. Hajazidiwa sana. Alikuwa anatapika. Wamemchoma sindano na kumuwekea
dripu ya maji. Ikiisha watamruhusu.” “Nashukuru kwa taarifa. Nakuja.” “Lakini usiwe na
wasiwasi Mzee wangu.” “Huyo hana ugonjwa mdogo wala mkubwa. Ukishamsikia
anataka niitwe, ujue ndio amefika kipimo chake cha mwisho cha uvumilivu. Hapo
atakuwa ameshafikiria kufa na kila kitu. Hawezi kutulia mpaka niwepo hapo. Acha
tu nije mwenyewe.” Malon akacheka kidogo. Akajua ndio tabia yake.
“Sawa. Sasa usiku huu utapata
usafiri kweli? Au uje kesho?” “Nitafika tu. Hapawezi kukucha leo kwa amani bila
mimi kuwepo hapo. Namjua Naya. Ikifika hatua hiyo ni heri daktari asiwepo, mimi
niwepo. Hawezi kutulia tena, na hakuna dawa itafanya kazi tena. Atakwambia
amezidiwa tu. Acha tu nije.” Malon akacheka tena. “Wewe mwambie nakuja sasa
hivi, ndio atatulia.” “Naweza kukufuata.” “Usiku huu!?” “Hamna shida. Tupo hapa
Mwenge.” “Hakuna sababu. Nitafika tu, nashukuru.” Yule Mzee akakata simu.
Malon akarudi ndani. “Baba
amesemaje? Anakuja?” “Anakuja. Ila amesema utulie. Utakuwa tu sawa.” Akatulia kidogo
akafunga macho. “Unafikiri atapata usafiri mida hii au labda unipeleke tu
nyumbani kwetu.” “Naya! Naomba ulale bwana. Baba atafika. Tafadhali tulia.” “Tunaishi Kiluvya,
Malon. Na sasa hivi...” “Naya! Naya! Naomba utulie bwana. Baba yupo njiani anakuja.” “Nipe
nizungumze naye.” “Kwa hiyo mimi hunihitaji hapa?” Naya akatulia kidogo. “Eti
Naya?” “Nahisi nikuzidiwa. Hamna dawa inafanya kazi, Malon! Naumwa
sana. Nimezidiwa sana.” Malon akakumbuka maneno ya baba yake Naya.
“Nisikilize Naya. Najua unaumwa. Wamekupa dawa na wamekuwekea
dripu ya maji. Tulia. Ipe muda ifanye kazi. Na ujue baba anakuja. Au unataka
mimi niondoke?” “Hapana Malon. Sina maana ya kukufukuza. Samahani. Ila nahisi
naweza kufa, halafu nikashindwa kuagana na baba yangu.” “Utakuwa
sawa. Haufi leo na baba yupo njiani anakuja” Akavuta pumzi, akarudi kulala.
Baada ya kama lisaa baba yake akafika. Akampigia simu, Malon
akatoka kwa haraka. “Tupo hapa nje.” “Nakuja kuwachukua.” Malon akatoka. Akamkuta baba
yake, mama yake na wadogo zake wote. Ikabidi asalimie wote na kuwashika mkono.
“Hajaanza kulia?” Zayoni akamuuliza Malon huku wanacheka. “Hajakwambia anataka
kufa baba akiwepo?” Bale akaongeza na kufanya wacheke taratibu. “Amelala.” Malon
akajibu huku akicheka kwa heshima. “Basi huyo hajui maumivu bila baba yake. Na
tungechelewa au angekuwa peke yake, angeanzia nyumbani kwanza, ndio baba yake
ampeleke hospitali. Na hatapiga simu kukwambia anakuja akiwa anaumwa. Ili usije
mwambia mkutane hospitali. Utashtukia yupo mlangoni, analia kama anakaribia
kukata roho. Na amkute baba yake. Asipomkuta, huna dawa utakayompa Naya,
ikamsaidia.” Mama yake akaongeza wakacheka taratibu.
Wakaingia kwenye chumba alichopumzishwa kwa muda. Baba yake
akamsogelea. “Naya!” Akafungua macho. “Naumwa baba. Nimezidiwa sana.” Malon akaona
wadogo zake wanakonyezana na mama yao. “Tokea asubuhi natapika baba.
Sipati nafuu.” “Mbona hukunipigia?” “Nilijua nitapona. Lakini nahisi
nitakufa tu baba.” Malon akashangaa sana. “Huwezi kufa. Nimeambiwa ni malaria.
Ukianza dawa, utapona tu mama.” “Umeniangalia joto lakini?” Baba yake
akamuwekea mkono kichwani. “Joto kali. Lakini utapona tu. Pole mama yangu
mzazi. Pole sana.” “Asante baba.” “Ngoja nikaombe kitambaa hapo mapokezi, nije kukuwekea
kichwani, nikukande mpaka joto liishe.” “Afadhali umekuja baba. Labda
nitapona.” “Lazima upone.” “Asante.” Naya akasikika ametulia kwa maneno
ya baba yake.
“Mama na kina Bale nao wamekuja.” “Usingekuja na kina Bale!”
Wadogo zake wakaanza kucheka. “Watanifanya nizidiwe tu hao.” “Nishawaambia
wanyamaze.” “Pole Naya.” Bale akamsogelea. “Sitaki.” Naya akajibu. “Pole Naya.”
Mdogo wao mdogo naye akajaribu. “Na wewe pia sitaki. Kwanza sijui
kwa nini mmekuja!? Wataanza kunichukua video baba.” “Nimewaonya.
Hawathubutu.” Baba yake akamtuliza. “Pole Naya, mama. Pole sana.” “Asante mama.
Ungepumzika tu, usingesumbuka. Nimepewa dawa, nitapona tu.” Naya akabadilika
kwa mama yake. Mpaka Malon akashangaa. “Hamna shida. Tulilala sana mchana. Hata
hao walilala sana mchana ndio maana wametaka kuja na wao.” “Msingekuja nao.
Kwanza kesho shule.” “Kweli umezidiwa Naya! Kesho jumamosi.” “Achana na mimi.”
Bale na mdogo wake wakazidi kucheka. Malon kimya akiwasikiliza na kuwatizama
kwa kujiiba.
“Samahani, tumeingia na swala la ugonjwa tu, tukasahau kufahamiana.
Sisi ndio wazazi wa Naya. Hao ni kaka zake.” “Nimefurahi kuwafahamu. Mimi
naitwa Malon.” Akajitambulisha tu hivyo. “Tunashukuru kwa taarifa za ugonjwa.
Maadamu tupo hapa, wewe nenda tu kapumzike. Wakimruhusu huyu, tutarudi naye
nyumbani mpaka apone kabisa.” Zile hazikuwa taarifa nzuri kwa Malon. Lakini
akajikaza. “Hamna shida. Nitawasubiri tu, ili niwarudishe nyumbani. Najua usiku
sana sasa hivi, mtapata shida ya usafiri.” Mpaka mama yake akamgeukia Malon.
“Umesema wewe ni nani tena?” “Mama!” Naya akashtuka. “Kwani nini?
Si nataka kumfahamu?” “Amesema anaitwa Malon.” “Oooh! Wewe ni mwenyeji wa wapi
mwanangu?” Akaendelea mama yake Naya. “Naishi Morogoro.” Ukimya wa ghafla.
“Sasa nini?” Naya akawauliza. Wakaanza kucheka. Hasa wadogo zake. “Baba si
nilikwambia mimi? Heri ungekuja tu peke yako.” Naya akalalamika. “Ujue
anachojiuliza mama ni kuwa, Malon wa Morogoro amejuaje kama wewe huku Dar
unaumwa?” “Umbea tu. Kwani wewe upo kwenye mawazo ya mama? Hayo ndio mawazo
yako wewe Bale. Kwanza ondoka.” Bale na mdogo wake wakaanza kucheka. Na Malon
akacheka kidogo.
“Labda mimi niulize, mnafahamiana na Malon?” “Mama Naya! Acha
bwana mtoto apone!” “Mimi namuuliza Malon, si Naya mgonjwa!” “Baba umeona sasa?
Nahisi utakuwa umejifunza. Siku nyingine usije nao hawa.” “Eti Malon?” “Ndiyo
mama. Nafahamiana na Naya. Mmoja wa wanafunzi mwenzake anayeishi naye pale
hosteli alimuona akitapika. Ndio nikajulishwa. Ikabidi nije.” “Kutokea
Morogoro!?” Bale akadakia na kuuliza kwa mshangao nakufanya wote wacheke mpaka
Malon mwenyewe. “Usimjibu mwaya Malon. Hao ni wachokozi tu.” Mama yake akacheka
kidogo, akatulia. “Nashukuru sana kumleta hospitalini.” Baba Naya akashukuru. “Na
kuja kutokea Morogoro, baba. Morogoro mbali!” Akaongeza mama Naya. “Tena kwa
malaria tu!” Bale akaongeza kichokozi, wakacheka tena. Naya akamrushia mto
aliokuwa amelalia.
“Haya tokeni nje.” Baba yao akawafukuza. “Sasa hapa kosa langu
lipi baba? Mimi nimekukumbusha kushukuru na hilo.” “Baba usimsikilize. Watoe
nje. Labda mama na wewe ungeenda kukaa nao hapo nje?” Naya akaongea kwa heshima
kidogo kwa mama yake. “Basi nitoke na Malon tuzidi kufahamiana.” “Malon
amechoka mama. Mwache bwana.” Wakazidi kucheka. “Sijui mkoje bwana! Baba naomba
waambie wakasubiri nje mpaka hii ndipu iishe, tuondoke.” Naya huyu, sio yule
aliyekuwa amezidiwa mpaka kutaka kufa. Alishapata nafuu kwa baba yake tu kuwepo
hapo, usingeweza jua hata ni kwa nini yupo pale. Baba yake akawafukuza. Akatoka
mama yao na kaka zake huku wanacheka. Naya akarudi kulala.
Walikaa pale chumbani kimya. Malon na baba yake. Dripu ilipoisha,
Naya akiwa usingizini, Malon akatoka kwenda kumwita nesi. Akaja akamtoa. Akampa
kikaratasi cha dawa. Malon akapokea na kumwambia baba yake Naya, ataenda
kuchukua dawa, na kulipia kabisa, ndipo atakuja kuwachukua awarudishe nyumbani.
“Asante Malon.” “Hamna shida. Nitarudi baada ya muda mfupi sana.” Malon
akatoka. Maswali mengi yalianza kwa baba yake Naya. Naya alijua, lakini
akanyamaza.
Malon alirudi na dawa mkononi. “Nafikiri tunaweza kuondoka.”
“Nashukuru sana. Mungu akubariki.” Baba yake Naya akashukuru. “Amina baba. Basi
twendeni ili huyu akapumzike. Kuna dawa za kuzuia kutapika wamempa. Wanasema
zinaweza kumfanya alale sana, lakini zitamsaidia kutotapika na kuweza kumaliza
dozi yake ya malaria.” “Asante.” Naya akashukuru tena. Malon akamsogelea.
“Nikubebe au utaweza kutembea?” Malon
akauliza kwa sauti ya chini ili baba yake asisikie. Naya akakataa kwa
kutingisha kichwa huku akicheka taratibu. Malon alikuwa amesimama katikati ya
baba yake na Naya. Akamsadia kushuka kwenye kitanda. Wakatoka. Wadogo zake
walikuwa wamemuinamia mama yao kama wanaangalia kitu kwenye simu moja.
Walipowaona wanatoka, wakasimama.
“Vipi?” Mama yake akauliza. “Tunarudi nyumbani. Malon amesema
atatusaidia usafiri.” Akajibu baba yake. “Asante.” Mama yake akashukuru, wadogo
zake wakaanza kukohoa kishabiki. Naya akawaangalia. “Sijui mnashida gani
nyinyi!” Naya akalalamika. “Sasa tumefanyaje? Sisi tumekohoa tu.” “Twende mwaya
Malon.” Naya akaongoza njia, wakawa wanamfuta nyuma Naya. Wakafika nje kwenye
gari ya Malon. Wakabaki wamezubaa. “Ni nini jamani kama sio kunitia aibu tu!”
Naya akalalamikia wadogo zake. “Bwana baba zungumza nao!” “Hii ndio gari
yakutoka Morogoro!?” Bale akauliza, wakaanza kucheka. “Hivi kwa nini hawa
hawapandi daladala, baba!” “Tusipande SUV!? Hata kidogo. Hata kwa kupakatana,
tunapanda tu.” Malon akacheka.
“Nafikiri tutatoshea tu. Kuna viti vya nyuma kabisa.” Malon
akafungua gari ili kuinamisha viti, wapande. “Ungewaacha wapakatane tu.” Naya akaongea
huku akifungua mlango upande mwingine nyuma lakini akimpisha baba yake akae
mbele. Wadogo zake wakacheka na kuingia nyuma kabisa kwa haraka. Malona
akarudisha kiti, nakumpisha mama yake Naya akae pale na Naya. Akafunga mlango,
Malon akaingia upande wa dereva, akaanza kuondoa gari.
Akaendesha bila kuuliza. Akafika mataa ya Ubungo, akakata kona
kulia, kuelekea Kibaha. “Mama! Bale anauliza mbona Malon haulizi njia? Au
anapafahamu?” Kila mtu akaanza kucheka tena. Naya akageuka na kumpiga kaka
yake. “Sipafahamu nyumbani. Ila Kiluvya tu.” “Ndio kwetu Malon. Kumbe mwenzetu
wewe mwenyeji kabisa. Kumbe ni sisi tu ndio tulikuwa hatukufahamu!” Bale
akaongeza kiushabiki. “Baba!” Naya akamwita kwa kulalamika. “Naomba waambie
wanyamaze bwana! Wananitia aibu.” Baba yake mwenyewe alikuwa akicheka.
Zikaanza stori mpaka walipofika Kiluvya. “Hapa ndio mwisho wangu.”
Malon akamgeukia baba yake Naya. “Hata hapa sio mbali na nyumbani. Ndio
kituoni. Tunatembea tu.” “Naweza kuwasogeza mpaka nyumbani, kama ni sawa.” “Ni
sawa Malon.” Akadakia Bale. Naya akaguna. “Yaani Bale! Malon anaongea na baba.
Wewe yamekupataje?” “Baba hakawii kusema tushushwe hapa wakati tunao usafiri wa
Moro mpaka nyumbani tena wa bure!” Ilibidi tu baba yao amuelekeze Malon mpaka
nyumbani. Malon alifurahia kufika nyumbani kwa kina Naya.
Wakamkaribisha ndani. Ilikuwa nyumba ya kawaida sana. “Karibu
baba.” Akakaribishwa na baba yake mpaka sebuleni. “Asante.” Naya naye akaenda
kukaa pembeni yake. “Malon umekula?” Bale akamuuliza. “Tena kweli. Hajala.
Alikuwa akinipikia uji, ndio nikazidiwa.” Naya aliropoka tu, akashangaa wote
kimya. Naya akajishtukia. “Umepika nini Bale?” Akajirudi kwa haraka. “Kumbe ulikuwa
Morogoro!?” “Acha maswali ya ajabu wakati ulimsikia Malon alikwambia amekuja
leo. Wewe sema umepika nini, Malon ale akalale.” “Wali, maharage na mboga za
majani.” Bale akajibu. “Akuletee? Bale anajua kupika vizuri sana. Utapenda.
Usiondoke bila kula. Usiku umeendelea sana. Utaishia kulala bila kula.” Naya akabembeleza.
Wengine wakisikiliza.
“Kalete sasa Bale. Unashangaa nini?” Mama yake akamshtua.
“Nilitaka kujua kama atapenda mama.” “Wewe nenda kapashe moto, ulete.” “Na Naya
amekuwa anatapika sana. Labda ajaribu kula na yeye.” Malon akaongeza. Naya
akasimama. “Wewe kaa tu, watakuletea chakula hapo hapo.” Baba yake akamtaka
Naya arudi kukaa. Kikaletwa chakula. Wakala. Malon akashukuru, na kuaga.
“Tunashukuru kwa kila kitu Malon.” “Asante kushukuru. Ni sawa kuja kumuona tena
kesho?” “Kutokea Morogoro!?” Akadakia Bale. Wakacheka. “Hapana. Nitakuwa
Kunduchi kwa muda.” “Aaaha! Ndio huko ulikompikia uji Naya?” Bale akauliza
tena. “Usimjibu mwaya Malon. Nenda zako.” “Kwani naongea na wewe Naya? Eti Malon?”
Malon akacheka. “Ndiyo Bale. Ni nyumbani kwangu pia.” Malon akajibu huku akicheka
kidogo. “Kwa hiyo unaishi Moro na hapa?” “Zaidi Morogoro. Sasa hivi nimekuja
hapa sababu ya ugonjwa.” “Wa Naya!?” Bale akadakia kwa mshangao mkubwa sana,
nakufanya kila mtu acheke. Malon akasimama.
“Karibu tu. Wakati wowote karibu.” Baba yake Naya, akamjibu Malon.
Hilo likamfurahisha Malon. “Nashukuru. Basi nitarudi tena kesho. Naamini
sitapotea.” “Kama utaona panakuchanganya, ukifika kituoni piga simu, kina Bale watakufuata
tu.” “Nashukuru.” Malon akamtizama Naya. Naya akaelewa. “Twende nikusindikize.”
Wakatoka.
“Pole na samahani Malon. Najua ulikuja kwa ajili yangu. Ungependa tukae wote.” “Lakini wewe ulitaka baba ndio akuhudumie.” Malon akamalizia, Naya akacheka kwa aibu. “Na wewe kina Bale wameshakuambukiza?” “Umenitoroka Naya!” “Nahisi napaniki nikiwa mgonjwa. Nitabadilika. Wakati mwingine nitakuwa na wewe tu. Nenda kapumzike, tutawasiliana.” “Nije kesho saa ngapi?” “Muda wowote ule.” “Hata asubuhi!” “Hata asubuhi ni sawa.” “Wazazi hawatakuwa na tatizo?” “Hivyo ulivyowaona, ndio wako hivyo hivyo. Na kwakuwa umetaka kufika nyumbani, mama atajua wewe sio muhuni wa mtaani. Atakuheshimu. Mama ndio mkali sana kwangu.” “Afadhali. Nilete nini sasa?” “Huna haja yakuleta kitu. Si unakuja kuona mgonjwa?” Malon akacheka, nakumbusu kidogo tu. “Nenda kalale. Nitakuona kesho.” Wakaagana.
Naya akarudi ndani. “Malon ni nani?” Mama yake akamuuliza kabla
hata hajakaa chini. “Ananipenda sana Malon. Na ananifuatilia kupita kiasi.
Alianza muda kidogo, tokea muhula uliopita. Nilikutana naye kwenye kazi zangu.
Hajui jibu la hapana. Yupo tayari kusubiri ilimradi tu yeye awepo kwenye maisha
yangu. Mimi nilikuwa nimelala hosteli, nikashtukia ananiamsha, ananiambia
ameambiwa ninaumwa. Nikamwambia natapika sana. Ndio akanichukua. Majuzi tu,
amenunua nyumba Kunduchi. Kama week mbili zilizopita mimi na wenzangu
tulikwenda kufanya kazi hapo kwenye sherehe ya uzinduzi. Nikakutana na wazazi
wake.”
“Na hapo nilikuwa nimeshamkataa. Kumbe alishanitambulisha mpaka
kwa wazazi wake! Nikiwa nafanya kazi na wenzangu, hata sikua najua kama pale ni
kwake, akanifuata jikoni, niende nikasalimie wazazi wake. Nikasita, nikiwa
sitaki anitambulishe kwa wazazi wake, nikiwa sijamkubali. Hapo hosteli
wanamgombania sababu ya pesa zake. Yeye amenikazania mimi. Mimi nilishamwambia
siwezi kuwa kwenye mahusiano sasa hivi nina mambo mengi, hasa shule.” Naya
akaendelea huku wazazi wake wakisikiliza na kina Bale.
“Turudi kwenye ufunguzi wa hiyo nyumba. Ndio akanishika mkono
mpaka kwa wazazi wake, akawaambia tu huyu ndio Naya. Kumbe wananifahamu. Basi
mimi siku ile baada ya kazi iliyonipeleka pale kuisha, nikaondoka zangu,
sikutaka hata kukaa. Na hapo nilikuwa nimebadili namba ya simu kwa ajili yake.
Sikutaka mawasiliano naye. Akaniomba tena namba mpya. Mimi nikamkatalia. Yaani
baba, huyu Malon anakuwa kama amechanganykiwa na mimi! Hata sielewi. Nikiwa
nimemkataa na kumpiga marufuku asinitafute tena, na nikafanya juhudi hata
yakubadili namba ya simu, eti siku ya birthday yangu akamtuma dada mmoja wa
pale pale hosteli aniletee maua, kadi na hii cheni.” Naya akaitoa ile cheni
kutoka ndani ya gauni alilokuwa amevaa.
Mama yake akasogelea.
“Si dhahabu hii?” “Dhahabu. Na kidani hiki. Hajui jibu la hapana. Namwambia kwa
nini asichukue wasichana wanaomng’ang’ania pale hosteli. Mimi nina malengo
makubwa sana mbeleni, anasema yupo tayari kusubiri. Hivi leo alinilazimisha
niondoke naye akaniuguze mpaka nipone ndio anirudishe hosteli. Akaniambia
nikikataa, yeye anahamia hapo hosteli aniuguze.” Wakacheka.
“Anaonekana ni kijana muungwana.” Baba yake akaongeza. “Mkorofi
huyo, ni kwangu tu ndio mtulivu.” “Labda anakupenda kweli.” Mama yake akaongeza
huku akiangalia ile cheni. “Hilo sina mashaka nalo. Ananipenda, na hawezi
kujisaidia. Namfukuza, namkataa, utashangaa baada ya muda anatokezea tena!
Halafu mtoaji sana. Mpaka utamuhurumia.” Wakatulia. “Sasa nifanyaje baba?”
“Nenda naye taratibu tu. Utakuja kujua kama ni mwanaume wa kuoa kweli au la.”
“Mbona ashasema labda nife au yeye afe! Amesema lazima anioe mimi.” Wakacheka.
“Na usifikiri anatania! King’ang’anizi kupita kiasi.” Wakacheka. “Wewe unampenda?” Baba yake akamuuliza. Wote wakamgeukia. “Maana asije akajaa kwenye maisha yako akakunyima uwezo wakufikiria.” Baba yake akaongeza. “Nafikiri nampenda Malon. Kila nikimfukuza, akiondoka, huwa natamani arudi.” Wakacheka tu na kuendelea kuzungumza.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kesho yake mida ya saa
nne, Malon akarudi tena nyumbani kwa kina Naya. Akaambiwa Naya amerudi kulala,
dawa zinamlevya. “Ameweza kula?” “Amekunywa uji. Na hajatapika tena. Atakuwa
sawa tu. Unaweza kurudi tena baadaye.” Mama yake Naya akamjaribu. “Naweza
kumsubiria? Kama ni sawa lakini.” Malon akaongea kwa heshima. “Haina shida
kabisa. Karibu ndani nikuonyeshe alipo.” Akafurahi sana kukaribisha na mama
yake Naya mpaka chumbani kwa Naya. Wakaingia chumbani kwa Naya. Alikuwa amelala
hana habari. “Naamini atapona tu. Vipi homa?” “Baba yake alimpima kwenye saa 12
asubuhi, ilikuwa juu. Akampa dawa.” Malon akamuwekea mkono kichwani. Anaonekana
hana joto kali.” Mama yake akatoka kuwapisha.
Malon alishinda hapo mpaka usiku. Alikula hapohapo. Hakuchagua
wala kujivunga. Kila alichopewa alikula. Na kesho yake pia siku ya jumapili
akarudi. Lakini safari hii alirudi na mboga mbalimbali. Nyama ya ng’ombe na
samaki wengi. Bale alishinda akikaanga na kuwaweka kwenye friji na wengine
kugandishwa. Jumatatu alirudi Morogoro. Hawakumuona siku hiyo nzima. Naya akawa
anamalizia dozi yake siku hiyo ya jumatatu. Akawaaga wazazi wake kuwa lazima
jumanne, arudi shuleni. Ni kweli alikuwa kwenye kipindi cha mwisho chakumaliza
shule. Ilikuwa lazima ajikaze shule iishe. Siku ya jumanne asubuhi Naya
alipomaliza kujiandaa, wadogo zake wakiwa wamekwenda shule na mama yake kazini,
Malon akarudi.
Baba yake Naya akajua ndio amekuja kumchukua. Wakazungumza kidogo.
Baba yake akimsihi apunguze kazi ili atulize mawazo shuleni amalize shule.
“Labda umwambie wewe baba. Mimi alinikasirikia kwa muda mrefu sana sababu ya
kumpa huo ushauri.” “Wewe ulitaka niache kabisa Malon. Mimi nategemea ile kazi
kwa vitu vingi.” “Yule mama nimuelewa Naya. Nimezungumza naye, anaonekana
anakupenda na anakuhitaji. Muombe upumzike kazi mpaka umalize mitihani ndipo
uendelee na kazi. Nina uhakika ataelewa tu.” “Nitaishije sasa?” “Naya!” Malon
akamshangaa. “Basi nitampigia simu nizungumze naye.” “Umeahidi mwenyewe Naya.
Tena mbele ya baba. Lazima utekeleze.” “Basi hapo Malon umepata sababu.” “Sio
sababu. Tulia umalize mitihani. Kazi zipo na utafanya mapaka mwenyewe uchoke.”
“Ni kweli anavyosema Malon. Umebakisha padogo sana. Jikaze umalize vizuri.”
Naya akanyamaza. Wakaaga na kuondoka.
“Asante kwa kuniuguza Malon. Nimefurahi.” Malon akacheka. “Lakini
umeniumiza kuwa na mahusiano na Lulu.” “Si wewe mwenyewe ulinielekeza kwake?” “Sasa kwa
nini umenirudia?” Naya akaanza kulia. “Nakutania Naya. Sikuwa na mahusiano naye.
Ilibidi kuwa naye karibu ili niwe karibu na wewe Naya. Ulinikimbia na kubadili
namba ya simu! Ulitaka nifanyeje?” “Kunifuata mimi mwenyewe sio kwenda
kulala na wanawake ili kunifikia mimi! Umeniumiza Malon. Umeniumiza sana.” “Ila na yeye
tokea mwanzo alijua nipo naye ili niwe karibu na wewe. Anajua kama nakupenda.” “Inasaidia
nini wakati umeshamvua nguo! Heshima ipo wapi sasa?” “Acha
kuzungumzia hayo mambo Naya. Naomba tusirudi nyuma. Nimeomba msamaha. Nakwambia
nilikuwa kama nimechanganyikiwa! Natapatapa sijui chakufanya.” Naya akanyamaza.
“Naya?” “Naomba nirudishe hosteli.” “Usianze Naya. Usianze
tafadhali. Nichukie, nifanye chochote unachotaka, lakini tuwe wote tu.
Umeshajua huwezi kunikwepa tena. Hata ufanyaje, ujue mimi nitakufuata tu.”
“Nipe muda wa kukasirika Malon!” “Sio mbali na mimi. Wewe kama umeamua
kunikasirikia, uwe na mimi.” “Sasa ndio inakuaje?” “Wewe ambaye hujui kusamehe,
ndio utafute hiyo njia Naya. Mimi sijui. Ila ujue mimi nitakufuata popote
uendeko.” Naya akamwangalia asiamini.
“Hivi wewe unafikiri ni kwa nini nimenunua nyumba Dar wakati
naishi Morogoro?” “Mimi sijui Malon.” “Kwa ajili yako. Ili niwe karibu na
wewe.” Naya akamtizama na kunyamaza. “Nakupenda Naya. Mimi siko hivi kwa
wanawake. Ni wewe tu.” “Sasa kwa nini hutulii?” “Naya! Nilikuwa na wewe tokea
ijumaa. Unataka nifanye nini?” “Usilale na wanawake wengine.” “Ila wewe tu?”
Naya akaona hapo pagumu. Akanyamaza. “Naya?” “Mimi nimebakisha muda mfupi
nianze mitihani Malon. Nahitaji kutulia shuleni. Nirudishe hosteli.” Malon
akamtizama.
“Nini?” “Unaniringia Naya! Na umekusudia kunitesa tu.” “Kwa nini
unasema hivyo Malon? Ulitaka nifanye nini? Mimi nimetulia na wewe.” Malon
akafurahi sana. “Hata tulipotengana, sijakimbilia kwa wanaume wengine. Au
umesikia nina mwanaume?” “Ila Ino alikufuata mpaka hosteli.” Naya akashtuka
sana. “Malon!” “Wewe ulifikiri nitatulia tu nisikufuatilie? Nataka kujua kama
ahadi uliyonipa unatunza au ndio uliondoka siku ile na kuvunja kila kitu.”
“Sasa hao wapelelezi wako wamekwambia nini?” Malon akacheka.
“Kwani wewe mmekubaliana nini na Ino?” “Nilikwambia juu yangu na
Ino. Na hakuna kilichobadilika.” “Basi twende nyumbani kidogo, halafu
nitakurudisha hosteli. Kuna kitu nataka kukupa.” “Nini?” “Tulia basi Naya
wangu.” “Umeniudhi Malon.” “Bado upo na Lulu tu!?” “Sasa je?” “Naya, jifunze
kusahau mpenzi wangu. Utahangaika na Lulu bure ambaye sina hata mpango naye.
Wewe ndio mke wa Malon, wengine wote wezi tu.” Naya akaguna na kugeukia
dirishani.
Malon akacheka. “Nilikuwa na hamu na wewe Naya!” “Hata mimi
nilikuwa nakukumbuka, Malon.” Malon akafurahi kusikia hivyo. “Twende mpenzi
wangu tukatulie kidogo ndio nikurudishe hosteli.” “Utanikumbatia?” Naya akuliza
taratibu. “Sana. Mpaka niridhike.” Naya akacheka. Wakatulia. Naya akajirudisha
nyuma, nakupitiwa na usingizi. Alishtuliwa na Malon kuwa wamefika. “Nalala
sana!” “Dawa bado zipo mwilini. Twende
nikukumbatie ulale mpaka usingizi uushe, ndipo nikupeleke hosteli.” Naya
akacheka kidogo. “Twende.” Akamfungulia mlango, akashuka.
Walielekea moja kwa moja chumbani, Naya akaenda bafuni ndipo
akarudi kitandani alipokuwa amejilaza Malon. “Vipi?” “Nipo sawa. Nilikuwa
nabadilisha.” Malon akaelewa. Naya akapanda na kujisogeza karibu. “Hizi ni
funguo zako za hapa. Muda na wakati wowote unaojisikia unataka kuja kupumzika,
unaweza kuja tu. Nitazungumza na walinzi.” Naya akashtuka kidogo. “Malon!” “Ni
kwangu Naya. Na sina mtu wakuja kuishi hapa isipokuwa mimi na wewe. Unaweza
kuwa unatamani sehemu tulivu, hapa patakufaa. Hakuna atakayekusumbua.” Naya
aliipokea ile fungua akabaki akiitizama. “Unafikiria nini tena?” “Sikutegemea. Asante.”
“Karibu.” Naya akainama na kuanza kumbusu.
“Nakupenda Naya.” “Najua Malon. Asante.” Akamsogeza karibu akajilaza, akamlalia pembeni. Malon akaanza kumpapasa taratibu. Huku akirudia kumbusu mara kadhaa shavuni. “Malon!” Naya akamwita taratibu tu. Akambusu na kuitika. “Na mimi nakupenda.” Malon akacheka. Akamgeuza upande wake, kutoka vile alivyokuwa amempa mgongo, akaanza kunyonya midomo yake. Shingoni, midomoni. Naya alikuwa akisikia raha ya ajabu. Malon alimchezea kwa muda mrefu, alivuka mipaka mpaka kifuani. Akaishia kwenye matiti hayo ambayo hayakuwahi hata kuonyeshwa mwanaume. Alicheza hapo akiyanyonya na kuyashika taratibu, mwishowe akamuachia taratibu kwa kurudi mdomoni. Maana hali yao wote ilikuwa mbaya na Naya alikuwa bado kwenye siku zake. Wakabaki wanapeana mabusu ya mdomoni. Malon akamfunika shuka, lakini mkono mmoja uligoma kutoka kwenye titi la Naya. Wakabaki wametulia, Naya akapitiwa na usingizi mkono wa Malon kifuani.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Malon alianzisha jambo mwilini kwa Naya, Naya akabaki akimfikiria.
Mitihani ilikuwa karibu na Malon alishamwambia atulize mawazo shuleni. Watapata
muda mzuri akimaliza mitihani. Lakini ilikuwa shida kwa Naya. Alikumbuka midomo
ya Malon kwenye matiti yake na vile alivyoweza kucheza na chuchu zake. “Utakuja?” Naya
akauliza kwa upole. Ilikuwa imeshapita juma moja tokea walipopata muda huo
nyumbani kwa Malon, Kunduchi. “Wewe unajua ukinihitaji nitakuja Naya. Ila nilitaka utulize mawazo
shuleni. Umebakiza muda mfupi mitihani ianze.” Naya akatulia. “Naya?” “Nina hamu na wewe
Malon.” “Basi nakuja.” Malon naye akawa kama amechanganyikiwa na Naya. Akiitwa tu,
anaweka kila kitu chini, anachukua funguo za gari, safari ya Dar inaanza.
Naya alitoka kwenye kundi la kujisomea, hajaelewa chochote. Akili zilikuwa kwa Malon, amtoe nguo na kumnyonya kama livyomfanyia mara ya mwisho alipokuwa naye. Akarudi hosteli kwenda kuoga na kujiweka tayari kwa ajili ya Malon. Baada ya kama masaa mawili na madakika kadhaa, Malon akawa ameshafika. Kama kawaida akaingia ndani kumfuata. Naya akacheka alipomuona. “Nimefurahi umekuja.” Malon akacheka. “Twende.” Bila kupoteza muda wakatoka. Bila maswali mengi, Malon akakanyaga mafuta mpaka Kunduchi, nyumbani kwake. “Leo nitalala. Na nimebeba madaftari ya kujisomea asubuhi. Usiku nita.. ” Malon akamsogelea, akamkumbatia na kuanza kumbusu.”
Chuoni Mzumbe.
N |
aya akacheka
peke yake akiwa bado amekaa hapo chuoni akikumbukia mwanzo wake na Malon.
Akajishika midomo yake. Akainama akiwa peke yake na tabasamu. “Malon anajua..” Akiwa mawazoni akashtukia busu la kichwani.
Akashtuka sana. Kugeuka alikuwa Malon. “Malon!” Akasimama. Malon akamvuta
karibu na kumbusu. “Vipi? Mbona umekaa hapa peke yako?” “Tulikuwa mapumzikoni.
Watu wanakula, tuingie kipindi cha mwisho. Mbona upo hapa?” “Nimekukumbuka,
nikaona nije kukuona.” Naya akamwangalia na kucheka.
“Nini sasa? Nimemaliza shuguli zangu mapema, nikaona nije tu.
Nimekuletea chakula na zawadi. Ipo kwenye gari.” “Sasa umejuaje kama nipo
hapa?” “Nimeuliza, nikaambiwa walikuona umekaa hapa. Unawaza nini?” Naya
akafikiria kidogo. “Nini?” “Nilikuwa nakumbuka tulivyaanzana Malon. Ulikuwa
ukinipenda karibu kuchanganyikiwa na mimi.” “Bado nakupenda Naya.” Naya
akacheka kwa kuguna.
“Mtu angeniambia kipindi kile kama unaweza au ungekuja kunipiga,
au ukaendelea kuwa na wanawake wengine!” “Kwa nini husahau Naya? Nimeomba
msamaha mara nyingi tu.” “Msamaha hauondoi kumbukumbu Malon. Na unayoyafanya ni
matukio yakurudia. Utalala na huyu, nikijua, unaomba msamaha, unatulia au labda
unaendelea kwa siri, mpaka najua tena.” Malon akanyamaza.
“Ulinionyesha upendo wa ajabu sana Malon! Sikuwahi kufikiri kama
mwanadamu anaweza kumpenda mwanadamu mwenzake kwa kiasi kile. Na tulikuwa na wakati
mzuri sana. Ulinifanya nikatulia, na ninakiri wewe ndio uliyenifanya nifaulu
kidato cha sita kwa kiasi hiki japo ulishaanza kuniumiza, ila ulinifanya
nitulie Malon. Mbaya sana ni unakuwa ukinisaliti katikati ya wakati mzuri.
Tunakuwa tumetulia, kuna amani na utulivu, ndipo unapoanza mambo ya ajabu.
Najiuliza kuna kuwa na nini? Au ni nini kinakupelekea kuanza kulala na wanawake
wengine? Unakuwa hutosheki au inakuwa ni nini! Najiuliza na kuumia sana.”
“Nimekuahidi haitatokea tena.” Naya akamwangalia kwa kumsuta.
“Mbona huniamini?” “Kwa kuwa hii sio mara yako ya kwanza Malon! Huwa
unashindwa kusimamia hiyo ahadi yako. Upo jasiri kwenye kila kitu, lakini
dhaifu sana linapofika swala la wanawake.” “Naya! Umeanza kunitukana, wakati
mimi nimekuja hapa kwa upendo tu. Leo ni alhamisi. Najua kesho nakuja
kukuchukua hapa, turudi nyumbani. Lakini nipo hapa kukuona tu. Nimeacha kila
kitu kwa ajili ya kukuona tu!” “Sijawahi kuwa na shaka na upendo wako kwangu
Malon. Hata mara moja. Kweli unanipenda. Lakini huthamini tulichonacho. Sasa
sijui ni kwa kuwa nimekuhakikishia sana uwepo wangu!?” Kimya Malon hakujibu.
“Ila Malon, sitavumilia hivi daima. Safari hii ukiamua kumvulia
nguo mwanamke mwingine, ujue ndio umeachana na mimi kabisa. Na sitabadili
mawazo. Tafadhali naomba jihadhari. Nitakuacha nikiwa nakupenda Malon, lakini sitakuwa
na jinsi mpenzi wangu.” Malon akavuta pumzi kwa nguvu, akanza kuondoka. Naya
akamfuata nyuma mpaka kwenye gari.
Kweli alikuwa ameleta vyakula. Alikuta na soda mbili. Inamaana
alitaka wale pamoja. “Umekula?” Naya akamuuliza baada yakumuona amerudi kwenye
gari ametulia kimya kitini. “Hapana Naya. Nilitaka tule wote. Lakini umenijaza
tumbo na maneno!” “Nataka ujihadhari Malon. Unajua nakupenda sana mpenzi
wangu.” “Lakini unanitisha sana Naya!” “Sikutishi. Nakwambia ukweli na
ninatamani uwe umenielewa na usirudie. Kwa kuwa utakaporudia, utakuwa
umeniambia wazi kuwa umechagua kuendelea na maisha yako au tabia zako, sio
mimi. Namuomba Mungu mchana na usiku unichague mimi Malon.” “Nimekuchagua wewe
Naya. Naomba uniamini. Huoni tumekuwa na wakati mzuri?” “Ni kweli tumekuwa na
wakati mzuri sana. Hata mimi nimefurahi na ninakushukuru. Asante.” Malon
akabaki akimwangalia.
“Nakupenda Malon.” “Najua sana Naya. Na asante.” Malon akavuta
mfuko. “Zawadi yako ipo humo ndani.” Naya akacheka nakupokea. “Asante.” Alikuwa
amesimama dirishani, upande ule wa dereva alipokuwa amekaa Malon. Akamshika Maloni
sikioni, akaanza kumbusu taratibu. Wanachuo wengine walikuwa wakipita,
wanawaona. Lakini Naya hakujali.
Tokea ajirudi, Malon alimpa mapenzi ya kweli Naya mpaka mwenyewe Naya alikuwa akishangaa. Kwa kuwa Malon alikuwa akifahamika hapo mjini Morogoro, kila mtu akajua mwanaume aliyekuwa akimshusha Naya hapo chuoni alikuwa Malon. Zamani alikuwa akiishia kwenye gari, Naya anashuka. Safari hii akawa anashuka yeye na kumfungulia mlango, na kumuaga na busu juu. Siku za kumchukua Naya zikawa hazitabiriki. Inategemea na Malon au Naya. Naya akikataa kuondoka akiwa na mitihani, basi Malon ataleta chakula muda wowote. Watakaa kwenye gari, watakula pamoja, nakuondoka kumuacha Naya. Iwe mchana au usiku, hata kama Naya hataondoka naye lakini atakuja kumtembelea.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kwa kuwa walishaanza kuishi
pamoja kama mke na mume tokea Naya yupo kidato cha tano na sita, hata kipindi
cha likizo, Naya alikuwa nyumbani kwa Malon. Wazazi wa Malon, ndugu na jamaa wa
karibu na Malon wote walijua mahusiano hayo kwa undani huo, isipokuwa wazazi wa
Naya hawakujua kama Naya anaishi na Malon kama mke, ila kujua yapo mahusiano
kati yao na akimaliza chuo wataoana. Naya aliaminika sana nyumbani kwao kwa
uwezo wakuzaliwa na kuishi katikati ya jiji na kuweza kuepuka vishawishi hata
alipokuwa nyumbani hajaanza maisha ya hosteli. Kama hayupo nyumbani akibishana
na Bale, basi ujue wapo na huyohuyo Bale kanisani wakifundishwa kwaya na Ino
pamoja na vijana wengine.
Hakuwa na tamaa ya wanaume wala hakuwa akisumbua nyumbani kwao kwa
tabia za uhuni. Kipenzi cha baba na akaaminika sana kuwa anajitunza. Na kilichomvutia
hata baba Naya, ni kule kwa Malon kuongeza msisitizo kwenye elimu ya Naya. Akimtaka
akazane na shule si kazi tu. Na kweli Malon alimpenda Naya na kumtunza vilivyo.
Hapakuwa na shaka juu ya mapenzi ya Malon kwa Naya. Linapofika swala la Naya,
kila kitu huwa kinasubiri kwanza.
Maisha ya wapi wanaishi ilikuwa ikitegemeana na ratiba za Naya na
Malon. Kama Naya yupo likizo, basi atakuwa ni wa Malon kabisaa. Alipo Malon ndipo atakuwepo Naya. Alishaacha kazi
kwa Madamu Vane muda mrefu tu. Lakini akabakiwa na kisingizio cha kazi ili kudanganya
wazazi wake anakazi awapo likizo ili awe na Malon bila shida. Akadanganya pia kwa
wazazi wake kuwa nyumba ya Malon ya Kunduchi ameachiwa yeye ili aitumie itakapo
mlazimu, atokapo kazini usiku sana. Kwa usalama wake asiwe akisafiri usiku
atokapo kazini kwenye kazi za Madamu Vane kurudi nyumbani kwao Kiluvya ambako
ni mbali sana na mjini. Hilo nalo likaongeza sifa na kujali kwa Malon, nyumbani
kwa kina Naya. Kwamba anamlinda Naya vizuri. Wazazi wake wakijua kuwa ameachiwa
nyumba na Malon anayeishi na kufanya kazi Morogoro, amempa funguo za nyumba
hiyo na kumuwekea ulinzi, aishi bure kwa usalama wake Naya asiwe anazunguka
usiku akitokea kazini, kumbe huyo Malon alishaanza kula faida za ndoa tokea
Naya ni mtoto wa sekondari.
Naya akiona amekaa sana kwa Malon, atashtukiwa nyumbani, ndipo atarudi
kwa wazazi kulala hata siku mbili au tatu, kisha anarudi tena kwa Malon. Chuo kikifunguliwa,
wakidhani anaishi chuoni, kumbe nyumbani kwa Malon, Morogoro au kweli siku
chache chuoni tena endapo wanamitihani, au wamegombana tena. Wazazi wake
hawakujua linaloendelea walibaki kumpongeza Naya kwa kuweza kumudu ratiba za
kazi na shule.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Safari za Brazili na Dubai zilikuwa za kawaida sana kwa Naya na
Malon. Kukaa mtaani kwa muda mrefu kwa Malon baada ya kukataa shule, kukamsaidia
kujua mengi. Alifanikiwa kununua kibali cha kimataifa cha ufanya biashara. Alikuwa
akinunua sukari kwa bei ya chini sana nchini Brazili na kuuzia nchi kama Dubai
na nchi nyingine ambazo hazikuwa na masharti magumu. Kwa hiyo kila Naya
anapokuwa likizo, na Malon akiwa na safari, basi atakwenda na Naya.
Maisha ya Naya yakaendelea kubadilika siku hadi siku, utu wake wa ndani ulivyokuwa ukibadilishwa kwa kasi kama huo utajiri wa nje aliovalishwa na Malon. Wazazi wake wasijue kinachoendelea, wakidhani ni binti mdogo, kumbe alishajiingiza kwenye maisha ya haso za ndoa muda mrefu tu. Naya mtoto wa kanisani aliyetulia, mwadilifu, akajiingiza kwa Malon mtoto wa mtaani haswa aliyeshindikana hata kwa wazazi wake. Ngono kwake ilikuwa ni starehe kama starehe nyingine yeyote ile akijiburudisha tu. Ila Naya akiamini ni jambo la heshima sana. Linatakiwa kuwa la watu wawili tu waliokubaliana. Akafungwa ndani ya penzi zito la Malon na pesa yake ambayo ni kweli ilimsaidia Naya. Maisha ya aina hiyo yakaendelea.
Malon na Ndoto Za Naya.
K |
atika safari
hizo za nje ya nchi Naya akapata wazo la kuweka kwenye matendo kipaji chake cha
ubunifu. Maswala ya ubunifu wa mavazi kitu anachopenda na kukijulia sana. Aliona
vile chuoni alivyopata wafuasi wengi wakijaribu kumuiga kwa kila anachovaa. Kila
wakati wakimsubiria ashushwe garini au atoke chumbani kwao, aonekane amevaa
nini siku hiyo na kuwa gumzo siku nzima wakimthaminisha na wengine kujaribu kwenda
kutafuta aina hiyohiyo ya vitu vya Naya. Hicho kikamuongezea ujasiri. Akataka kubuni
na kuuanza kujitangaza yeye kama Naya, na kuwauzia watu. Binti huyo mwanafunzi
wa masoko, akajua biashara matangazo. Ili kujulikana na kufikia wengi ni lazima
kufanya maonyesho ya mavazi.
Akamshirikisha Malon, kwa kuwa ni kitu anachokipenda Naya, Malon akakubali
bila shida tena kwa haraka sana. Na kwa kuwa pesa ya Malon ilikuwepo utekelezaji
wake hata Malon hakuona kama utasumbua, pesa ipo ni kutendea kazi tu. Na kwa
kuwa Malon alikuwa akifahamika sana hapo mjini Mororgoro, Naya naye akafahamika
kwa haraka sana hapo Morogoro kama mwanamke wa Malon. Kwa hiyo haikuwa shida
kuzungumza na yeyote anayemtaka. Na jijini Dar napo ikawa rahisi. Kazi
aliyokuwa akifanya tokea kidato cha nne, ilimkutanisha na wengi. Kwa hiyo
akajua haitakuwa shida kufikia ndoto zake.
Akafikiria kitu mashuhuri nchini Tanzania ambacho hakitagharimu
wengi na kila mwanamke wa kitanzania anatumia. Tajiri kwa msikini. Wazo likamjia
kuwa ni khanga. Akawekeza muda wakutosha kwenye kuandaa hilo. Akaanza kwa michoro.
Akichora mitindo mbali mbali. Huku akiwa tayari na picha ya warembo atakao
watafuta wakipita jukwaa siku ya tamasha lake. Nini anataka wageni wake waone
na kufurahia! Hiyo ikamuongezea hamasa na ari kwa kuwa alishaona mwisho tokea
mwanzo.
Wakati akiendelea kuchora, huku anaandaa mipango ya idadi ya
warembo atakao hitaji siku hiyo. Kuanzia wembamba sana, umbo la kati na wanene
kiasi mpaka wanene kabisa. Ikaanza kazi ya kuwatafuta na kuandaa mitindo
aliyobuni yeye mwenyewe. Kokote alipokuwa hata mapumzikoni na Malon, basi
utamkuta akiwa peke yake akichora na kuweka mipango yake. Katika hilo Malon akazidi
kumpenda na kumuheshimu sana Naya.
“Kwani unataka watu wangapi?” Malon akamuuliza. “Kwa kuwa ndio ninaanza,
nataka wasichana 12 tu. Niwafundishe mwenyewe, ndipo niwaweke jukwani. Sitaki
wajuaji sana kama kina Tula. Watanisumbua. Nataka wasichana wakawaida ambao
wataweza kunisikiliza na kuelewa kwa haraka, lakini pia sitaki washamba sana.”
Malon akacheka. “Na kwa kuanzia, kila mmoja nataka apite na mavazi yasiyopungua
matano.” “Tofauti!?” Malon akashangaa sana. “Mbona nimeshafikisha mitindo 53
tofauti! Nitafika tu mavazi 60. Naanzia Dar, nitafanya na Morogoro. Mwitikio
ukiwa mkubwa, nitafanya na mikoa mingine. Baadaye nataka nifungue sehemu yangu
ya kushonea. Watu ambao watatengeneza nguo nitakazobuni mimi mwenyewe, na
ziuzwe kwa jina langu.” Malon akakaa sawa na yeye akiwa amesha hamasika.
“Vyote vinaweza kuanza pamoja Naya. Tena wakati unafanya hayo
maonyesho, unawaelekeza watu kwa mafundi wako.” “Kweli Malon!?” “Kabisa. Hakuna
kupoteza kwenye kuwekeza. Kwani kinachohitajika ni nini? Si eneo tu?” Malon
akauliza kama kitu kidogo sana. Naya akaanza kuona ndoto zinaweza kutimia
mapema zaidi ya alivyotarajia. “Unakumbuka tulivyokuwa China tulienda
kutembelea wale mafundi wanaotengeneza nguo? Ukauliza wanafanyaje? Wakakwambia
wanapokea vipimo kama hivyo kwa njia ya mitandao tu. Mtu anachagua nguo online.
Anatuma vipimo au anachagua vipimo vyake hapo mtandaoni na pesa, anatengenezewa
na kutumiwa. Au kubuni zaidi jinsi yakuwahudmia kirahisi. Hakuna kupoteza
kwenye kuwekeza. Tufikirie kufungua sehemu ambayo tutaweka mashine za kisasa za
kushonea na kuajiri mafundi. Tunafanya hayo maonyesho ya mavazi ili kujitangaza
kwa wengi, na kuhakikisha kila anayetaka vazi fulani analipata kwa haraka, tena
kutoka kwa mafundi wako. Na kwa kuwa unakipaji cha mitindo kizuri na chatofauti,
kwa muda mfupi sana utakuwa mbali mno.” Naya akafurahia hilo wazo, maana na
Malon mwenyewe alijiunganisha na hilo wazo kumuashiria atasimama naye.
“Sasa eneo?” “Kwa kuwa wewe utengenezaji wako nguo utakuwa tofauti.
Tutafute eneo kubwa. Hata shamba tu. Tujenge hapo lijengo likubwa tu kama godauni.
Tuweke mashine za kisasa kama nilivyokwambia na tutafute watu.” Naya akaona
faida ya kutoka na mtu kama Malon. Mwenye pesa na akili yakuwekeza. “Basi ngoja
nimuombe baba atutafutie eneo hata maeneo ya mbele ya Kibaha. Tutapata kwa bei
nzuri.” “Sawa tu.” Malon akakubali bila shida. Kwa kuwa alishaishi na Naya,
akaujua moyo wake na tabia zake. Na alijua kwa hakika atamuoa tu, akajua hapotezi
atakapowekeza kwake. Hakufikiria hata mara mbili. Kwanza akafurahia kupata
mwanamke kama Naya.
Naya akampigia simu baba yake wakiwa nchini Dubai, akamueleza
mipango yake na mawazo ya Malon. Baba yake akampongeza sana na kumuahidi kutoka
muda huo kwenda kusaka eneo. Na kweli, kabla ya kurudi nchini, baba yake Naya
akawa amepata eneo zuri tu, maeneo ya Picha ya ndege, karibu tu na Kibaha.
Alipokutana na mwenye hilo eneo na kumpa bei, akampigia simu Naya kumjulisha.
Malon aliposikia bei, akakubali na kuzungumza na mwenye kiwanja kuwa atakwenda
kumuona watakaporudi nchini.
Baada ya siku 4 mbeleni, Malon na Naya waliporudi nchini, wakaelekea Picha ya ndege kuonana na muuza lile eneo. Walifuata taratibu zote za manunuzi. Bila kupoteza muda, Malon na Naya wakaanza kufuatilia hati ya lile eneo. Ikawa chini ya jina la Malon na Naya. Akili za Naya, zikahamia kwenye ujenzi wa lile eneo huku akiendelea kutunza mitindo yake aliyokuwa akibuni yeye mwenyewe.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Sasa ili asipoteze wateja au umaarufu mjini kwa kuwa alishaacha
kazi za waitress kwa Madamu Vane, Naya akafikiria kufanya kitu cha kumjengea
jina mjini na kumsogeza karibu na watu. Akapanga kila mwisho wa mwezi, kukutanisha
watu mbali mbali kwa lengo tofauti tofauti. Akafikiria wakati mwingine akutanishe
wanawake tu, akitaka kuwafanyia maonyesho ya vipodozi mbali mbali atakavyokuwa
anavitoa Dudai na nchi nyingine atakayokuwa akipata kwa bei nzuri na kuja
kuwauzia nchini. Au Perfume za kike na kiume. Hapo akapanga kuwe na kula na
kunywa na kuwatafutia wageni wake viburudisho mbali mbali. Auze bidhaa mbali
mbali. Viatu, pochi na kadhalika. Na hakutaka kuwe na watu wengi. Malengo ni
kwa watu wachache na wenye pesa. hilo nalo likafanikiwa, Malon akiwa nyuma yake
kumuunga mkono.
Naya alikuwa mtoto mdogo lakini mwenye akili iliyomshangaza mpaka
Malon akajua hata akifilisika kwenye biashara zake, basi anaye mwanamke
wakumuinua. Hapakuwa na swali kama ni watu waliokusudiwa kuwa pamoja au
wanaofaa kuwa pamoja. Walikuwa wakiendana kwenye mawazo ya kibishara na
kuungana mkono. Na huo mpango Malon akaukubali bila shida. Naya akaanza kufanyia
kazi mawazo yake. Akaanza kufanya tafrija ndogo ndogo mjini. Akisaidiwa
kutafuta kumbi kwa bei nafuu na Madamu Vane. Basi atapatengeneza na kualika
watu aliowakusudia kwa wakati huo, anauza vitu. Warembo wote aliokwisha fanya
nao kazi na marafiki wa marafiki zao Naya akawatafuta. Basi na kwa kuwa alijua
ni nini warembo wa mjini wanataka, na wanawake wenye pesa, Naya akawa akiingiza
bidhaa hadimu. Hana duka. Analeta vitu. Anauza kwenye tafrija anazokuwa
akiandaa. Anamaliza na kubuni kingine na shule ikiendelea na ujenzi kupamba
moto.
Mahusiano yake na Malon yakawa yameongezeka, kutoka kuwa tu wapenzi, mpaka kuwa wawekezaji wa pamoja. Kila faida aliyokuwa akipata ya ziada, alijitahidi kukumbuka kwao, hasa baba yake. Hakufanya kitu bila kumshirikisha baba yake aliyekuwa anajiona ni kama alijizaa pale kwa Naya. Akili ya kufikiria na kuchukua hatua.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Alimnunulia baba yake gari nzuri tu kutoka kwa mtu aliyekuwa
akiuza kwa bei nzuri pia, aina ya pickup. Ikawa msaada sana kwenye biashara ya
baba yake. Kubebea mayai na maziwa kusambaza mjini. Pesa ya Malon, wazo kutoka
kwa Naya. Wadogo zake pia aliwashirikisha kwenye mambo anayofanya. Naya na
familia yake wakaanza kuinuka kiuchumi. Hakuna kukopa hovyo tena. Naya alijua
nini kinahitajika kwao, basi hakuacha kumsaidia baba yake.
Malon na Naya wakazidi
kupanuka na kujulikana kwa bishara. Morogoro sababu ya Malon, watu walijazana
kwenye matamasha yao. Dar sababu ya Naya. Ungependa uwaone pamoja. Walijua
kuvaa. Walijua kuungana mkono kwenye mambo yao. Akisimama Naya, ujue Malon na
Chezo wapo nyuma yake. Mwili wa Malon, ulivutia kutizama alichoweka. Na Naya
alijua kujipangilia haswa. Mtoto huyo aliyekuwa akiimba kwaya kanisani na
kwenye matamasha ya dini, hakupata shida kusimama mbele ya watu na kunadi
bidhaa zake. Akajibeba kimwanamtindo haswa, ukichanganya na akili na ubunifu aliojaliwa
na Mungu, sura na umbile lake, lazima ufurahie kuwa kwenye kila tamasha
wanaloandaa.
Shule nayo ilikuwa ikiendelea, huku maisha ya nje yakiendelea. Na
kwa kuwa alikuwa na mama mwalimu wa shule ya msingi, Naya alikuwa akitamani
kulia. Utafikiri mwalimu anayemsimamia mwanafunzi na kiboko. Neno shule,
lilikuwa kila wakati mpaka Naya alikuwa hataki kumpigia simu mama yake mara kwa
mara. “Fanya mambo yako weee, lakini uniletee cheti hapa nyumbani. Wajukuu
wanaweza kusubiri mpaka shule iishe. Lakini wakitokea hapo njiani, niletee
nilee mwenyewe, shule hiyo iishe Naya.” Alimkera kwa hayo maneno kila
anapomuona Naya. Hata kama akimpa habari njema kuwa amefanikiwa kwenye tamasha
fulani, au jengo lao linaendelea vizuri kwenye ujenzi, basi mama yake lazima
atamalizia kuwa anataka cheti kizuri nyumbani. Basi Naya hakuwa na mapumziko.
Akiwa shule, basi akili zinakuwa shule. Na anapokuwa nyumbani, kwenye mambo
yake anakumbushwa na shule. Akawa busy kupita kiasi.
Wakati anamaliza mwaka wa pili, Malon naye akawa amemaliza ule
ujenzi huko Picha ya Ndege. Lilikuwa tu kama godown, lenye ofisi 4, mlemle
ndani. Zilitenganisha na mbao chini, vioo juu. Ofisi ya Meneja ambaye ndio
Naya. Malon naye akajiwekea ofisi yake yeye mwenyewe Malon. Ofisi ya masoko.
Ofisi hiyo ya mtu wa masoko aliifanya kubwa kidogo. Kukawekwa meza tatu.
Alimwambia Naya, wanahitaji mtu ambaye atakuwa akitafuta wateja, mtu wa kupokea
kazi kutoka nje na ndani ya nchi, na mtu ambaye atakuwa akiandaa hizo oda
kutokana na tarehe alizopokea, na kupeleka kwa watendaji pamoja na ofisi ya
wafanyakazi wa stoo. Napo kwenye hiyo ofisi palikuwa pakubwa tu kwa ajili ya
mtu wa kutoa oda ya malighafi. Kumwambia Naya na Malon ni nini chakununua na
usafirishaji wa nguo za watu na kupokea kutoka kwa mafundi.
Naya alifurahia kila kitu kwenye lile eneo. Walirudi China tena
kwenye kiwanda wanachotaka kuwaiga. Wakatumia muda hapo kujua ni vipi wanafanya
na aina gani za mashine. Malon akanunua vitu kama vile walivyoona kwenye hicho
kiwanda. Wakati huo nchini Tanzania mama yake Naya akiendelea kutafuta mafundi
wazuri ambao bado hawajawa maarufu sana. Tena alitafuta wale mafundi wa kawaida
tu wanaoshona nje ya nyumba zao. Akazungumza nao. Naya alitaka wawe 10 tu kwa
kuanzia. Ili aweze kuzungumza nao na kuwafundisha ni nini anataka kutoka kwao.
Waliporudi nchini, walikuwa wameshazungumza na Malon juu ya malipo
kwa hao mafundi. Badala ya kulipwa kwa nguo, Malon na Naya, wakawaahidi
mshahara kabisa na marupurupu kama chakula cha mchana kitakachokuwa kikipikwa
hapo hapo kazini, tena bure. Wote hao mafundi wakakubali bila shida. Kutoka
kuganga njaa na kushonea watu nguo moja mwezi mzima, pale walipewa mashine za
kisasa, mazingira mazuri na wakawa wengi. Wakagawana kazi kutokana na ujuzi.
Kiwanda kikafunguliwa rasmi.
Mpaka Naya anarudi chuoni kumaliza mwaka wa mwisho, kiwanda chake kilikuwa kimeanza. Walikisajili kwa majina yao. Malon na Naya. Naya ndiye aliyekuwa mtoa mitindo yote aliyokuwa amebuni. Kazi yakutengeneza na marekebisho ili kitokee kitu anachokitaka yeye mwenyewe Naya, ikaanza. Hakutumia vitu vya gharama sana ili kuweza kufikia watu wengi. Alitumia khanga, vitenge, na vitambaa tu vya kawaida alivyoweza kuvipata kwa bei nafuu. Lakini alibuni mitindo mizuri sana.
Mwaka wa tatu na Wa Mwisho Chuoni
C |
huo
kikafungua, mwaka wa tatu akienda kumaliza, mambo yakiwa mengi mno. Naya akawa
na majukumu mengi kupita kiasi. Shule ambayo ndio ilikuwa salamu ya mama yake,
hicho kiwanda, Malon mpenzi wake, na tamasha alilokuwa akiliandaa, na kuendelea
kujitangaza jijini Dar kwa mavazi. Maonyesho ya kwanza alikusudia kufanya kwa
watu aliokuwa akiwafahamu kwanza na marafiki zao. Alikuwa akiwapigia simu,
kuwakaribisha yeye mwenyewe rasmi, na kuomba wakaribishe wengine. Idadi ya
tamasha la kwanza hakutaka iwe kubwa. Ilikuwa na kiingilio kwani aliandaa na
viburudisho vingine. Naya na Malon wakawa busy kupita kiasi, wakiwasiliana huku
na kule kuhakikisha jambo lolote haliharibiki.
Malon aliwekeza pesa na nguvu. Alimsaidia Naya na kuamini kile
anachokifanya mpaka Naya na wazazi wake walikuwa wakimshangaa Malon. Lile wazo
la Naya, alilipokea na kulifanyia kazi kama lake! Sehemu nyingi na mambo mengi
alifanya Malon, ili Naya atulie shuleni kwa kiasi fulani, japo kuna mambo mengine
yalimuhitaji Naya mwenyewe.
Nidhamu ya shule ikaongezeka ili asije kufeli hata somo moja na
kumlazimu kurudia. Kwa hiyo kila alipopata mwanya, popote alipo, akili
alirudisha shuleni, kusoma. Hakuwa na masaa mengi ya kulala kama wengine, ila
kufanya kazi, shule na kuandaa hilo tamasha alilotaka lifanyike kipindi cha
likizo. Hakujulikana analala wapi. Kama ni chuoni au kwa Malon hapo hapo
Morogoro au Dar.
Mpaka inafika katikati ya mwaka wake wa mwisho wa shule, mambo hayakuwa mabaya. Hakuwa akifaulu sana, lakini alikuwa na uhakika hatafeli somo hata moja. Alipomaliza tu mitihani yake ya muhula wa kwanza, Malon akaenda kumchukua, safari ya Dar kumalizia maandalizi ya tamasha, ikaanza. Kuhakikisha nguo alizobuni zipo sawa, na wavaaji pia wapo sawa, na pia kuhakikisha anawanoa vilivyo ili waweze kuzitendea haki jukwaani. Hapakuwa na mapumziko mpaka aliporidhika kila kitu kipo sawa.
Siku ya Tamasha La Mavazi Ya Naya.
S |
iku ya
tamasha yenyewe kila mtu aliyemfahamu Malon alinunu tiketi akawepo ukumbini,
Ubungo Plaza, Dar. Chezo naye alikuwa akihangaika tu kama Malon, akihakikisha
hilo tamasha lenyewe linafanikiwa. Kuanzia usalama wa wageni wao, ukaaji pale
ukumbini ambapo walipapamba vizuri na kuweka jukwaa zuri tu la kutembelea hao
wavaa mavazi aliyobuni Naya. Kulikuwa na vinywaji vingi tu kwa wageni wao.
Muda wote huo Naya na mafundi wake walikuwa kwenye vyumba vya
nyuma wakiwasaidia wavaaji wao kuvaa na kuhakikisha nguo hizo zinawakaa vizuri.
Malon alikuwa ukumbini na wageni waalikwa pamoja na Chezo. Malon akamtuma Chezo
ampelekee Naya maji ya kunywa. “Hajala kitu tokea asubuhi. Naomba mpelekee haya
maji na soda.” Chezo akachukua na kurudi alipokuwepo Naya.
Katika wasichana wote waliokuwepo pale kambini, Naya alitokea
kumpenda Loi, binti aliyetokea Morogoro. Alikuwa na umbile la kati tu. Zuri
lililopendeza kila nguo. Na uzuri wa Loi alikuwa mwepesi. Wakati wa mazoezi,
kila Naya alipokuwa akimvalisha nguo ya aina fulani, kwenye kundi fulani,
alimtaka yeye ndio awe anapita wa kwanza kisha kurudi kwa haraka kuvaa vazi
aina jingine, apite na kundi jingine labda la kundi la mavazi ya ofisini kama
wametoka kwenye vazi la kanisani au ufukweni. Na Loi alifanya hivyo kwa haraka
sana, bila kuchelewa, kitu kilichokuwa kikimfurahisha sana Naya, na kumfanya
Naya kumsifia mbele za wenzake walipokuwa wakifanya mazoezi huko kwenye hoteli
waliyokuwa wamekodishiwa na kufanya kambi ya siku tatu kabla ya siku hiyo ya
tamasha. Kwenye kila zoezi, Naya alimsifia Loi akiwa hana hila kabisa ila
kutambua kipaji chake.
Asidi Haachi Asili.
W |
akiwa kwenye
pilikapilika ya kuvaa na kutengenezwa, Naya akawasikia wakilalamikia uchache wa
aina hizo za pini wanazotumia kwa warembo hao na wanazihitaji sana. Akakumbuka alikuwa
nazo kwenye gari aina hizo za pini alinunua zamani akabaki akizunguka nazo tu
kwenye gari. Akatoka pale kwenye kile chumba walichokuwepo wale warembo kufuata
hizo pini garini. Alirudi kimya kimya bila wengine kujua na kumkabidhi mmoja wa
wapambaji kisha akarudi kufanya kazi kwenye nguo ya Loi, ambaye ndio alitakiwa
kuwa wa kwanza atakayeongoza kundi la kwanza la mavazi ya weekend kwa wadada. Akiwa
ameinama anamtengeneza yule msichana, na Chezo naye akawa ameingia na vinywaji
vyake wote wakasikia minong’ono kwa nyuma.
Japo ukumbini kulikuwa na mziki ukiendelea, ila waliweza kusikia.
“Na angejua kama Loi ni mke mwenzie, wala asingehangaika naye hivyo!” “Hawezi
kujua. Malon ni mshenzi. Anacheza karata zake kwa akili. Alitaka mimi ndio
nimpendekeze Loi kwa Naya, ili Naya mwenyewe ampigie simu. Na kweli, Naya akakubali
na kumpigia Loi. Wote wanamfanyia kazi yeye Malon, bila wao kujua.” Mwingine
akaongeza. “Lakini nasikia hii shuguli ni ya huyu dada!” “Sio yake Naya. Na
yeye mfanyakazi wa kulipwa tu kama sie. Sie Loi katuambia. Anasema Malon
amemwambia ameona huyu Naya anaakili ya mitindo, ndio akampa hii kazi. Kwani
nyinyi hamumjui Malon jinsi alivyo mshenzi kwa wanawake? Anajua kut..” Chezo
akakimbilia kule walipokuwepo wale wasichana wakinong’ona kwenye chumba cha
pembeni, hakikuwa na mlango.
Wote wakashtuka kwa sababu walikuwa kama wapo nusu uchi. “Kwa nini
hugongi Chezo, wewe!?” Wengi walikuwa
wakimfahamu Chezo kwa kuwa walitokea Morogoro na wale wageni pia walimfahamu
kabisa kwa kuwa kwa siku tatu ambazo Naya aliwakusanya kwenye hoteli, na
kuwaleta hapo ukumbini kwa mazoezi, Chezo na Malon wakisaidiana na Naya,
walikuwa karibu nao sana. “Toka bwana.” “Nilitaka kuwaomba tu, habari zenu za
umbea, msubiri mtakaporudi hotelini au Morogoro. Hapa tunataka mfanye kazi
tuliyowaitia. Kama mnaona hamuwezi, ondokeni.” “Hapana Chezo.” Naya akaingilia.
“Malon amemwaga pesa nyingi sana kwenye hii shuguli. Kwanza
naombeni wote mje hapa.” Naya akawaita. Wote wakasogea. “Naombeni tusikilizane.
Kama nilivyowaambia mwanzo. Malon amemwaga pesa nyingi sana kwenye hii shuguli.
Wote sisi tutanufaika kwa namna moja au nyingine. Na ninaamini katika juhudi
tulizoweka kwenye hii shuguli nzima, tutafanikiwa tu. Sasa, sidhani kama kuna hata
mmoja wetu hapa anataka leo ndio iwe mwisho.” Wote wakatulia. Naya akawaangalia
mmoja hadi mwingine.
Ukweli wote waliingiwa na hofu, wakijua Naya amewasikia na Malon
ni mvuta bangi. “Eti jamani?” Naya akaliza akiwa ametulia tu. “Hapana.” Wote
wakajibu. “Basi. Ili kufanya tamasha hili liendelee, na tufanye mengine zaidi,
nilazima tuweke akili zetu hapa. Kwanza kuhakikisha tunafanikiwa kuwauzia
huduma nzuri wateja wetu, na kuhakikisha pesa ya bosi wetu Malon, inarudi.”
Naya aliongea hiyo sentensi kwa tabasamu. Lakini Chezo alijua wazi
ameshabadilika.
“Na niwaombe radhi kama nimeonyesha upendeleo kwa Loi. Mnisamehe.
Labda kwa kuwa amekuwa kwenye kila kitu. Naona na kutambua juhudi mnayoweka
nyinyi wote hapa. Sina nia yakuonyesha huyu anafaa na huyu hafai. Wote mpo hapa
kwa kuwa nimewaamini na ninajua mnaweza. Hata kama utaonyesha vazi moja tu nililokupangia,
ujue ni kwa kuwa nimekuamini kama unaweza kuwakilisha mawazo yangu kwenye hilo
vazi. Hakuna vazi hata moja nililobuni ambalo si la thamani. Yote imenilazimu
kukaa chini, kuchukua muda mrefu kufikiria na kuchora, ndipo kushonwa mpaka
kufika mwilini mwako. Hapakuwa na vazi lisilo la thamani na hakuna asiye na
thamani kati yenu. Kwa hiyo naomba tuendelee na kama tulivyozungumza, naomba
mjiamini.”
“Mmevaa vitu vya thamani sana. Lakini kama utavaa hilo vazi, halafu
wewe mwenyewe ukawaonyesha wateja wetu upo duni, inamaana aina hiyo ya vazi
ndio halitauzika sokoni. Naomba kila mmoja wenu, ajiamini, na kila mmoja wenu
ajue yupo hapa kwa sababu najua mtaweza kuuza bidhaa zote tena kwa bei ya juu.
Sijui kama mmenielewa?” “Sisi tumeelewa Naya. Na tunaomba msamaha. Hatukutak..”
“Wala msijali. Naomba turudi kwenye kujiandaa.” Naya akamaliza hapo na kurudi
kumtengeneza Loi.
Chezo alibaki ameduaa hapo kwa dakika kadhaa, akaamua atoke. Naya
hakumuongelesha kabisa Chezo, kwani alijua kama kweli Loi ni mwanamke wa Malon,
na yeye lazima anajua ila amemficha. Aliumia sana kuona anazidi kujidhalilisha.
Kusikia kuwa Malon anatangaza kama ile ni biashara yake, na Naya ni mfanyakazi
tu, iliondoa nguvu kubwa sana moyoni mwa Naya. Ile morali ikaisha kabisa. Akatamani
ingekuwa sio siku yenyewe ya tamasha hata angeahirisha. Lakini hata wazazi wake
walishakuwa ukumbini wakisubiria kwa hamu hilo tamasha lianze. Aliwekeza nguvu
nyingi sana. Ndoto na mawazo yake yalishafika kwenye uhalisia, tayari kuonyesha
kwa walimwengu! Naya akaamua kujikaza tu, ili ile ndoto yake itimie. Akajiambia
afanye kwa ajili yake mwenyewe.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
C |
hezo alitoka
pale akaamua atoke kabisa pale ukumbini. Akaenda kusimama nje ya ule ukumbi
lakini ndani ya lile lile jengo, akasimama akiwa ameegemea ukuta. Na yeye akawa
kama amepigwa na butwaa. Malon akawa amemuona kwa mbali akitoka, akamfuata kwa
haraka. “Wewe vipi? Shuguli inakaribia kuanza.” Kimya, Malon akashangaa na
kushindwa kumuelewa jinsi alivyobadilika. “Vipi Chezo, mbona hivyo kaka!?”
Chezo akaguna na kubaki akitingisha kichwa. “Nini tena?” Malon akazidi kuuliza
asimuelewe Chezo.
“Hivi shida ni nini Malon?” “Kwa nini tena!?” Malon akawa bado
hajaelewa. “Hivi unakuwa zile hamu za kuku ambazo huwezi kuvumilia, au unakuwa
unataka kuvua tu wanawake nguo?” “Chezo!” Malon akatoa macho. “Tafadhali
niambie Malon. Kinachokufanya unahangaika wakati unaye Naya, ni nini ndugu yangu!?”
Hapo Malon akanyamaza kidogo. “Eti Malon?” Kimya. “Kwa nini unamtesa na
kumdhalilisha Naya kwa kiasi hicho Malon!? Wewe mwenyewe uliniambia hakuna
mwanamke anayekukata kiu kama Naya. Sasa kwa nini unapita kufunua funua
wanawake wengine? Mbaya zaidi, unawaleta mpaka karibu na Naya! Shida ni nini
kaka!? Ni nini unataka?” Chezo alikuwa akiongea kwa kuumia sana.
“Kinachoniuma na kushindwa kuelewa, sijui unakuwa unazungumza nao
wakati wamekuvulia nguo! Unaongea mambo ya ndani ambayo sijui kama ni kweli au
sio kweli!” “Nimeongea nini!?” Malon akauliza hilo. “Mimi sijui Malon ndugu
yangu. Lakini mimi nishakuona na wanawake wote unaolala nao, hutapata mwanamke
kama Naya. Kwanza anakupenda kwa dhati. Ashakufumania mara nyingi tu, lakini
yule mtoto amebaki mwaminifu kwako, sisi wote ni mashahidi. Pili, Naya ametulia
kaka. Mbegu hizo mjini hadimu. Ametulia, hana papara. Tatu mzuri. Mzuri kwa
kila kitu ambacho ungekitafuta kwa hao wanawake zako. Ana uzuri wakumfanya
mwanaume yeyote akatuliza macho kwake tu. Cha
nne na mwisho, yule mtoto anaakili kaka. Hutakufa njaa ukiwa naye. Hata
ukifilisika, unauhakika atakulishia watoto na wewe atakulisha. Sasa mimi
najiuliza mpaka naogopa Malon, unachotaka ni nini kaka!? Mbona hufikii mwisho
wala hukinahiwi? Unataka kuvua chupi ngapi ndio utosheke? Hakuna mwanaume
mwenye akili yake, akakubali kumdhalilisha mwanamke kama Naya, Malon!
Ninauhakika hakuna. Nimekaa na wewe, na Naya, nawajua nyinyi wote.” Malon
kimya.
“Sasa unakwenda wapi Chezo?” “Mimi siwezi kukaa hapa Malon.
Binafsi nimevurugukiwa akilini, nitaharibu shuguli nzima kama nikibaki hapa.
Acha mimi nirudi Morogoro kaka. Mimi sijajalia kama wewe, Malon. Sina uwezo
wakucheza karata zote kwa wakati mmoja. Siwezi. Hapa natetemeka hata sijui
nafikaje Moro. Ila najua lazima niondoke hapa. Siwezi. Sasa najifikiria kama
mimi niliyeyasikia tu na sio Naya, nipo hivi, je Naya mwenyewe!?” Malon na
Chezo wakatizamana kwa muda, Chezo akatingisha kichwa kwa masikitiko na kuondoka.
Alibadilika, hata Malon alimuona amefika mwisho, hakuwahi kumbadilikia hivyo.
Malon akabaki ameduaa asijue ni nini kimetokea na asijue dhambi ipi imejulikana, tena kwa umbali gani! Kwa kuwa kipindi cha mwisho wakati Naya yupo chuo anajiandaa na mitihani, Malon alikuwa huru mtaani. Kwa kipindi hicho cha maandalizi ya mitihani na mitihani yenyewe, Naya alirudi kabisa kuishi chuoni. Hakujihusisha na chochote cha nje ya shule yake. Malon ndiye aliyekuwa akifuatilia na kumpa maendeleo. Labda ndio kipindi hicho!? Hata Naya naye aliendelea kujiuliza wakati akiendelea kuwavalisha warembo wake, asiamini katika kumsihi kote kule Malon, amerudia tena!
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Daaaah maloni unahitaji maombi maalumu
ReplyDelete