Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Chozi Langu! - SEHEMU YA 16. - Naomi Simulizi

Chozi Langu! - SEHEMU YA 16.


N

elly akatua jijini Dar, Jax akawepo kumpokea dada yake uwanja wa ndege. Wakiwa njiani kurudi nyumbani akaanza. “Nampenda Lara, Nelly. Nampenda sana.” “Hayo umeyagundua lini Jax, kama sio unafanya tu fujo?” “Wakati mwingine huwezi kugundua uthamani wa kitu mpaka ukipoteze na kuna tabia za kupenda kujificha kwenye maisha fulani uliyozoea. Nimejigundua kilichonirudisha kwa Tula hayakuwa mapenzi ila mazoea.” Nelly akamwangalia. “Niliishi na Tula kama mke wangu kwa muda mrefu kuliko Lara. Tula akajaa kwenye maisha yangu kuliko mtu mwingine yeyote yule kiasi ya kwamba akaacha historia ambayo haikufutwa na Lara kiurahisi. Nikisema kiurahisi namaanisha Lara sikupita naye mapito niliyopita na Tula nikiwa sina kitu, tukihangaika sehemu ya kuishi. Lara alinikuta naweza kula kwenye hoteli yeyote nitakayoamua mimi, hata kwa mkopo. Lakini si Tula. Alikuwepo kipindi ambacho siwezi hata kukopesheka! Akaandika historia kubwa. Lakini haimaanishi ndiye aliyekuwa mwanamke sahihi kwangu au ndiye mwanamke aliyeshika moyo wangu! Hapana. Sijui kama unanielewa?” Jax asijue anazungumza na dada yake zaidi.

“Imenigarimu ndoa na mtoto wangu kugundua hilo. Nahisi na Mungu alinipitisha hapo makusudi kujua historia niliyoandika na Tula, sio historia ya mwisho wangu hapa duniani. Bado  nina nafasi kubwa tu na nzuri yakuandika upya historia yangu. Kwa Tula sio mwisho. Na dada, nitapambana kumuhakikishia Lara yeye ndio nataka kumaliza naye kuandika historia yangu ya maisha, na Tula alipita tu kama mwalimu. Hilo darasa nimehitimu, na yeye Lara ndiye mpenzi wangu. Mama wa watoto wangu, mwanamke pekee nitakayezeeka naye.” Nelly akamtizama mdogo wake na kunyamaza.

Akahisi amefanya haraka kutoka kwa Billy. Ni kweli Anele amepita kwenye maisha yake, na amekuwa naye kwa muda mrefu, akatoka akiwa amemuumiza. Hapana jinsi ya kuacha kumtaja. Akatoa simu na kuamua kumtumia ujumbe. ‘Billy, nimefika Dar salama na Jax ndiye amekuja kunipokea. Uwe na mapumziko mazuri.’ Akautuma huo ujumbe. Baada ya muda mfupi tu majibu yakarudi. ‘Hata kama ungekuwa umeniumiza kwa kiasi gani Nelly, mimi nisingekuacha hotelini. Tena peke yako! Kwa hakika nisingekufanya hivyo.’ Huo ukawa ujumbe aliojibu Billy. Nelly akafunga macho baada yakusoma. Billy alishaanza kumuingia moyoni.

Nelly akamtizama Jax, akaangalia tena simu yake. Akabaki akifikiria chakufanya. Akampigia, akapokea bila ya kuchelewa. “Samahani Billy. Samahani sana.” Jax akashituka sana aliposikia Billy. “Samahani kwa nini?” “Kukuacha.” Pakatulia kwa muda. “Unaondoka lini?” Nelly akauliza. “Kwenda wapi? Maana pale uliponiacha, sijasogea, nipo palepale.” “Kwamba bado upo kitandani?!” Nelly akanong’ona Jax asisikie kumbe mdogo wake alikuwa akimsikiliza. “Kwa jinsi ulivyoniacha Nelly, ulitegemea niweje?” Nelly akamtizama Jax. “Naomba nisimamishe gari hapa, nikupishe uzungumze.” Bila kusubiri jibu, Jax akaegesha gari pembeni na kushuka garini kabisa kumpisha dada yake.

“Billy?” “Nipo Nelly.” “Samahani. Samahani sana.” Kimya. “Leo ndio siku hata kama naogopa helikopta, ingekuwepo ningepanda nirudi kuja kukuchukua turudi wote Dar.” “Zipo ndege.” “Kwamba nirudi tena!?” “Mimi ningerudi kwa ajili yako Nelly. Ningerudi bila yakufikiria mara mbili ilimradi niwe na wewe.” “Billy jamani! Kwa nini?” “Naanza kuamini nakuependa Nelly. Ingekuwa mtu mwingine asingeniumiza hivi! Mpaka nimejishangaa! Nimeshindwa kutoka kitandani sababu ya mwanamke! Mimi sipo hivi Nelly. Ila wewe imekuwa tofauti. Na samahani kama nimekuumiza. Sikukusudia.”

“Hapana Billy. Nahisi na mimi sijui nimekuaje! Sikutakiwa kuondoka kwa haraka. Samahani.” Wakatulia. “Njoo Dar. Mimi mwenyewe nitakuja kukupokea uwanja wa ndege.” “Halafu?” “Nitakuwa na wewe mpaka tuagane vizuri.” Billy akabaki akifikiria. “Kama ukiona vipi, basi natafuta ndege nirudi huko.” “Tulipanga tumalize likizo pamoja, Nelly.” “Lakini sio hotelini au hatukuwa na makubaliano ya tumalize pamoja.” “Wewe ulitegemea nini!?” “Sijui Billy. Lakini mimi nilijua unamaanisha tuchukue likizo tarehe na siku zinazofanana ili twende wote kupanda mlima Kilimanjaro.” “Nelly!” Billy akashangazwa. “Kweli Billy! Hatukuzungumza hilo.” “Wewe umetoka kuniambia wewe sio mtoto mdogo. Kweli ulifikiri nataka muda na wewe kwa kulinganisha tu tarehe?” “Basi narudi Billy. Acha nitafute ndege ya kurudi jioni.” “Sawa.” Billy akakubali bila shida wala kusita mpaka akamshangaza tena Nelly.

“Kwamba unataka nirudi kweli?!” “Kumbe hukuwa ukimaanisha? Nilifikiri ulimaanisha uliposema wewe hutakuwa ukinidanganya!” “Namaanisha Billy.” “Basi nitakuona baadaye.” “Sawa.” Nelly akabaki akifikiria garini asijue anarudije tena Moshi. Akamfanyia ishara Jax arudi garini.

Jax akarudi garini kimya. “Nilikuwa na Billson huko Kilimanjaro.” Jax akamtizama na kunyamaza. “Nimepanda naye mlima.” Kimya. “Nimemuacha kwenye mazingira  ambayo si sawa.” “Ninaye mtu anayeweza kukupa tiketi ya kurudi leo jioni.” Jax akaongea bila kufikiria wala kushangazwa na dada yake, alimjua ni mkorofi. Ila Billson! Akabaki akifikiria na kujiuliza ilikuaje maana mara ya mwisho alimkataa vibaya sana, tena mbele ya umati! Kibao kiligeuzwa lini! Akabaki akijiuliza Jax huku akiendelea kukanyaga mafura kumrudisha dada yake nyumbani.

“Billy ni mtu mzuri.” Nelly akajikuta akisifia. Jax akacheka kimyakimya. “Acha nimpigie nione kama anaweza kukupa nafasi.” Jax akatoa simu yake kumtafutia dada yake nafasi ya kwenye ndege kurudi tena Kilimanjaro huku wakielekea nyumbani kwake.

‘Change of plans.’ Ujumbe huo mfupi ukaingia. Ulikuwa ukitoka kwa Billy akimwambia mipango inabadilika. Nelly akakunja uso. Akatulia kusubiria. Baada ya muda ukaingia ujumbe wa pili. ‘Usitafute ndege ya huku. Baada ya kama lisaa hivi, sekretari wangu atakutumia tiketi. Nipe muda mfupi nifanye maandalizi mazuri ya mapumziko yetu. Lakini andaa hati ya kusafiria na wewe mweyewe. Na ujue usiku wa leo tutakuwa na wakati mzuri sana.’ Kisha ujumbe wa tatu ukaingia tena. ‘Kuweka hili wazi, natizamia kwa hamu penzi la usiku kucha.’ Jax akamuona dada yake anacheka na kutizama nje. Hakuwahi kumuona akicheka kwa soni vile kama mtoto wa kike! Jax akajua dada yake amepatikana.

Zikaendelea jumbe nzuri, ikawa kama Billy anamuandaa Nelly kwa usiku wa penzi alilokuwa akilisubiri kwa hamu. Akimueleza nini atamfanyia kwenye mwili wake, mpaka Nelly akawa anaona aibu mwenyewe, tena chumbani kwake akijiandaa kwa hiyo safari. “Haiwezekani Billy! Wewe matiti yangu umeyaonea wapi!?” Ilibidi Nelly ampigie tu. Billy akapokea akicheka sana. “Nilijua tu safari hii lazima upige. Niliona unasoma jumbe zangu, halafu hujibu!” Billy akazidi kucheka. “Acha bwana kucheka Billy! Umeelezea kama yalivyo! Wewe umeyajuaje? Au umeambiwa tena!?” “Hapo sasa unanitia wasiwasi. Nani huyo aniambie?” “Huko unakotoa habari zangu.” “Kwamba ndio yanajulikana hivyo!” “Acha kunipoteza bwana! Wewe umeeleza matiti yangu kama yalivyo! Mpaka mimi nilivyokuwa nakua nikajua yamedumaa!” “Na wakati ndio mazuri! Ukoje Nelly?”

“Napenda hivyo yalivyo. Yaani nilibaki nikijipimishia mkono kama nitaweza kukamata kila moja kwa mkono mmoja.” “Hakika nakukatia simu. Yaani mimi nipo na wewe nafikiri akili zako zipo vizuri, kumbe zipo kwenye matiti yangu!” Billy alingua kicheko kwa sauti ya juu sana. “Mimi nisingekwambia hivyo Billy!” “Kwa sababu sina matiti ambayo ni kama yalitaka kuanguka hivi, yakagoma na kutengeneza duara kubwa hapa chini. Yakajaa haswa na kushikiliwa na chuchu...” Nelly akamkatia simu.

Hapohapo Billy akampigia tena. “Naona simu imekatika katikati ya...” “Hapana Billy. Nimekukatia.” Billy akazidi kucheka kwa sauti. “Mimi najiandaa kwa safari Billy. Unanichelewesha.” “Hutaki kujua niliyaonea wapi?” “Naanza kutotaka.” Billy akazidi kucheka kwa sauti. “Sema sasa.” “Unakumbuka siku ile ya kwanza kule Moshi  hotelini, mimi ndio nilikuwa wa kwanza kuoga?” Nelly kimya. “Najua utakuwa umeshanisoma Nelly. Mimi kazi za mikono sitaki na sifanyi kabisa japo najua. Nilishajiambia hapa duniani ni mgawanyiko wa kazi. Wengine tunabarikiwa kipato kwa ajira za maofisini, wengine majumbani. Sasa huwa nikivua vitu vyangu, naachaga hapohapo. Na hata kitanda changu yupo wa kunitandikia kila siku na mashuka ninayolalia nilazima yabadilishwe kila siku.” Nelly kimya.

“Usinikimbie sasa.” “Nakusikiliza.” “Sasa siku ile nikajisahau. Nikadhani nipo peke yangu. Nikavua kila kitu bafuni na kuacha hapohapo sakafuni. Nilipotoka ndipo nikakumbuka sipo kwangu na nipo na wewe, inabidi nionyeshe tabia njema ili usinikimbie.” Mpaka Nelly akacheka. Akiwa ameshamuelewa. “Nikakumbuka ukiwa umeshaingia bafuni, nikasema nikuwahi niokote vitu vyangu ili kukupa nafasi. Ndipo nilipoingia nikakukuta umeshaingia kwenye shower unaoga.” “Unatabia mbaya Billy wewe! Kwa hiyo ulinichungulia pale ndani ya shower?” “Sikukuchungulia ila nilikuona.” “Huna lolote. Ungejuaje kwa undani hivyo?” “Kwani wewe hujawahi kushangazwa na jambo na kujikuta ukipigwa na butwaa kidogo.” Nelly akamkatia simu tena.

Baada ya muda ujumbe ukaingia. ‘Siamini kama leo nitalala na hizo chuchu mdomoni.’ “Haaa!” Nelly akahamaki kwa sauti. “Huyu Billy anaakili za kitoto jamani! Alale na chuchu mdomoni, yeye mtoto mchanga!” Nelly akawaza akishanzwa na vile Billy alivyomkamia. Ila ikamgusa na kumuongezea ujasiri.

Akabaki akimtafakari Billy huku akiendelea kujiandaa. Pakatulia kwa muda akatuma ujumbe mwingine. ‘Natizamia wakati wetu wa pamoja Nelly. Na asante kwa kuamua kunifuata.’ Nelly akakaa kabisa na kuacha kufungasha. Akarudia huo ujumbe na kutafakari kidogo. Anamjua Billy huwa hajui kumpunja. Anajitoa kwake na kutumia pesa nyingi sana juu yake. Na alimwambia ni ili amfurahishe tu. Akajisikia kuvutiwa naye zaidi. Akaanza kufikiria kufanya mapenzi na mwanaume kama Billy! Akajisikia furaha moyoni. Akajikuta akimrudishia ujumbe. ‘Na mimi Billy. Naamini tutakuwa na wakati mzuri.’ Hilo likamfurahisha Billy alipopata hayo majibu. Akajua na yeye ameridhia. Alishamsoma Nelly, maisha yalifanikiwa kufunga hisia za kimapenzi kabisa. Sasa kuja kupata huo utayari wake, ikamuongezea shauku ya usiku huo.

Nelly Mikononi kwa Billy.

N

elly alitua kwenye uwanja wa kimataifa wa Robert Gabriel Mugabe, mjini Harare, Zimbabwe usiku huo, akakuta Billy akimsubiria. Wote wakacheka. “Nimefurahi umenifuata, Nelly.” Nelly akagundua hilo amelirudia tena. Inamaana amemaanisha. “Sasa kama ulitaka nibaki kwa nini hukuniambia nibaki?” “Hapana. Nilitaka na mimi kuchaguliwa. Safari hii na mimi nilitaka kuchaguliwa.” Nelly akacheka. Hata kabla hajampokea mizigo yake, palepale nje ya uwanja wa ndege, akamvuta pembeni ya kigari cha mizigo alichokua akakisukuma, akamkumbatia Nelly vizuri na kuanza kupata mabusu. Akambusu kwa kituo kabisa ndipo akamuachia.

          “Karibu, Harare Zimbabwe. Ndio kwetu.” Ndipo akachukua sasa kigari kilichokuwa na mizigo yake, aliyorudi nayo. Giza lilikuwa limeshaingia. “Kwa nini imekua hapa?” “Tokea Anele anitende vibaya, nilipachukia sana.” Akajishitukia kwa haraka akaingiwa na hofu mpaka Nelly akamuona. Ni kama aliropoka tena. “Samahani kwa kumleta tena..” “Hapana Billy. Tafadhli kuwa tu na amani. Nataka na mimi niwe mtu wako unayeweza kumwambia chochote kinachokusumbua.” Hilo lilimgusa sana Billy. Mpaka akasimama kabisa.

          “Kweli Nelly?” “Kabisa. Sasa usipozungumza na mimi, utazungumza na nani! Tafadhali kuwa tu huru.” “Nashukuru. Hilo limenifurahisha zaidi na nitakavyokwambia! Ni kweli huwa nazungumza na mama karibu kila siku, pamoja na binti yangu, lakini kuna mambo siwezi kuzungumza kwao. Sijui kama unanielewa? Najikuta mpekwe!” “Samahani mwanzoni niliondoka kwa haraka, Billy. Lakini mimi sio dhaifu kiasi cha kutishwa na Anele ambaye mlishaachana! Kuwa huru kabisa.” “Afadhali. Sasa tokea Anele anitende vibaya, sijawahi kurudi tena kwenye hii nchi. Nafikiri labda nilikuja kikazi tu, basi. Ila napakwepa sana. Sasa kwa kuwa ni nyumbani kwa wazazi, kwamba nilazima siku moja ningetakiwa kurudi, kama nyumbani, lakini nikawa sina huo ujasiri. Sasa kwa wewe kukubali kunifuata, nikaona angalau tuwepo hapa pamoja, nitengeneze historia mpya, nyingine, mbali na ya uchungu niliyobaki nayo.”

Nelly akamuhurumia. Akagundua bado Billy yupo na maumivu yakutendwa. “Umekula?” “Tutakula chumbani. Nimeandaa usiku mzuri sana. Kila kitu kitatufuata tulipo. Nimefurahi sana umerudi.” Bill akarudia tena. Nelly akamwangalia. “Na mimi nataka kupendwa Nelly. Na mapungufu yangu yote, bado nataka kupendwa. Nastahili jamani!” “Kweli unastahili Billy. Wewe ni mtu mzuri, mwema, na ndio maana nimerudi. Na samahani kwa kuondoka vile. Nahisi ni wivu tu.” “Huna haja yakumuonea wivu Anele. Hatawahi kurudi kwenye maisha yangu tena. Ila sikatai kama ameacha historia kubwa na ameniumiza. Lakini hata nijikute naye uchi, hakika sitamgusa.” Nelly akacheka. Dereva akaendelea kukanyaga mafuta kurudi hotelini.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Walipofika tu mlangoni, wakaangaliana, Billy akaanza tena kumbusu wakiwa hata hawajaingia ndani. Muhudumu wa hiyo hoteli aliyekuwa amewabebea mizigo yao alifungua mlango wa chumbani kwao akiwa na mizigo yao wote wawili, akawaacha hapo nje wakiendeleza kiss za haja. Billy alikuwa amemvutia Nelly pembeni akaweza kuegemea pembeni ya ukuta hapo karibu ya mlango, na yeye akawa kama amejiegemeza kwake akiendeleza kiss kwa kutulia tu. Baada ya muda yule muhudumu akatoka na kueleza kila kitu kipo tayari ndani, amekwisha panga. Alijieleza akiangalia pembeni kwani bado walikuwa wakiendelea kubadilishana ndimi kama wanandoa wachanga waliokuwa wamesubiriana kwa muda mrefu, ndio siku hiyo yametimia. Akataka kuondoka kwa kuwa hakuwa amejibiwa na Billy ndiye aliyekuwa amempa mgongo. Alipofika mbali kidogo, Billy akamuita ili kumpa tip. Pesa ya kumshukuru kuwabebea mizigo yao mpaka ndani. Akamuacha Nelly akishika midomo yake na cheko la taratibu.

Wakati akimlipa yule muhudumu, Nelly akaingia ndani. Kwa hakika alishangazwa na hicho chumba. Billy akaingia na kumdaka kiunoni akiwa bado anashangaa. “Subiri kwanza Billy!” Nelly alikuwa amekanyaga maua hapo sakafuni. Yalimwagwa kuanzia mlangoni, yakatengenezwa njia kuelekea chumbani na mpaka bafuni. Na kila sehemu Nelly alipoyafuata, yalikuwa yamemwagwa kwa unadhifu sana. “Waw!” Nelly akahamaki asiamini ndio chumba atakachokuwepo kwenye mapumziko yake na Billy.

Akageuka nyuma, akakuta Billy akimwangalia. “Sijawahi ingia chumba kizuri hivi!” Hilo likamfurahisha Billy.  Kwa hakika kulipangiliwa, Nelly akajua na hapo atakua ameacha pesa ndefu tu. Alilipia classic romatic suite. Sekretari wake ndiye aliyemsaidia maandalizi yote hayo yeye akiwa bado KIA, uwanja wa ndege wa Kilimbanjaro akisubiri ndege yake iondoke wakakutane na Nelly, Harare. Aliendelea kuwasiliana naye akimpa maelekezo ya aina ya chumba anachotaka akikute. Na kweli waliitendea haki pesa yake. Hoteli yenyewe ilikuwa nzuri sana ya kimataima. Ipo sehemu nzuri na hata chumba chenyewe, Billy alitaka kiwe sehemu ambayo hapatakuwa na kelele.

“Nakushukuru Billy. Najua na wewe utapumzika, lakini mimi nilihitaji haya mapumziko. Mwenzio huwa sichukui likizo.” “Haiwezekani Nelly! Miaka yote?” “Niende wapi au nifanye nini nyumbani Billy? Sina familia kwamba niende likizo. Sina starehe yeyote ila kazi tu.” “Kama ndio hivyo basi ni afadhali tumepata hiki chumba. Huu upande hutasikia kelele za watu, itakusaidia kupumzika.” Nelly mwenyewe akamsogelea na kuanzisha busu yeye mwenyewe. Billy akacheka kwa furaha kuona Nelly ameanzisha. Akajua amefurahia ndio anashukuru. Akamuona anazidi kumng’ang’ania. “Ooohooo!” Billy akasikika. Wakati Nelly akimvua shati. “Tonight, Am in troubleee!” Nelly alicheka vile Billy alivyosema usiku huo yupo matatizoni. Lakini aliendelea kumtoa nguo za juu taratibu huku akimbusu kule alipotoa zile nguo. Walikuja kujikuta kitandani hamna mwenye nguo ila wote wakiwa tayari kuyachukua mahusiano yao kwenye ukurasa mwingine.

“Unauhakika? Maana baada ya hapa hakuna kurudi tena nyuma, Nelly.” Billy aliongea akiwa amemlalia Nelly juu yake, matiti yake chini ya kifua cha Billy, na mkono mmoja upo kwenye hips ya Nelly kwa chini amemkata kwa nguvu. “Unamaanisha nini!?” “Sitafuti mwanamke wa kulala naye usiku wa leo tu! Wapo wengi. Nakutaka wewe kwenye maisha yangu.” “Hunifahamu Billy!” “Basi hiki tunachotaka kufanya, naomba kisubiri.” “Billy!” “Sio na wewe Nelly. Wewe si kwa kupunguza haja za siku moja halafu basi. Nakutaka kwenye maisha yangu. Nimechoka kuwa peke yangu Nelly! Nataka uwe wangu. Ni nini unachoogopa bwana? Mimi sio mtoto mdogo. Kama ingekuwa ni mapenzi tu, tungeyafanya siku nyingi sana. Ndio maana nilisubiri mpaka nione umbali unaoweza kwenda na mimi.” “Sasa umeridhika?” “Nisingefika umbali huo kwenye mwili wako!” Nelly akacheka kwa aibu na kujifunika.

Maana ni kweli Billy alimfanyia mengi kwenye mwili wake ambayo hakuwahi kufanyiwa kabla. Mpaka Nelly aliyeanza na mwili ukionekana stiff kwa tension, yaani uliokakamaa kwa wasiwasi, ukatulizwa kabisa hapo kitandani. Billy alimfanyia yote kama alivyoahidi tena bila papara. Hapo Nelly alikuwa tayari tu ammalizie.

Billy akawa kama ameshitushwa na kitu. “Subiri kwanza Nelly! Wewe ulifikiri ndio nafanyia wanawake wote niliyokufanyia wewe hapa!?” Nelly akatingisha kichwa kukubali. “No way! Haiwezekani kabisa! Wewe unaniona kwa wasiwasi nini!? Au unafikiri kwa kuwa nimekung’ang’ania hivyo unafikiri ni kwa kila mwanamke?” “Mimi sijui bwana Billy! Wewe fanya mapenzi na mimi sasahivi. Unanikata stimu.” Billy alicheka sana. “Usiniambie umenogewa hivyo!” “Sana. Kumbe ndio vitamu hivyo!” Billy akarudia romance kidogo akijua ni kweli ameshamtoa kwenye hali ya utayari aliyokuwa nayo kabla ya swali lake alilopenyeza hapo katikati. Akamfanyia tena kidogo, akatoa midomo chini, akairudisha kwenye chuchu kisha akamwangalia. “Kwa hiyo hakuna kurudi nyuma?” “Sasa hivi naweza kukuapia chochote kile. Wewe endelea tu, nitakuwa chochote unachotaka.” Billy alicheka sana na kuendelea.

Ukweli Nelly alifurahia mapenzi ya Billy. “Utaalamu huu wa mapenzi ni wa kila siku au leo tu kunivutia?” “Tuna siku tano hapa. Kwa nini usivumilie ukajionea mwenyewe?” “Ninachojaribu kukwambia ni, usipunguze hiyo nguvu ya mvuto ila kuongeza.” Billy alicheka sana. “Hakika nimependa Billy. Upo vizuri halafu umetulia, huna hekaheka nyingi, una nguvu na stamina. Napenda unavyonishika kwa nguvu, na ukiingia hakika nakusikia vizuri sana bila maumivu! Halafu nimependa vile ulivyonimwagia...” Nelly akawa kama anajaribu kuvuta kumbukumbu hapo kitandani baada ya mapenzi marefu matulivu waliyomaliza.

“Ile ya baridi au vuguvugu?” Billy akajaribu kumsaidia kumkumbusha kwa swali akicheka. “Labda unimwagie tena, halafu usiharakishe kuilamba ukinyonya ndio nitajua kama napenda ya baridi zaidi au vuguvugu.” Billy alicheka mpaka akapaliwa. “Pole.” Nelly akatoka kitandani kwa haraka kumletea maji ya kunywa akiwa uchi kabisa akichikilia matiti yake. “Kunywa maji.”  Billy akanywa mpaka akatulia, ila akagundua kuna vipande vya barafu ndani. Nelly akamuona anacheka. “Nini sasa?” “Ulivyonisimamia hivyo uchi, nishapata wazo la wapi pakumalizia hizi barafu zangu kwenye hii glasi.” Nelly alifurahia na kujitupa kitandani akisema. “Enjoy your ice cubes.” Billy alizidi kucheka vile Nelly alivyokuwa akimkaribisha bila kusita huku akijiweka sawa hapo kitandani, chini ameweka taulo mbili ili kitanda kisilowe, miguu wazi ili Billy aweke chochote huko.

Alipenda sana jinsi alivyokuwa akimmwagia mwilini mwake vitu tofauti tofauti kuanzia katikati ya matiti, anaweka michirizi kiasi mpaka  kitovuni, kisha kushuka chini akiweka nyingi juu ya kinena ili ichirizike kiasi chini kabisa. Na mapajani kidogo kisha kuanza kuila hivyohivyo. Jinsi alivyopitisha ulimi juu ya huo mwili wa Nelly, kwengine alilamba na kwingine kunyonya. Nelly alijikuta akitoa milio tofautitofauti. Kwengine ikawa akicheka sana, kama anayemtekenya, kwengine migugumo ya haja. Na Billy alijaliwa utaalamu wa mikono pia. Hakuna alikopita na kumuacha Nelly salama, na kumtaka tena na tena, mpaka aibu ikamuisha akabaki akidai, kitu kilichomuongezea ujasiri Billy mwenyewe akijua anafanya kitu kinachopendwa. Hapakuwa na kutoka tena. Chakula kiliwafuata hapohapo chumbani. Wakamaliza uchovu wa kupandisha mlima, na likizo hapohapo hotelini. 

Kwa Jax

J

ax alikusudia kwelikweli kumrudisha Lara kwenye maisha yake. Wakati dada yake anafaidi na Billy, na yeye akaendelea kutengeneza yake ambayo hayakuwa hata na tumaini. Safari za Dodoma nyumbani kwa kina Lara zikaendelea bila kuchoka mpaka na wao wakamzoea. Anafika jumamosi, anaondoka jumapili bila ya kumuona Lara. Japokuwa alishakatazwa kurudi hapo, wakamuonyesha wazi hatakiwi, lakini Jax hakukoma kufika hapo. Akafanya hivyo mfululizo mpaka wakaanza kuandaa chakula kizuri kwa ajili yake siku za jumamosi wakijua lazima usiku atakuwepo hapo. Alipofululiza weekend tatu mbeleni mpaka mzee Chiwanga akaanza kumuhurumia. Kila akifika hapo hataacha kuomba msamaha. Akitubu kwa kuwafedhehesha.

Mzee Chiwanga mwenyewe akamwambia inatosha. “Hii imeshatokea, nafikiri Mungu aliruhusu kila mmoja wetu apokee funzo lake. Basi. Maisha yaendelee. Huna haja yakuendelea kuomba msamaha.” Hapo Jax akafurahi sana, akapiga tena magoti kama mtoto wa kike na kushukuru. Akafurahia angalau moyo wa Mzee Chiwanga umeanza kufunguka kwake.

Akaendelea kwenda hapo japo hakuwa akimuona Lara ila akaanza kuona mabadiliko. Akaona wanaanza kujirudi mmoja baada ya mwingine. Akifika, hawakimbii tena sebuleni. Wanakaa naye. Na yeye hakuacha kuleta zawadi hapo. Akaweka urafiki na Lucas. Akimuuliza maswali ya hapa na pale akitaka kujua shule ikoje na mambo mengine. Siku anazofika hapo mapema, anaweza hata kutoka naye nje na kucheza naye mpira. Watamsikia akicheka nje na Lucas pamoja na marafiki zake Lucas. Akawa mwenyeji. Bado hawakuwa wameonana na Lara.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alipoona anapokelewa vizuri nyumbani kwa kina Lara, akabadili utaratibu. Akawa akitoka tu kazini siku ya ijumaa, basi safari ya Dodoma inaanza. Anafika ijumaa usiku, anakaa hapo Dodoma siku ya jumamosi, jumapili jioni anaondoka. Akaendelea kuja hapo mpaka mtaani nao wakaanza kumzoea. Anaonekana mtaani siku za jumamosi akiwa anazunguka na Lucas kama asiye na shuguli za maana. Akajiunga kwenye kucheza mpira wa miguu na vijana hao wadogo wa hapo mtaani, rafiki za Lucas na Lucas mwenyewe aliyependa mpira kuliko nafsi yake. Mama yake alishasema juu ya kushinda kwake mpirani mpaka akachoka. Tangia mtoto mdogo, Lucas alipenda mpira, ndio shule ilifuata, tena kidogo sana. Ila hata shuleni, alitumia muda wake kucheka mpira wa miguu.

Kwa hiyo hizo siku za jumamosi, utamkuta Jax uwanjani na Lucas pamoja na vijana hao akicheza mpira mpaka giza linaingia ndipo wanarudi hapo nyumbani na Lucas wakiwa wanatokwa jasho wakicheka. Atasubiri chakula. Akila ndipo anarudi hotelini. Alishamletea Lucas raba nzuri sana za kuchezea mpira na nguo za michezo. Huna utakalomwambia tena Lucas juu ya Jax akaelewa. Sifa zake zilikuwa zikiimbwa na Lucas kila siku mpaka Jax aje kurudi tena hapo. Wakawa marafiki kweli na mpaka vijana wanaocheza mpira hapo mtaani na Lucas, wakamfahamu Jax na kumzoea. Ikawa jambo la kawaida kwao kugongwa na kuuliziwa Jax kana kwamba anaishi hapo. Akawa kama mtoto wa hapo mtaani.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

 “Nashauri uzungumze naye, mama yangu. Huyu mtu inamgarimu sana kuja hapa kukufuata. Anakuwa ni kama anaishi huku!” Mwishoe huruma ikamzidia mzee Chiwanga. Akajaribu kumshawishi binti yake. “Anaonekana anajutia kosa, na amekusudia kujirudi na kwa vitendo. Nilishamsemesha vibaya sana. Sikutegemea kama angeendelea kuja hapa! Kila mtu mpaka mama yako amekuwa akimkatisha tamaa, lakini hajaacha kuja. Mara aje na ndege, mara awe anaendesha! Kila ijumaa yupo huku Dodoma kwa ajili yako mama, mpe hata dakika tano tu, mzungumze.” “Mimi sina kitu chakuzungumza naye baba. Nilishamwambia simtaki tena, sina kitu kingine chakumpa. Kwa nini anang’ang’ania!” Lara akalalamika. Baba yake akaamua kumuacha.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ijumaa inayofuata, Jax hakutokea. Jumamosi nayo kimya. Hakutokea asubuhi kama walivyozoea kumuona. Lara akaanza kuhangaika. Wazazi wake wakatoka kwenda kwenye biashara yao wakamuacha hapo anasafisha kwa mkono mmoja akipanga. Ilipofika saa 9 mchana wakamuona amewafuata pale dukani, amepoa. Akakaa hapo hakuna aliyemuuliza. Ilipofika saa 12, akauliza. “Kwani umemwambia Lily apike nini usiku?” Akamuuliza mama yake. “Vipi? Kuna kitu unataka kipikwe?” Akatulia mama yake akiendelea na kazi zake hapo dukani. “Labda kuongeza kidogo. Jax anapenda sana mboga za majani.” Mama yake akasikia kucheka moyoni. “Anatengeneza chapati na maharage. Nitampigia nimwambie aongezee mboga za majani.” “Labda nimpelekee na samaki.” “Sawa mama.” Kumbe Mzee Chiwanga alikuwa akisikiliza tu. Lara akaondoka.

Siku hiyo ya jumamosi mpaka wanakwenda kulala saa nne usiku Jax akawa hajafika hapo na chakula aliachiwa. Jumapili nayo asubuhi hakutokea. Wakaenda kanisani na kurudi hapo mchana. Wakapika, wakala, Jax hakutokea. Ilipofika usiku wakamuona Lara amejikunja kwenye kochi ameegemeza kichwa kama mnyonge anaangalia tv hata hazungumzi tena. Ameshikilia mkono wake.

“Mkono vipi mama? Umeanza maumivu?” Lara akamwangalia baba yake na kurudisha macho kwenye mkono. “Wala hauumi. Nafikiri umeshapona. Week hii tukatoe, baba. Nahisi muda umeshapita!” “Tutaenda wakaangalie. Tuone.” Baba yake akataka atoke kwenye yale majonzi. Lara akahamia kwenye kochi alilokuwa amekaa baba yake, akamsogezea mkono uliofungwa PoP.

Familia nzima walikuwepo hapo. “Halafu ujue ni mimi peke yangu humu ndani ndio sijaandika hapa!” Lara akacheka kidogo. “Nitaenda kutoa ukiwa hujaandika chochote!” “Acha leo niandike. Lucas niletee kalamu.” Wote wakacheka nakutaka kujua baba yao ataandika nini maana walishamshawishi sana, bila mafanikio. Akaletewa kalamu. “Nitafutie sehemu nzuri.” Lara akawa anacheka huku akitafuta. “Huku juu ndio wengi hawajaandika.” “Ewaa!” Kila mtu akasogea pale kwenye kochi walilokuwa wamekaa Lara na baba yao. “Mtanitingisha sasa! Si msubiri kwanza niandike ndio msome?” Wakasogea pembeni wakicheka, wakisubiria kwa hamu.

‘Vipingamizi visiwahi kukusimamisha maishani. Unapokumbana na ukuta ukikusimamia njiani, usiogope wala usikwame. Jifunze jinsi ya kuupanda, au kupita katikati yake au kufikia lengo lako na wenyewe ukiwepo.’ Wakamuona Lara anafuta machozi, wakajua baba yao amemaliza. “Nisome na mimi, Lara.” Lucas mleta kalamu akawahi na wengine wakasoma. Mama yake naye akasoma na kunyamaza. Lara akajirudisha nyuma kwenye kochi akatulia. Hiyo siku nayo ikapita bila Jax kuonekana.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mambo yanaendelea. Usikose Muendelezo kujua kitakachoendelea kwa Penzi zito la watu wazima hao wenye pesa.

Je, Tamu mpaka mwisho?

Je, Jax amekata tamaa na kuamini hatampata tena Lara?

Si kwamba aliishiwa. Ni maisha mazuri aliyoishi na Lara ndio aliyataka tena na kufanya amrudie. Lakini bado Jax yupo zaidi ya vizuri. Jax bado anakazi nzuri, mvuto, na yupo jijini ambako angeweza kupata yeyote na kumuoa. Hilo ndilo lilianza kumuumiza Lara kila masaa yakizidi kuyoyoma na Jax kutoonekana tena hapo kwao.  Akamkumbuka Tula ambaye hajui kumzira Jax. Kwa yeyote na popote, hana haya yakusema shida yake ni Jax. Wasiwasi ukazidi kumuingia Lara. Amemringia Jax zaidi ya kawaida.

Je, nini kitaendelea?

Usikose muendelezo....

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment