Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Chozi Langu! - SEHEMU YA 21. - Naomi Simulizi

Chozi Langu! - SEHEMU YA 21.

 Chumba kizima kilitulia wakati Anele akieleza ya Nelly kwa ujasiri. “Na sidanganyi kwamba nataka kumuharibia Billson! Ni ukweli, hata mkitaka naweza kumpigia simu huyo Yasinta. Amebakisha kitu kimoja tu, athibitishe. Lakini vingine vyote anauhakika kwa asilimia 100.” Anele akaweka msisitizo. “Acha nikusaidie Anele. Maana najua unapoteza pesa yako kwa Yasinta.” Billy akaanza alipoona amemaliza na wazazi wake pamoja na ndugu wakihisi anarudia kosa kwenye ndoa. “Wewe ni kosa nililojifunza kwa machungu sana. Umenigarimu mimi na watoto wangu. Mpaka leo watoto wangu wanalipa garama.” “Sasa mimi hapa nimefanya nini!? Kwa nini unanigeukia mimi na sio huyo mwanamke unayefikiri ni mwema unataka kumuoa?” Akauliza Anele akishangaa sana.

“Wakati ukizungumza, wote tulikupa nafasi ya kukusikiliza. Umemaliza na ndio na mimi nazungungumza. Unanisikia Anele?” “Sawa. Lakini niliona ni kama unataka kuni...” “Nyamaza Anele. Na wewe ujifunze kusikiliza watu. Chumba kizima hapa tulitulia tukikusikiliza. Acha na Billy naye azungumze. Binti yako huyo anakuangalia kwa karibu sana na anaiga kila kitu unachofanya. Kuwa mwangalifu.” “Kwani kuna shida gani ya yeye kuwa kama mama yake?! Wewe vipi Beila?” “Kama hivyo alivyo huoni kama anatatizo, basi sina sababu ya kuzungumzia hilo tena.” “Mnamuhukumu mwanangu kwa kuahirisha tu mwaka!? Mbona wewe watoto wako kutwa wanafeli na sisemi!?” “Acha kuongea kama mpuuzi Anele! Ni bora lipi? Junior anayefeli na anakazana na shule, au hata akiambiwa arudie anarudia, akionyesha anayo nia, au kuliko huyo Briana ambaye hata shule haendi yupo tu mitandaoni?” Billy akamuuliza kwa ukali kabisa.

“Ninachotaka kukwambia Anele, kwa sababu unachofanya hapa hakikuhusu. Hii ni kuniingilia mimi na Nelly, na sitakuruhusu.” Hapo kidogo hata Jax akapumua. Maana alishamuhurumia dada yake kuona kama amewekwa kati, anasomewa shitaka. “Jamani, nilifanya kosa kwa Anele, kumuoa bila kumfahamu. Lakini nimejifunza wazazi wangu. Mama anajua. Nimekuwa nikimshirikisha hatua moja hadi nyingine juu ya Nelly, japo sikumpa taarifa zisizomuhusu juu ya Nelly. Nelly ninayemuoa leo namfahamu kwa asilimia 95, zilizobaki ni chake sana kwa sababu simfahamu Nelly ajae. Nelly atakayekuwa na mimba ya miezi 9, au Nelly atakayekuwa mama na mke. Ambazo hizo asilimia 5 zilizobaki, zinanipa ujasiri wa kumuoa Nelly kwa asilimia 95 ninazomfahamu. Nelly anampenda Billy kama Billson.” Billy akaendelea.

“Huyu Yasinta anayemzungumzia hapa, na mimi namfahamu kwa kuwa mimi ndiye niliyemtafuta nikitaka kumfahamu Nelly kwa karibu sana. Nilikubali kumlipa kama alivyonidai yeye mwenyewe ili kunipa habari za Nelly. Hichi anachowaambia Anele sasa hivi, mimi niliambiwa na Yasinta, na kutaka kunipeleka mpaka kwa mama yake mwenyewe ili kuthibitisha.” Mpaka Nelly akakunja uso. Jax akashangaa sana aina ya ndugu zake na kumuelewa Nelly ni kwa nini anajaribu kuwa nao mbali.

“Nilimlipa Yasinta na kumwambia alichoniambia kinatosha kabisa, sina sababu ya kwenda kwa mama yake kwa uthibitisho. Tukaachana. Alipokuja kusikia namuoa Nelly, na sijui aliambiwa na nani, Yasinta alinitafuta sana. Akaomba miahadi ya mpaka kwa sekretari wangu, akaambiwa kalenda yangu imejaa, mpaka nitoke likizo, pengine anaweza kupata nafasi. Sikuambiwa, ila nilimkuta akinisubiria getini. Nikamwambia dereva asimamishe gari na kumruhusu aingie. Narudia tena, aliyarudia yote na kunionya nisimuoe Nelly.” “Kwa nini hukuniambia Billy!?” “Ili iweje Nelly?” Billy akamuuliza, Nelly akatulia.

“Nikampa jibu ambalo pengine na wewe Anele litakusaidia na uache kunifuatilia mimi na Nelly. Ubaya wooote uliosikia juu ya Nelly, nimepata uthibitisho kutoka kwa Nelly mwenyewe akinithibitishia kwa kadiri ya tulivyokuwa tukiishi naye na mengine kunishirikisha yeye mwenyewe bila kumlazimisha. Namfahamu Nelly na ninampenda, na ndio sababu ya kunifanya nikubali au nimuombe akubali nimuoe. Wewe sijawahi kukupigia goti nikikuomba nikuoe. Lakini kwa Nelly, nikiwa namfahamu kwa asilimia zote hizo, nilifanya. Na hata nikipewa nafasi nyingine tena, kwa Nelly nitafanya. Na jibu la hapana kutoka kwake si chaguzi na yeye ananijua. Ameshanifukuza zaidi ya nitakavyosema na Jax mdogo wake huyu ni shahidi. Nafikiri hakuamini aliposikia tupo pamoja na dada yake. Nelly hakuwa akinihitaji japo alijua wadhifa wangu. Nelly alinikataa akiwa ametambulishwa mimi ni nani. Ila wewe Anele ulinikubali kwa haraka kwa kuwa ulitambulishwa mimi ni nani.” Kimya.

“Niliweke hili wazi pengine litawasaidia nyinyi wote. Na nafikiri Nelly alimwambia hata mama na Britney. Sijui kama mlimuelewa?” “Labda urudie Billy. Taarifa nyingi zinapita sasa hivi.” “Usichanganyikiwe mama yangu. Nelly niliyekutambulisha kwako na ukaniahidi kuniombea ukinipa baraka zako, ndiye Nelly huyuhuyu anayemzungumzia Anele na ndiye ninayemuoa.” Mpaka hapo Billy hakuwa amekanusha jambo hata moja.

“Naliweka hili sawa kwa wote. Nelly alikuwa na maisha yake, wala hakuwa na mpango wa mwanaume wala mtoto. Hichi anachozungumzia Anele kuwa mimba ndio imekuwa sababu ya Nelly kuninasa au sijui ni ujauzito wa mwingine ameshika kwa ajili yangu, jamani si kweli. Huu ujauzito ndio unaomnyima Nelly usingizi. Nelly hataki mtoto wala hakuwa akitaka mume. Mimi ndio nilimlazimisha sana mahusiano. Kwa kutumia kila nguvu mpaka kumuona yupo hapa ni mimi kumtaka wala si yeye kunirubuni. Kuahirisha harusi sasa hivi kwake ni jambo la furaha kuliko kuendelea na hii harusi, maana haikuwa kwenye mipango yake ya maisha. Nina uhakika kwa asilimia 100, sasa hivi tukisema harusi hamna, atabeba mizigo yake na kurudi kwenye maisha yake bila shida na asione amepungukiwa.”

“Sio kweli Billy.” Hapo Nelly akakanusha. “Wewe nakupenda. Nitasema ‘ndiyo’ kwako tena na tena, popote kule. Wewe nakuhitaji na wala sitaogopa kusema. Kama nilishafanya kosa nyuma, sio wewe. Na hata mtoto japokuwa sikuwa nikitaka kabisa, lakini naanza kujifunza na kumfurahia kadiri ninapomsikia akicheza. Hofu ya pengine nitashindwa kuwa mama mzuri inaanza kupungua. Kwa hiyo hapa nilipo, na wewe Billy, sijutii na sina mpango wa kukimbia kwa haraka.” Billy alifurahi sana.

Akamsogelea na kupata busu hapohapo, tena la muda tu akivuta midomo ya Nelly kwa utulivu tu. “Nashauri msubiri baada ya harusi.” Angalau Brandon akafanya watu wacheke lakini Billy akaendelea kidogo na kumuachia maana Anele alitaka kutoka. “Subiri kwanza Anele. Sijamalizana na wewe.” Akabaki amemshika Nelly mkono. “Nakushukuru Nelly. Asante.” “Nakupenda Billy.” Nelly akanong’ona. Wakati Billy anataka tu kuinama kwa busu jingine Brandon akamuwahi. “Nope. That’s enough man! Mtachelewesha ratiba.” Wakacheka sana. “Fine. It was just a peck though!” “No, man! I saw that. It was NOT just a peck. Ulikuwa ukiiendea midomo kabisa.” “Hata mimi nimeona.” Beila akaongeza nakufanya wazidi kucheka. “Fine.” Billy akamuachia Nelly.

“Anele, kwa kuwa hapa si nyumbani kwangu, sina uwezo wa kukufukuza. Ila hukaribishwi kwenye harusi yangu. Eneo ambalo nitafanyia mimi harusi leo, huruhusiwi kusogea hapo. Huruhusiwi kufika jikoni ambako kuna vyakula na vinywaji vya harusi. Japokuwa sina amri juu ya hii nyumba, lakini nimeruhusiwa na wazazi kufunga ndoa hapa. Hivyo basi, kama utabaki hapa, nitataka uwe eneo la wazi ambalo kila mtu atakuwa akikuona. Nashauri iwe sebuleni. Ikitokea unaonekana eneo jingine lolote zaidi huku vyumbani ambako wageni wangu mimi wapo, zaidi Nelly, utakamatwa na kupelekwa polisi.” “Kwa nini!?” Anele akashangaa sana.

“Moja, nakuhofia kuwa karibu na Nelly pamoja na mtoto wangu aliyetumboni. Uchu wako wa mali zangu unaniogopesha sana, naona unaweza kufanya chochote ili kujinufaisha na pesa yangu. Chochote kitakachompata Nelly, hata food poison, wewe utakuwa mtuhumiwa wa kwanza.” “Naondoka.” “Hata ukiondoka. Omba Mungu chochote kibaya kisitokee leo. Maana umeingia kwenye hii nyumba kwa siri na kutokezea chumbani alipo Nelly. Sijui ulijuaje alipo! Sijui umepita wapi na umeshika nini, maana baadhi ya vyakula na vinywaji vilishaanza kuletwa tokea asubuhi.” “Sio sawa kwangu, Billy. Unaniadhibi bila sababu!” “Ilikuwa sawa kwako kumuanika Nelly hapa mbele za watu? Si kwamba ulitaka kumuharibia tu? Na je, nitajuaje kama umeridhika na kukubali kumuacha au kutuacha moja kwa moja kwamba hutatumia njia yeyote ile kuhakikisha unatimiza azma yako?” “Mami...” “Nyamaza Briana, na wewe sijamalizana na wewe.” Akamkatiza Briana.

“Umenielewa Anele?” “Mimi naondoka jamani. Na japokuwa nilipitia jikoni, lakini nilikuwa na Briana, hatukushika kitu.” “Briana.” Billy akamgeukia Briana. “Na hili nataka Anele ulisikie, ili mkitoka hapa mjue ni jinsi gani mtaendelea kuishi. Sitakulazimisha uishi kama Britney.” “Unampendelea Britney. Wakati wote unampendelea Britney, mimi hunipendi, dad.” Briana akaanza kulia. “Wala sijawahi kuonyesha upendeleo kati yenu ila wewe umekuwa ukinitenda ubaya Briana. Kila nilipotaka mahusiano na wewe, umekuwa ukinipa sababu zote za wewe kutotaka kuwa na mimi ila Carlos na mama yako. Ni lini wewe umeshawahi kunyanyua simu ya salamu kunisalimia tu, kama si kuniomba hela?” Kimya.

“Kila siku Britney kabla hajatoka kitandani kwake lazima atume ujumbe wa kunijulia hali kama amechelewa, lasivyo atapiga simu kunisalimia. Hata kwa sekunde 30 tu, lakini atanisalimia. Na lazima atanipigia simu jioni kujua nimeshindaje! Hataki pesa yangu kwa kuwa anasema pesa anayolipwa inamtosha. Muulize babu au bibi yako kama sijawatuma kumchunguza Britney ili tujue uhitaji wake ili niweze kumsaidia!” “Ni kweli.” Bibi yake akajibu. “Na wala hatujawahi kujua uhitaji wake. Anaishi maisha ya kawaida sana ambayo nafikiri ndio sababu anaweza kumudu garama zake.” Babu yake akaongeza. “Anko, Britney is a good people.” Junior akafanya wacheke jinsi alivyozungumza. Lakini wote wakamtetea kuwa yeye hana shida na anaupendo.

“Kisheria, siwajibiki kukutunza Briana. Ila nilifanya kama wazazi wetu walivyotufanyia sisi. Tafadhali amka Briana, angalia maisha jinsi yalivyo. Sijui mama yako huwa anakwambia nini, ila sisi kwetu hatuna kurithishana mali ila kusaidiana elimu, basi. Wote sisi tuliozaliwa na hawa wazazi, hatutamrithisha mtu kitu ila elimu.” “Mimi najua maana ni wimbo naimbiwa na mama kila siku.” Junior muongeaji kuliko wote akadakia tena.

“Ndivyo ilivyo sweetheart. Sina mali ya kukurithisha kwa sababu mimi si kama mama yako mwenye mahoteli huko Zimbambwe. Sina cha kukupa. Na kwa kuwa hutaki shule, usithubutu kunipigia simu na kuniomba pesa. Mkataba wangu mimi na wewe umekwisha.” “Si amesema atarudi shule!” Mama yake akaingilia. “Akiwa tayari kusoma, ndipo sasa wewe ambaye unaakiba yake, kutoka kwenye pesa mlizokuwa mkinidai, nikijua nimeshamaliza ada yake, utatumia hiyo akiba kumalizia ada yake. Umenielewa Anele na Briana?” Palizuka ukimya hapo, Briana hakuamini. Kwamba akafanye kazi!

“Unauhitaji wa pesa, fanya kama Britney. Wewe si wa tofauti. Tena kwa sababu umepunguza jukumu la shule, inamaana unaouwezo wakutengeneza pesa kwa kadiri utakavyo. Kama utataka lakini. Sikulazimishi kufanya kazi, ni pale utakapoona kuna uhitaji.” “Sio sawa Billy!” Anele akashangaza wote.

Billy akamgeukia Briana. “Mama yako alikwambia kama anahoteli zaidi ya moja huko Zimbambwe?” “Aliuz...” “Hayawahusu Briana. Huna haja yakuwaambia, baby.” “Kweli hayatuhusu. Ila kama hakukwambia, wakati ananipa talaka ili muanze maisha na Carlos, alitaka tugawane hata kichache alichokuwa amenibakiza nacho. Tukagawana mpaka salio langu benki. Alipoona sijakataa, akadai mahakama iniamrishe nimuachie ile nyumba kwa sababu yako wewe. Napo sikubisha. Na baba huyu nishahidi. Alisema Anele anabaki na wewe, si sawa kwako kuanza kuhamia sehemu ingine kimaisha, itakusumbua zaidi. Kwahiyo hata ile nusu aliyonibakisha nayo, nayo pia alikuja kudai. Ninachotaka kukwambia ni hivi, mimi sina uwezo kama alionao mama yako. Mama yako anamiliki nyumba zaidi ya moja. Mimi sina nyumba hata  moja. Huko Tanzania naishi kwenye nyumba niliyopewa na ofisi, niitumie wakati nikiwafanyia kazi zao. Nikishindwa kufanya kazi zao, inamaana na mimi nitakuwa sina pakuishi. Sijui kama unanielewa?” Briana kimya akilia.

“Narudia tena, sijui mama yako amekuwa akikwambia nini juu yangu, lakini mimi si tajiri kama pengine unavyodhania. Unaponipigia simu kunidai pesa, sina sehemu ingine ninayopata pesa isipokuwa ni kama hivi Britney anavyokwenda kazini kila siku, wanamlipa. Ndivyo hivyohivyo na mimi. Ila tofauti yangu mimi na Britney ni mimi inanilazimu kutoa kwenye mshahara wangu, kukupa na wewe nikidhani upo shuleni, nikitaka kukusaidia usome tu. Sasa kwa kuwa umeshakuwa mkubwa, unaelewa maisha ni nini, na wewe tafuta pesa za kujikimu. Ukitaka kurudi shule, rudi ila jua utakapokuwa na uhitaji, simu hazitakuwa kwangu tena kudai pesa ila wewe mwenyewe kufanya kazi kwa bidii na kukabiliana na maisha yako, au mama yako mwenye uwezo.” “Au Carlos.” Akaongeza Beila.

“Kwani Carlos ni baba yake? Acha kuzungumza kama mtoto mdogo, Beila!” Anele akawa mkali. “Hayo umeyagundua lini? Yaani sasa hivi, gafla Carlos sio baba yake!?” Beila akamuuliza kwa kumshangaa sana. “Siye huyu Briana aliyesema pale mahakamani kuwa Carlos ni baba bora kuliko Billy? Na si ametoka kusema hapa kuwa Carlos anampenda sana. Sasa atashindwa vipi kumsaidia akiwa na shida?” Beila akauliza. “Wakati akisema hivyo pale mahakamani, Briana alikuwa mdogo, auntie. Na ni mama ndiye aliyetufundisha wote tuseme hivyo. Briana hakuwa akijua jema na baya, ila kufanya kile mama alichokuwa akimwambia.” Britney akamtetea mdogo wake. Kumbe alirudi akawa amesimama mlangoni kabisa.

 “Sio kweli.” “Unabisha nini mama jamani!? Hukutukataza tusiseme ukweli kama tunavyojua na kuona jinsi tulivyokuwa tukishi? Wewe unafikiri ni kwa nini mimi nilikataa kuzungumza mahakamani?” “Kwa sababu ni jeuri.” Mama yake akajibu. “Hapana, ni kwa sababu ulitukataza tusizungumze tunachofikiria ila kile ulichotaka wewe kisikike siku ile, ndio maana mimi nilikataa. Na babu alipokuja kututembelea, ndio maana nilimlilia asiniache pale nyumbani kwa sababu wewe ulishaanza kuwa mkali kwangu. Na kuonyesha hasira.” “Wewe sasahivi utazungumza chochote sababu umesifiwa.” Mama yake akaongeza.

“Hata Briana si mtu mbaya. Naombeni tumpe nafasi. Dad, nakuahidi Briana atabadilika kuanzia leo. Mimi nitapata naye muda. Akikubali nitamchukua akakae na mimi kwa muda wakati akijipanga. Atatafuta kazi na kurudi shule.” “Mimi sitaweza kusoma na kufanya kazi.” “Hakika utaweza Briana. Labda mama yako akusaidie.” Billy akaweka msisitizo. “Utapata nafasi nyingine, lakini ambayo nilazima uilipie wewe mwenyewe garama, na sivinginevyo. Kama watoto wengine wanafanya, basi na wewe utafanya tu. Ukishindwa, chukua mikopo, utakuja kulipa ukimaliza chuo. Watu wengi sana wanafanya, wewe hutakuwa wa kwanza wala wa mwisho. Nashauri mtumie dada yako vizuri, atakusaidia maishani.” Billy akahitimisha kwa upande huo.

“Jamani, naomba tuhitimishe, mtupishe wote hapa ndani, ratiba inaendelea kama kawaida.” “Njoo Briana.” Dada yake akamfuata na kumshika mkono. “Dad, anaruhusiwa kubaki?” Britney akamuulizia mdogo wake. “Kama atataka. Sitamlazimisha kwa lolote.” “Mimi naomba abaki, dad. Nakuahidi atatulia. Si ndiyo Briana?” Akakubali akilia. “Basi twende kule chumbani kwangu.” Akatoka na mdogo wake na kumuacha mama yao hapo. Wengine wakaanza kutoka pia.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Jax akamsogelea dada yake. “Upo sawa?” “Kidogo. Nahisi nimeshituka sana.” “Nisikilize Nelly. Lara alipoteza mtoto kwa sababu kama hiyo. Tula alimfuata na kumvamia kama hivi. Pressure ikapanda, tukaishia kupoteza mtoto. Tafadhali tulia. Nimemsikia Billy yupo upande wako. Na hapa hutakaa kwa muda mrefu, umesema baada ya harusi tu unaondoka. Si ndiyo?” “Ndiyo.” “Basi Lara atakuwepo hapa, mpe maelekezo nini unataka kianze kufungashwa na mengineyo ili kukusaidia kuokoa muda. Najua hutaki kuchelewa popote. Tulia. Kila kitu kitakuwa sawa.” “Nashukuru Jax na naomba..” “Huhitaji kujieleza kwangu Nelly. Ulifanya kile ulichoweza kutufikisha hapa. Ila ukitaka kulizungumzia hilo, iwe baada ya kutoka fungate, umetulia. Sio sasa hivi. Na wala usione unawajibika kujieleza kwangu. Tafadhali tulia kabisa.” Hapo Jax akamfanya Nelly atulie. Walibakia wao wanne tu hapo chumbani. Lara, Billy, Jax na Nelly mwenyewe. Jax akampa maji.

“Naombeni na nyinyi mtupishe. Nahitaji muda na Nelly.” Billy akawafukuza Jax na Lara. “Nelly atakuwa sawa, Jax. Naomba uamini na wewe uondoke hapa unipishe.” “Sitaki kosa lililotokea kwa Lara, lijirudie kwa Nelly.” “Nakuahidi yeye na mtoto watakuwa sawa. Wewe ondoka.” “Nipo sawa Jax. Nahitaji tu kutulia ila kweli nahisi pressure imepanda. Sijisikii vizuri.” “Acha nichukue BP machine ya mama nikuangalie.” Billy akatoka, Jax na Lara wakabaki.

“Nielekeze nini chakufungasha.” “Hutaweza Lara. Huwa napangilia vitu vyangu kwa namna yake. Najua Jax anaelewa. Hapa kila kitu kipo kwenye masanduku. Vilivyo nje ni kwa kuwa bado navihitaji. Na kabla sijatoka hapa, ndio nitakuita ili uchukue baadhi ya mizigo yangu nitakayotaka mrudi nayo Tanzania. Mingine yote inaendelea na safari. Kwa hiyo nipo sawa. Acha aje anipime. Nikiona ipo juu, wala sitataka kuendelea na kupambwa. Nitalala kabisa ili nitulie.” Billy akarudi na machine yakupimia pressure pamoja na dada yake ambaye ni daktari.

Wakampima na kukuta sio mbaya ila juu kidogo. Billy akaangalia muda. “Unaweza kupata masaa mawili ya kulala. Naomba umwambie huyo anayetengeneza watu aje achukue vitu vyake aendelee na watu wengine, Nelly alale kabisa.” “Sasa na yeye kupambwa?!” “Naona Billy yupo sahihi Beila. Nahitaji kutulia kabisa. Sijisikii vizuri.” “Nahitaji afya yake na mtoto kuliko urembo wake. Hata akiwa hivi tukifunga ndoa, mimi sina tatizo.” “Nafikiri mpo sahihi. Uzima ni muhimu.” Beila akatoka. Lara akamvuta mkono Jax kama anayemzuia asitoke kwa haraka.

Nelly na Billy wakashangaa kidogo. “Mimi na Jax huwa tunaomba.” Lara akaanza akitetemeka. “Naomba tuombee hii siku nzima. Sitachukua muda mrefu.” Hata Jax hakutegemea. Akageuka vizuri akimtizama Lara. “Naomba tuombee amani, utulivu na furaha katika siku ya leo mpaka tutakapoondoka hapa.” Lara akaendelea akimwangalia Nelly kwa hofu. “Anasema nini?” Billy akamuuliza Nelly kwa kuwa Lara alizungumza kwa lugha ya kiswahili. “Anataka tuombee siku ya leo. Tuombee amani, utulivu na furaha.” Billy akacheka kama kawaida yake na kuongeza. “Wazo zuri sana, ila aombe kwa kingereza.” Lara alishituka nusura akimbie chumba.

“Hapana Billy! Utamnyima uhuru wa kuomba.” “Sasa mimi nitaelewaje!?” “Kwani anazungumza na wewe, Bill au unataka uchokozi tu hapa? Si anazungumza na Mungu! Wewe nishakwambia atakachozungumza na Mungu, utulie na uache kucheka. Unazidi kumtia hofu.” Eti Billy akajifunika uso na mto kwa haraka. “Yaani Billy wewe! Hakika sijakupatia mwenzio!” “Wewe umesema nitamtia hofu, nitamfanya ashindwe kuzungumza na Mungu. Na mimi nataka amani, utulivu na nini tena?” “Furaha.” Nelly akamjibu. “Yeap. Sasa kwa nini nisipunguze vikwazo.” Nelly akamtizama na kumwangalia Lara. “Achana naye huyu. Wewe omba. Kweli tunamuhitaji Mungu.” Nelly akamruhusu.

Mtoto wa mama Chiwanga akaanzisha sala kwa kiswahili huko uzunguni. Akamuombea mtoto wa Nelly tumboni. Akamuombea Nelly mwenyewe afya yake amani na uwezo wa kumbeba mtoto wake bila matatizo ya mwili. Akakemea magonjwa yote kwenye mwili wake. Akaombea harusi yao na kumbariki Jax. Ndipo akamaliza.” Nelly akaanza kucheka.

“Kwanza asante kwa kuniombea Lara. Nashukuru. Ila nina swali.” “Niambie na mimi, Nelly.” Billy akadakia. “Lara ameomba vizuri sana. Na wewe amekuombea.” “Oooh! Asante.” “Ila nina swali juu ya maombi yake kwa Jax. Huwa unambariki hivi kila siku?” Lara akacheka kwa aibu. “Huwa ananiombea hivyo mara kwa mara.” “Ndio maana siku hizi kichwa chako kimetulia!” Jax akacheka kwa masikitiko. “Kwani uongo?” “Mimi kichwa changu kilikuwa kimetulia tokea zamani.” “Mmmh!” Nelly akaguna kwa kutomsadiki mdogo wake. “Twende Lara, tumuache apumzike.” Jax na Lara wakatoka, wakamuacha Billy na Nelly.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

“Njoo ulale hapa nikukumbatie.” “Usiondoke nikipitiwa na usingizi, mpaka niamke.” “Japokuwa najua hakuna atakayeingia tena hapa, lakini sitaondoka. Usiwe na wasiwasi.” Nelly akajilaza. Na kweli akapotelea usingizini kwa haraka tu.

Akiwa usingizini akasikia “Nelly! Nelly!” Sauti ya Billy ikimuita taratibu kama asiyetaka kumuamsha kwa kumshitua. Lakini alikuwa amechoka, mwili hautaki tena kufanya chochote, sio kama asubuhi walivyoamshana kwa hamasa wakiambiana hiyo ni siku yao. Wakapeana mabusu mazito hapo kitandani wakitizamia penzi la fungate ndipo wakakiacha kitanda. Lakini mchana huo Nelly amelala hapo, moyo hautaki tena kama mwili wake. Akabaki amejilaza tu bila kuitika japo Billy alijua amemsikia.

Akamsikia tena Billy, “The More You Take The More You Leave Behind. Who Am I?” Nelly akajua anampa hicho kitendawili makusudi ili afikirie mpaka usingizi uishe. Na kwa kuwa Billy alimjua kwanza ni ‘light sleeper’. Kwamba huamka kirahisi sana. Hata yeye huwa hawezi kutoka kitandani kabla ya Nelly kama anataka Nelly apumzike. Hata kwa kwenda chooni wakati wa usiku au kujigeuza mara nyingi hapo kitandani, huwa Nelly anaamka. Kwa hiyo hata hapo alijua amemsikia, hana haja ya kurudia. Pili alimjua Nelly hapendi kushindwa. Akajua lazima hapo alipotulia, anafikiria. Akamuacha.

Alipomuona anatabasamu, hajafungua macho, akaanza kucheka. “Wewe sema kama umeshindwa.” “Si kirahisi hivyo.” “Sawa Nelly.” Nelly akamgeukia. “Nina jibu, lakini sina uhakika.” “Na unapata nafasi moja tu ya kukosea. Kwa hiyo kuwa mwangalifu.” Nelly akatulia kidogo kisha akamwangalia tena. “Gari.” Akajibu. “Mmmh! unakaribia ila sio jibu.” “Billy wewe! Mimi nahisi wewe mwenyewe hujui hicho kitendawili.” Billy akacheka sana. “Yaani mleta kitendawili hajui jibu?” “Hushindwi kutunga tu jamo ili kunisumbua.” “Sawa Nelly. Ila mimi nakwambia hilo sio jibu lake.” “Basi katika hilo jibu lako ongeza na hili langu. Maana linaleta maana. Yaani, jinsi gari inavyotembea, inachukua umbali zaidi, na kuacha umbali nyuma.” “Wewe tunga cha kwako na uweke hilo ndio jibu lake. Acha kulazimishia majibu kwenye riddle yangu.” Akamuona ametulia. Akajua anafikiria tena. Hakubali kushindwa. Billy akacheka sana na kutoka hapo kitandani.

“Usikimbie sasa!” “Nakwenda kutumia choo, nitarudi kuja kusherehekea kukuweza.” “Si kirahisi hivyo Billy. Ukirudi nitakuwa na jibu. Ila ujue nafasi ya kujaribu zinakuwa mara nne.” “No way!” Billy akakataa kabisa. “Mimi ndio nimekupa kitendawili na mashariti ya kujibu.” “Sijakataa. Mimi mara mbili, na mtoto mara mbili.” Billy alicheka mpaka akarudi kukaa. “Nelly!” “Kumbe! Wewe unavyosema nile, kunywa na kuishi nikijua sasa hivi tupo wawili kwenye huu mwili, unategemea nini? Ndio ujue tupo wawili kwenye kila kitu. Ila kwa jinsi ya akili ya huyu mtoto na mimi mama yake tulivyo, usiogope, dad. Hatutatumia nafasi zote tatu zilizobaki. Tutakuwa tumeshapata jibu.” Billy akacheka sana. Ila kwa furaha kuona kwa mara ya kwanza Nelly anazungumzia ujauzito wake akitambua mtoto aliyebeba na kumuunganisha na yeye. Akajua ni kweli ameanza kukubaliana na matokeo.

“Sawa Nelly. Ila siamini kama umeshaanza ku play pregnacy card! Hayo ni matumizi mabaya ya huo ujauzito.” “Ndio ukweli wenyewe. Wewe tupishe tufikirie.” Billy akatingisha kichwa kwa masikitiko akicheka na kuelekea maliwatoni. Akiwa chooni akamsikia Nelly akimuita kwa kuhamasika sana. Akajua amepata jibu la hakika na hataki kusubiri. “Nitajikojolea Nelly!” “Nimepata jibu. Ni footsteps. Hapo huwezi kubisha.” Akamsikia akicheka sana huko chooni. Akajua amepatia.

“Yes!” Nelly akajipongeza. Billy akatoka akicheka. “Kweli mwanangu anakusaidia sana.” Nelly alicheka mpaka machozi. “Sio akili yangu mwenyewe?” “Wewe ulishashindwa. Hiyo ni akili ya mwanangu. Hongera sweetheart. Akambusu Nelly tumboni. Utakua na akili kumzidi mami wako?” “Nahisi ni kukuzidi wewe dad. Maana amepata nafasi ya kwanza na kuitendea haki.” Billy akazidi kucheka. “Mimi sina shida ya kupitwa na mtoto, Nelly!” “Mimi  nina shida.” Billy akazidi kucheka akimjua Nelly, kweli hapendi kushindwa.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Wakasikia mlango ukigongwa taratibu. “Ni mimi, dad.” Sauti ya Britney. “Unapenda kucheka kwa sauti wewe! Nyumba nzima wameshajua tumeamka!” Billy akakimbilia mlangoni. “Hey baby girl.” Akamfungulia kwa furaha. Nelly alijua jinsi Billy anavyompenda huyo mtoto, kuliko nafsi yake. “Umependeza sana, sweetheart.” Akamsikia Billy akimsifia. “Asante dad. Naweza kuongea na Nelly?” Billy akarudisha kichwa ndani kumtizama Nelly pale kitandani. Nelly akatingisha kichwa kukubali akimjua huyo mtoto jinsi alivyo mwema. “Ingia.” Billy akampisha mangoni.

“Vipi Britney?” Akamsogelea pale kitandani. “Kwanza umependeza sana.”  Britney akacheka lakini akionekana ana jambo anataka lazima kuzungumza. “Asante. Wanamalizia kutengeneza wengine ili waje kwako.” “Hamna shida. Vipi?” Akatulia kidogo, baba yake akiwa nyuma yake. Wote wakampa muda wa kujipanga na kuzungumza. Akamuona baba yake anambusu kichwani kwa nyuma taratibu kama asiyetaka kuvuruga nywele. Britney akacheka taratibu na kugeuka. “Thanks dad.” Billy akamkumbatia. “Si unajua unaweza kuongea na Nelly chochote?” Akajua anamtuliza na kumtia moyo aongee.

Akabaki amesimama na baba yake, amemkumbatia kwa upendo. Wakamuona anacheka. “Ni nini?” “Kwanza nataka kumuombea msamaha Briana. Kabla dad hajasema chochote, acha nimalizie.” “Mimi sitaingilia. Wewe umesema unataka kuzungumza na Nelly. Ila nitataka kujua huo msamaha unatoka kwake au ni wazo lako?” “Labda nimwambie Nelly ukweli pengine italeta maana.” Akaendelea Britney. “Wakati mama akidai talaka, Briana alikuwa mdogo na hatukutaka au alifichwa mambo mengi ili isimuathiri. Hakuwa akijua kinachoendelea kabisa. Hata mimi sio kwamba niliambiwa. Ila nilikuwepo nyumbani, nilijua kinachoendelea, dad akiwepo na wakati hayupo. Kuna mambo hata kabla mami hajaomba talaka alikuwa akituambia mimi na Briana, juu ya dad, lakini kwangu hayakuwa yakileta maana kwa vile nilivyokuwa nikimuona dad anavyokuwa kwetu na hata kwa mama mwenyewe, pale dad anapokuwepo nyumbani.” Britney akaendelea.

“Kwa haraka sana mimi nikajua kama kuna ukuzwaji wa mambo. Alichokuwa akikizungumza mama kwetu ni kama kukuza au kuweka tatizo ambalo kwanza halikuwepo na dad mwenyewe alionekana ni kama hajui kabisa kama hilo tatizo lipo. Kwa jinsi dad alivyokuwa akiishi pale nyumbani anaporudi. Kwa hiyo kwa upande wangu nikawa napata muda wakumwambia Briana kile ninachojua kitamsaidia. Kuwa dad anatupenda sana, ila inamlazimu kufanya kazi ili sisi tuishi vizuri. Kwa kifupi tu ili kumfanya asihisi tupo kwenye mazingira mabaya. Na ukweli hakuwa akielewa sana kwa kuwa hata mama alipokuwa akitaka kuanzisha ugomvi, dad alikuwa akitaka wakazungumzie nje kabisa wala si chumbani au pale ndani ambako sisi tupo. Kwa hiyo mara nyingi maneno yaliyokuwa yakiendelea kati yao, yaani kati ya dad na mom, dad aliyaweka kwa kificho ili kupunguza wasiwasi kwetu pale nyumbani.” Britney akaendelea taratibu tu.

“Ninachotaka kukwambia, ni kuwa, mimi nilikuwa nikijua mambo mengi kuliko hata Briana na dad, kwa kuwa nilikuwa mkubwa, niliweza kujua kinachoendelea tukikuzwa katikati ya hawa wote watatu. Dad, mami na Carlos. Lakini si Briana. Na tabia ya Briana kutaka vitu vizuri na kuhakikisha anavipata ni tabia iliyopo ndani yake ila tu hajapata uongozi mzuri ya jinsi ya kujipatia yeye mwenyewe. Nimetoka kuzungumza naye hapo chumbani nikijaribu kumuelewesha na kumpa uhalisia wa mambo zaidi maisha kwa jumla. Anaonekana ameanza kuelewa, ila anahitaji muda. Hajui maisha mengine bila mama. Hawezi kuishi kwengine ila na mama. Mama anamjulia sana Briana. Na ni marafiki wale ambao wanasindikizana kila mahali. Ila ameanza kuelewa. Anaomba msamaha kwa kuwaingilia. Hakuwa hata akijua kama mama ndiye aliyeomba talaka. Yeye alijua dad aliamua kututelekeza ndio Carlos akawepo kumsaidia mami.” Billy akaumia sana.

“Alikuwa akijua dad alichagua maisha yake zaidi yetu sisi. Na sio kosa lake. Alifichwa na kila mtu, akabaki kusikiliza upande mmoja tu. Tafadhali naomba msamehe. Sio mtoto mbaya. Na usibadili mawazo juu ya baba hata juu yetu.” “Nimekuelewa Britney. Na asante.” Nelly akajibu hivyo tu kwa jumla. “Utamsamehe Briana?” Akamuuliza Nelly kwa upendo kama alivyo, akiwa amejua ametoa jibu la jumla sana.

“Acha nikwambie ukweli Britney. Hapa si kwenye kusamehe au kutokusamehe, kwa sababu wote tunajua ni zaidi ya hichi alichokifanya hapa na mama yenu, au kushindwa hata kunishika mkono kwa salamu, au kuniuliza maswali mabaya mbele ya watu, akionyesha kunidharau na kutaka kunidhalilisha. Sidhani yeye kama Briana anashida na mimi kama Nelly, ila mwanamke yeyote anayejaribu kuonekana kuchukua nafasi ya mama yenu kwa baba yenu. Hata kama nikisema sitamsamehe au ninamsamehe yeye, ukweli haitajalisha kwetu sisi wawili. Nikimaanisha mimi na yeye kama mtoto wa Billson.” Nelly akaendelea.

“Kama ulivyosema. Anahitaji muda. Basi apewe muda na mimi nina mambo mengi, hamtanisikia hata kuwabugudhi. Pale mnapohitaji msaada wangu, mnijulishe kwa njia yeyote ile, hata kupitia baba yenu nitafanya kwa kadiri ya nitakavyoweza. Lakini ninachotaka kukuhakishia Britney, nampenda baba yenu, na sitaki kumtumia kifedha. Mimi sina shida na hela ya baba yenu hata kidogo. Yaani hata akiniacha leo na huyu mtoto, kifedha nakuhakikishia tutakuwa sawa kabisa wala hatutahisi kupungukiwa ila kumkosa Billy kama Billson mwenyewe. Hilo tu.”

“Nampenda Billy na ninamuhitaji. Hapa nilipofika, hakuna mtu atafanya nisiwe naye, hata kama ni mara moja kwa mwezi ndio nitakuwa nikimuona, mimi sitajali, ilimradi najua nipo naye. Nishafikiria, nishahesabu garama zakulipa na faida, nikaishia kuona mizani inalemea kwenye faida za kuwa na baba yenu. Anachohangaikia kwenye maisha ni kama mimi tu. Hatuna tofauti. Najua maana ya kufanya kazi kwa bidii, kujituma zaidi ya unavyotakiwa na kulipwa, na uthamani pamoja na nidhamu ya pale milango inapofunguka mahali. Kwa kuwa na mimi nimekua si kama nyinyi Britney. Mimi nimejikuza kwa shida sana huku nikimkuza huyu mdogo wangu. Nimepambana sana kufika hapa nilipo nikisubiria milango migumu ifunguke ili niweze kuingia. Najua maisha kwa kuyaishi. Na namjua binadamu kwa kuishi nao.”

“Pressure ilipanda si kwa maneno aliyoyasema mama yako na Briana. Hata kidogo. Mimi namfahamu mwanadamu. Najua anaweza kugeuka mbaya kuliko simba mwenye njaa. Ila nafikiri nilishitushwa na kule kuvamiwa kwao, nikiwa tayari na tension ya maandalizi, na mambo mengine mengi. Billy ananijua. Napenda vitu vizuri ndio maana nafanya kila kitu changu mwenyewe na kwa bidii. Na ninapenda kwenda na muda. Siwezi kuchelewa popote pale. Ndivyo nilivyo. Kwa hiyo sio mzuri sana kufanyiwa mambo na baba yako ndio yupo kwenye kunisaidia. Siwezi kufanyiwa mambo na zaidi nikiwa sijui kinachoendelea. Nataka kusimamia kila kitu mpaka kuona mwisho wake. Sasa kitendo cha kukaa hapa ndani, jambo letu muhimu likiendelea huko nje, halafu sijui kinachoendelea, ila kuambiwa tu tulia, usiwe na wasiwasi, tayari sikuwa sawa. Nipo stress out.” Billy akacheka.

“Billy ananijua. Anyway, kingine huu ujauzito umekuja na pressure.” “Pole Nelly.” “Asante. Sio mbaya sana, ila huu mwili huwa unatafuta sababu yeyote ile ili kuipandisha. Ninachotaka kusema kwako ni, acha muda ujibu kila kitu. Tusiwe na haraka ya kesho kabla hatujaishi leo. Leo naolewa na Billson. Na wewe ni mmoja wa wasimamizi wangu, hilo nimeliheshimu sana, Britney. Asante kunipokea na kuniamini bila kunifahamu.” Britney akacheka taratibu. “Karibu Nelly. Nataka dad awe na furaha kama hivi ninavyomsikia anacheka sasa hivi! Mpaka bibi alikuwa anasema Billy wake wa zamani amerudi. Dad alibadilika, Nelly!” “I am standing right here!” Nelly na Britney wakacheka vile Billy alivyosema wasimtete, anasikia.

“Huyo nimekutana naye akicheka hivyohivyo.” “Anapenda kucheka kama babu na baba mkubwa. Lakini hakuwa akitoa kicheko cha kutoka rohoni cha kweli.” “Britney!” Baba yake akajidai kushangazwa kwa kuumia sana akishika moyo. “Kweli dad! Ila nakupenda.” Wakazidi kucheka hapo. “Baba yako ananijua. Nikikusudia kufanya kitu, huwa nafanya kwa juhudi zangu zote. Leo naolewa na Billy, hakuna kitakachonibadii mawazo labda Billy mwenyewe akatae. Ila si kwa maneno ya yeyote yule au vitisho. Hata pressure ipande vipi, leo nitaolewa na bili hata wodini, nitaita atakayefungisha ndoa, hili limalizike leo, wala si kesho, Mungu akipenda. Kwa hiyo usiwe na wasiwasi kabisa. siwezi kubadilika kwa baba yako. Sisi wawili tupo sawa kabisa.” “Asante Nelly. Ni sawa nikiku hug?” Akaomba kumkumbatia kwa upendo. Nelly akacheka. “Karibu.” Akaenda kumkumbatia pale kitandani.

“Ila na wewe ni mzuri Nelly. Hata babu amekusifia.” Nelly akacheka. “Asante Britney.” “Acha niwaite watu wa kukutengeza wakuweke sawa kabla ya harusi. Shangazi ameondoka na kuniachia maagiza ya usisumbuliwe kabisa. Unywe maji mengi na lazima utengenezwe vizuri.” “Nitamshukuru Beila baadaye. Lakini kwa sasa nipo sawa.” “Basi nakupisha kwa muda. Baada ya dakika 20 wapiga picha na wachukua video, pamoja na wasimamizi wote wa kike tutakuja kupiga picha za kitandani tukiwa na robs zetu, ndipo tukavae, tuje tupige tukiwa na nguo rasmi. Kila kitu kipo vizuri. Hakuna kitakachoharibika. Tumejipanga vizuri.” “Bora umuhakikishie wewe.” Billy akaongeza, wakacheka, Britney akatoka.

“Acha nikupime pressure kabla sijawaruhusu waingie wakutengeneze.” “Sitamani mtu anishike tena Billy. Sijui kwa nini! Natamani hata kubaki hivihivi tu.” “Jikaze utengenezwe. Huu ni ukumbusho wako wa muda mrefu. Utakuja kujichukia kama hutatoka kama ulivyotamani. Tuna siku nyingi tu za mapumziko, utapumzika tukiwa sisi wawili tu bila mtu mwingine. Jikaze.” Baada ya yote, Nelly akafanikiwa kutengenezwa na picha kupigwa hapo chumbani akiwa na wasimamizi wake kisha kubakiwa na msimamizi wake, ambaye ni mke wa Brandon, akamsaidia kuvaa.

Nelly&Billy


Ukweli Nelly alipendeza sana. Walimpamba kwa ustadi wa aina yake. Alivaa nadhifu mno. Hakuvaa shela ndefu sana wala nguo kubwa, lakini alipendeza na kuzidi kuvutia. Alikuwa akichukuliwa video wakati akishuka ngazi yeye mwenyewe mpaka mlango wakutokea nje. Nje ya mlango wa sehemu ambayo wanafungia harusi alikuwa amesimama Jax akimsubiria atoke amshike mkono akamkabidhishe kwa Billy. “Umependeza sana Nelly.” “Hakika siamini kama ni mimi leo eti nimevaa shela, nafunga ndoa! Kweli maisha hayatabiriki!” Jax akacheka. Wawili hao walikuwa wakizungumza pale Nelly alipotoka tu na kukutana na Jax akitaka kumshika mkono, watu wakiwa wamesimama baada ya Nelly kutoka tu nje. “Hongera kwa kukubali kubadili maisha Nelly. Naamini utaendelea kuwa na furaha.” “Kweli Jax, au unanitia tu moyo kwa kuwa unaona nishaianza safari?” “Kabisa Nelly. Billson anaonekana kukupenda sana. Utakuwa na furaha.” “Na mimi naamini hivyo kama hatanibadilikia.” “Acha kukaa mkao wa kusubiria baya litokee. Kuwa..” “Come on Jackson!” Akasikika Billy na kuamsha kicheko kwa wote.

“Unachukua muda wangu wote na Nelly, bwana! Unazungumza nini humalizi? Wewe mlete hapa mbele, niachie mwenyewe.” “Sawa Billson.” Jax akamshika dada yake na kuanza kutembea kuelekea mbele alipokuwa amesimama Billy, kaka yake na wasimamizi wengine pamoja na mchungaji.

Harusi ya Billy na Nelly ikafungwa palepale nyumbani kwao ila nyuma tu kwenye ua. Palitengenezwa vizuri sana. Ukweli Billy alionekana amefurahia sana. Billy alitaka wimbo wa ‘Your my african qeen’ uwe unarudiwa rudiwa kila wakati na baadaye wakafungua mziki kwa kucheza wimbo wa taratibu wa George Benson wa ‘Nothing’s Gonna Change My Love For You’. Aliimba Billy huku akicheza na Nelly, mpaka watu wakaelewa safari hii amepata mwanamke anayempenda. Aliimba akiwa amewekewa kipaza sauti kile chakushikiza kwenye tai aliyokuwa amevaa, sauti yake ilisikika vizuri sana kupitia kipaza sauti hicho kidogo tu, akimwambia Nelly, ‘hakuna kitakachobadilisha mapenzi yake kwake’. Akaendelea kumuimbia huku amemshikilia vizuri wakicheza.

Walipomaliza wakamuona anamnong’oneza kitu Nelly, akatingisha kichwa kukubali, akambusu na kutoka kwenye dance floor, sehemu waliyokuwa wakichezea akaenda kumnong’oneza kitu Jax. Jax akasimama na kwenda kucheza na dada yake, yeye Billy akaenda kumuomba binti yake wacheze naye. Britney alifurahi sana. Akasimama na kumbusu baba yake, akaenda naye karibu na Nelly. Kama waliojua, wimbo ukabadilishwa kwa haraka, ukawekwa wa Whitney Huston wa ‘I will always Love you’. Alilia sana Britney kila maneno yalipokuwa yakirudiwa na baba yake, kuwa hata akiondoka, akimaanisha akibadili maisha yake kuwa na Nelly, lakini wakati wote atabaki akimpenda. Britney akachukulia kama anamwambia upendo wake kwake utabakia vilevile hakuna kitakachobadilika daima. Akamlalia baba yake begani wakiendelea kucheza. Briana akabaki ameinama sehemu aliyoachwa na dada yake. Billy alicheza na binti yake huyo mpaka akamaliza.

Akamrudisha na kumvutia kiti akakaa. Kisha akamsogelea binti yake mdogo pale alipokuwa amekaa pembeni ya dada yake, akamuomba wakacheze. “Nilijua umenichukia, dad!” “Never sweetheart. Hata iweje, sitakuchukia.” Akamnyoshea mkono, Briana akapokea mkono wa baba yake akijifuta machozi. Akasimama na kurudi pale katikati sehemu ya kuchezea. Wakarudia tena wimbo uleule kama aliomuimbia dada yake. Ila Billy akaanza kwa binti yake. “Unaweza kusahau kila kitu juu yangu Briana. Lakini nataka ujue hili, wakati wote utabakia kuwa my little princess. Nakupenda sana, sweetheart. Na sijawahi kubadilika kwako na hakuna atakayechukua nafasi yako kwenye moyo wangu. Ila nataka usichelewe kwenye maisha. Ishi maisha ya uhalisia. Na nataka uanze kuishi mimi nikiwepo. Nakuahidi kukushika mkono, endapo utanipa nafasi, au ukinichagua nitembee na wewe.” Briana akalia sana. Na yeye akamuimbia wimbo uleule kama dada yake. ‘I will always Love you’. Akamuimbia mpaka ukaisha. Ulipobadilika tu na kurudiwa wimbo wa, ‘Your my african qeen’. Jax akaenda kumchukua Lara. Wakarudi naye kucheza pale mbele. Billy akapenda jinsi wanavyoucheza huo wimbo, akaanza kufuatisha. Walicheza usiku huo wakicheka mpaka Nelly akasahau swala la ujauzito wake na Anele. Baada ya harusi kuisha wawili hao walitoka hapo kuelekea fungate.

Lara&Jax.

K

esho yake Jax na Lara wakapelekwa uwanja wa ndege kurudi nchini Tanzania. Jax alitakiwa kazini. Ikawa kama mchezo tu, dada yake ambaye hakuwa hata na mipango mingi juu ya ndoa, ndio akaolewa kwa haraka bila kikao cha harusi wala mipango ya muda mrefu, na baraka ya mtoto juu. Wakiwa kwenye ndege Jax akaanza. “Nakupenda Lara. Na nakusubiria kwa hamu kwenye siku yetu na sisi.” Lara akacheka. “Na safari hii nasema wazi kabisa, nataka watoto.” “Wangapi?” Lara akauliza akicheka. “Nguvu yako tu.” Lara akafurahi sana. “Hata watano!?” “Ukiwa na uwezo huo, mimi sina shida.” “Jax! Huogopi garama za maisha?” “Nikikwambia hivyo nitakuwa nakudanganya Lara. Wewe unajua historia yetu mimi na Nelly. Hapakuwa na mipango mingi tuliyowekewa na wazazi wetu kwenye maisha, lakini si unaona tulipo? Wewe mwenyewe umekuwa ukinifundisha juu ya mipango ya Mungu kwa mwanadamu. Wala si mipango ya mwanadamu kwa mwanadamu mwingine. Japo mimi kama baba sitazembea na kufanya kosa kama baba yangu. Nakusudia kufanya vizuri zaidi. Lakini sitaogopa.” Hilo likamfurahisha sana Lara.

“Mwenzio napenda watoto, Jax.” “Hilo nimekuja kugundua kwako. Sikuwa nikijua kabla.” Akamuona Lara ametulia kabisa, anataka kupotea pale kimawazo. Akajua kumbukumbu zinataka kumrudisha vile alivyopoteza mtoto. “Mungu atatujalia wengine Lara. Tafadhali jipe moyo.” “Naamini hivyo Jax. Sijui kwa nini yule mtoto ananiuma sana! Huwa nakaa nahesabu, najiambia pengine nisingefanya hili au lile, leo angekuwa amefikia hiki au kile! Umri huu au kile! Ilimradi tu. Ila tuache hilo. Nimefurahi kama huna shida na kuwa na watoto wengi.” Jax akatulia kidogo.

“Nikuulize swali?” Lara akamgeukia. “Huwa ukikumbuka hivyo unanichukia?” “Hapana Jax! Hata kidogo! Kwa nini unafikiria hivyo?!” “Sijui!” “Hapana. Unajua mama aliniambia Mungu huwa akipanga jambo lake hakuna mwanadamu anaweza kusimama na kuzuia. Akaniambia wapo wanawake huwa wanapigwa na waume zao kila siku na bado wanauwezo wa kubeba mimba na kuzaa. Kama Mungu angeona wakati ule nina uwezo wakumlea yule mtoto, angeacha niwe naye. Nahesabu ni kama Mungu alimchukua kiumbe chake, aliona sipo tayari naye au hapakuwa na mazingira mazuri yakumlea. Simaanishi kifedha, ila pengine hata mimi. Sijui Jax. Kuna mambo mengine hayana majibu. Lakini kwa hakika sikuchukii. Au unafikiri ni kwa kuwa hatufanyi mapenzi?” “Eti nakuhisi umebadilika Lara. Siye Lara ninayekufahamu. Siye Lara unayetaka nikuweke mikononi.” “Ni kwa sababu ya kukataa usinikumbatie jana usiku?” “Sijui Lara.” Jax akajibu kama ambaye anakata tamaa.

 “Jax, amini nakupenda na kukutamani sana mpenzi wangu. Jana nilikuwa nimezidiwa, nikajua ukinishika tu pale kitandani, naweza kuamka asubuhi na majuto na kujichukia sana. Nilitamani sio unishike tu. Nilikuwa natamani unifanyie kila kitu ndio maana nilikuwa nakukwepa. Nahisi nipo mwenye siku za kushika mimba ndio maana nimepandisha joto na hamu ilinizidia. Ila sio kwa sababu nakuchukia Jax. Nisingekuwa na wewe kama najilazimisha. Sina sababu Jax. Na sitafanya hivyo.” “Kufanyaje?” “Eti kujilazimisha kuwa na wewe! Hapana Jax! Sina sababu yakufanya hivyo. Kwa nini kwanza? Nakupenda Jax na ndio maana nipo na wewe na nakusubiria kwa hamu.” Jax akaridhika.

“Nelly ameniambia mambo yanaenda vizuri. Naamini tutafanya kila kitu kwa wakati. Na nimebania siku zangu za likizo ili nizichukue zote kama zilivyo tukapate muda mrefu wa pamoja baada ya harusi yetu. Tutakuwa na wakati mzuri sana.” “Mimi mwenyewe nasubiria kwa hamu. Nakupenda Jax. Huna makuu. Rahisi kuishi na wewe. Namimi nakuwa kama Nelly. Nakutaka wewe, sibadiliki hata iweje.” Wakacheka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Nelly alirudi nchini akiwa amepata mapumziko ya kutosha. Mke wa Billy, kazi na ujauzito ambao unao mume.  Akawa ametulia, akili kwenye harusi ya mdogo wake. Ndani ya miezi mitatu akawa amekamilisha harusi ya Jax. Lara akawa amejawa furaha, ndoto zake zimetimia. Gauni alilokuwa kiota tokea mtoto, akawa amelipata tena la hadhi zaidi ya alivyotaraji. Jax ni wake na Nelly anampenda, yupo upande wake. Alikuwa akimuhangaikia na mimba ya miezi saba lakini akawepo mstari wa mbele kuhakikisha jambo haliharibiki.

Siku mbili kabla ya harusi yake akiwa ofisini akashitukia shemeji yake amemsimamia. “Siku ya harusi yangu sikumbuki kama ulinipa zawadi.” Jax akakunja uso akimwangalia Billy. “Nimekuja kukwambia kuwa hujachelewa.” Jax akabaki akimwangalia na uso wa sikuelewi, na Billy naye akabaki amesimama kama anayesubiria. “Unataka zawadi gani!?” Ikabidi Jax amuulize. “Umeuliza swali zuri sana. Sasa, nataka kujua jinsia ya mtoto wangu.” Jax akakunja uso. “Hapo ndipo wewe unakuja. Fanya juu chini umlazimishe Nelly, akaangalie jinsia ya mtoto.” Jax alishangaa mpaka akarudisha kiti nyuma na kubaki akimtizama Billy.

“Naanzia wapi!? Hivi unajua mimi na Nelly hatuzungumzii mambo kama hayo?” “Na hivi unajua ni wewe peke yako hapa duniani ambaye Nelly hawezi kusema ‘hapana’ kwako hata kama umemuudhi?” “Billy!” “Hakika nahitaji msaada wako Jax, na nilazima unisaidie. Nelly amekataa kabisa, na mimi mama ananiulizia kila wakati. Mpaka muda mfupi uliopita amenipigia kutaka kujua jinsia ya mtoto!” “Sasa ni kwa nini humwambii Nelly mwenyewe?” “Nelly amekataa. Na amesema niwaambie nyumbani kwetu wote wasubiri mpaka ajifungue.” “Sasa kwa nini huheshimu hilo?” Jax akamuuliza. Akamuona anauma meno huku akisema. “Shhhhhhh, nope!” Akakataa.

“Billy!?” “Siwezi kusubiri mpaka siku anazaliwa eti ndio nakwenda kukutana na mtoto nisiyemjua! Hapana! Nataka kuandaa jina kabisa. Yaani siku ile anazaliwa, nakwenda kukutana na mtoto ninayemfahamu. Hapo sasa ndipo unapokuja wewe kusaidia.” “Sidhani kama nitaweza kuwasaidia, Billy.” “Usijali. Nimeshaanza kukutengenezea mazingira mazuri. Kliniki ya kesho, nitamwambia uende naye wewe. Atashangaa kwa sababu kesho ni siku ya kuangalia mtoto, anategemea ning’ang’anie kwenda naye, lakini mimi nitajidai nipo busy, ili wewe uende naye. Mkiwa njiani na kule sasa ndipo umwambie unataka kujua jinsia ya mtoto.” “Nelly anaakili sana, atagundua ni wewe umenituma!” “Sio kwako. Kwako huwa hafikiriii.” Jax akabaki akimtizama.

“Tafadhali Jax.” “Siwezi kumdanganya Nelly. Wewe nipe siku ya leo, nitazungumza naye.” Billy akavuta punzi kwa nguvu, kwa furaha. “Do you Jax. Do you man.” Akamwambia hivyo akimpigapiga mgongoni, kisha akaondoka kwa furaha akimwambia afanye vile awezavyo yeye.

Hapohapo Jax akampigia simu Nelly. “Naweza kukuona mida ya jioni?” “Nakuja hapo ofisini kwenu kumsuprise Billy. Amekuwa akinisumbua anataka kujua jinsia ya mtoto.” “Umeshajua?” “Nimejua. Nilienda leo sehemu kumuangalizia, ili amwambie mama yake, waache kunikera. Kwa hiyo nakuja hukohuko, nitakupitia na wewe.” “Huna haja ya kuja. Nilitaka kuzungumza na wewe juu ya hilo.” “Usiniambie na wewe alikufuata kwa ajili ya hilo!?” Jax akacheka na kumjibu. “Inaonekana kwao inamaana kubwa sana.” “Hana lolote huyo Billy. Ni mpenda kujua tu mambo. Acha nikazungumze naye.” “Ni mtoto gani?” Jax akauliza. “Acha kwanza nikamwambie yeye wa kwanza, yeye mwenyewe ndio akwambie. Akijua wewe umejua kabla yake anaweza kuumia.” Wakacheka na kuagana.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kitendo cha Billy kujua Nelly amebeba mtoto wake wa kiume, ikawa shida. Kila mtu alijua mtumzima huyo anatarajia mtoto. “Wewe si ulisema hujali jinsia wewe?” “Hata angekuwa wakike pia ningefurahia tu.” Nelly akamtizama kwa kumsuta, lakini kwa hakika wote walifurahia huyo mtoto, wakaongeza kitu kingine wanachokitizamia kwa hamu, wakijua ni jukumu si la kutumia tu akili na pesa, ila wao wenyewe kama wazazi. Na Billy alionekana kuwa na furaha na Nelly, zaidi ya walivyotarajia. Akawa akilala akiwa na uhakika wa kuamka pembeni ya Nelly wake.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

          Jax alihamia kuishi nyumbani kwa Nelly kwa muda wakisubiria harusi, kwani Nelly ni kama alihamia anakoishi Billy, Lea naye alishakuwepo jijini tokea Lara na Jax wanarudi nchini kutoka Uswiz. Akawa akiishi hapo na mdogo wake. Kwa hiyo hata ndugu wa Lara walitua jijini mapema tu tena wakiwa na furaha wakiwa na tumaini safari hii harusi ipo tena wakiwa na uhakika na sehemu ya kufikia. Nyumbani kwa Jax na Lara. Japokuwa Lara alimwambia Jax angeenda mwenyewe kuwapokea ndugu zake kituo cha mabasi, lakini na yeye Jax akataka kuwepo. Wakaongozana kwenda kuwapokea na kuwapeleka nyumbani kwao.

           Baada ya chakula cha usiku cha pamoja, Nelly na Billy nao wakiwepo kuwakaribisha, mama Chiwanga akaona atoe neno la shukurani. “Nelly mama, Mungu akubariki kwa kusimama na wanangu. Kumpa kazi Lea na kusaidia Lara kwenye kila hatua ya harusi yake. Na wewe Mungu akuinulie wakusimama na wanao.” “Ni mmoja tu mama yangu. Hii shuguli sirudii tena.” Nelly akawahi kwa haraka nakufanya wacheke.

          “Kamoja kama dawa, mama!?” “Kabisa baba yangu. Huyuhuyu. Sitaongeza. Na umri wenyewe umekwenda. Sitaki Jax aje alemewe kusomesha baadaye.” “Basi mimi nakuombea umri mrefu. Usomeshe mwenyewe, ulee mpaka uje umkabidhi kwa mkewe kama hivi unavyohangaika kwa Jax na wanangu, basi na wewe Mungu akutendee.” “Amina mama yangu. Hilo nashukuru.” “Kabisa mama. Huyu Lea alishachoka hiyo kazi aliyokuwa akifanya huko Dodoma. Akabakia kwenda tu kazini ilimradi siku ziende. Kwa hiyo kama anavyosema mama yao, asante kwa kumtafutia Lea kazi.” “Ni amempa kazi ofisini kwake, baba.” Lara akamrekebisha. “Kumbe! Basi Mungu wangu akubariki.” “Amina baba, lakini nimempa masharti magumu huyo, na hana jinsi. Nimemwambia nilazima ayatimize yote lasivyo namfukuza kazi.” Jax akajua Lea ataonja joto vilivyo, Nelly hana utani.

          “Ameniambia. Nakuahidi atarudi tu shule. Atasoma.” “Lara alishanisindikiza chuoni. Nimeshachukua fomu na kulipia, nitakuwa nikisoma masomo ya jioni, na nimeshaanza kufanyia kazi kuzungumza kwangu. Namfanya Lara ndio mtu wangu wa kunisikiliza nikitoa ripoti yangu ofisini kila siku. Na Jax naye pia ananisaidia kwenye swala la kuzungumza na jinsi ya kusimama na kuangalia watu.” “Na lugha Lea.” Nelly akaweka msisitizo. “Anafanya na anajitahidi kwakweli. Ripoti zote anazokuwa akiandika, anaandika kwa lugha ya kingereza. Namsaidia kurekebisha jioni nikipitia hapa kuwaona, ndipo anajaribisha kuizungumza kama yupo mbele yako. Naona na hofu imeanza kupungua.” “Hapo sawa. Ilimradi kila muhula uwe unanipa matokeo yake ya chuo, nijue bado yupo chuoni. Aweze kujieleza vizuri, basi ajue ajira anayo. Lasivyo ajira itaota mbawa. Mimi siwezi kuwa karibu ya watu wasiojituma, wazazi wangu. Naona kama wananichelewesha.” “Lara alishatumbia.” Jax akacheka akitingisha kichwa. “Sasa unasikitishwa na nini na wewe Jax. Si bora niwaambie ukweli tu, na Lea aelewe. Sifanyi michezo ya kizembe. Lazima ajifunze kukimbia na timu yangu.” wao wakaondoka mpaka Jax, wakamuacha Lara na ndugu zake. Vilikuwa vimejaa vicheko hapo.

          “Ameniambia. Nakuahidi atarudi tu shule. Atasoma.” “Lara alishanisindikiza chuoni. Nimeshachukua fomu na kulipia, nitakuwa nikisoma masomo ya jioni, na nimeshaanza kufanyia kazi kuzungumza kwangu. Namfanya Lara ndio mtu wangu wa kunisikiliza nikitoa ripoti yangu ofisini kila siku. Na Jax naye pia ananisaidia kwenye swala la kuzungumza na jinsi ya kusimama na kuangalia watu.” “Na lugha Lea.” Nelly akaweka msisitizo. “Anafanya na anajitahidi kwakweli. Ripoti zote anazokuwa akiandika, anaandika kwa lugha ya kingereza. Namsaidia kurekebisha jioni nikipitia hapa kuwaona, ndipo anajaribisha kuizungumza kama yupo mbele yako. Naona na hofu imeanza kupungua.” “Hapo sawa. Ilimradi kila muhula uwe unanipa matokeo yake ya chuo, nijue bado yupo chuoni. Aweze kujieleza vizuri, basi ajue ajira anayo. Lasivyo ajira itaota mbawa. Mimi siwezi kuwa karibu ya watu wasiojituma, wazazi wangu. Naona kama wananichelewesha.” “Lara alishatumbia.” Jax akacheka akitingisha kichwa.

          “Sasa unasikitishwa na nini na wewe Jax? Si bora niwaambie ukweli tu, na Lea aelewe. Sifanyi michezo ya kizembe. Lazima ajifunze kukimbia na timu yangu.” “Nitajihidi au najitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu.” “Na wewe mwenyewe usiwe kipimo chako. Maana unaweza kudhani umefikia mwisho kwa kuangalia uwezo wako tu. Angalia kwa walioweza ndio ujiulize kwa nini wewe ushindwe! Kwa hiyo upambane, bila kujihurumia na kuubembeleza huo mwili. Weka malengo na ujiambie lazima yatimie. Kushindwa sio chaguo.” “Nimeelewa bosi wangu. Utapata matokeo mazuri.” “Hilo ndilo nilitaka kulisikia sio uniambie kwa kadiri ya uwezo wako.” Nelly akawa anataka kusimama, Jax akamuwahi kumshika mkono, akamsaidia kusimama. “Nakushukuru.” “Karibu. Ukapumzike sasa.” “Ndicho ninachoenda kufanya. Maadamu nishalisha haya matumbo matatu, hapa ni kitandani tu.” Akimaanisha tumbo la Billy, lake na mwanae. “Lea na Lara, tunashukuru kwa chakula kizuri.” “Karibu. Nimefurahi mmekuja kusalimia wazazi na kuungana nasi kwa chakula cha usiku.” Wakaondoka mpaka Jax, wakamuacha Lara na ndugu zake.

          Vikabaki vicheko tu hapo kwa Chiwanga na binti zake. Lucas naye alifurahi sana kumuona Jax. Lara akamtolea baba yake gauni. “Nilipata lile gauni la ndoto yangu, baba. Nelly wifi yangu alininunulia tulipokuwa nchini Uswiz.” Baba yake akacheka. “Bado mimi nilitunza ile suti yangu uliyoninunulia yakuvaa siku yako ya harusi.” Lara akacheka. “Hujaivaa mpaka leo!?” “Niliificha huku nikimkumbusha Mungu anijalie siku yako ifike na mimi niwepo, niivae. Hivi hapa bado ipo vilevile hapo ndani. Sijaigusa.” “Hakika tutapendeza sana, baba yangu. Tena tutembee taratibu ili nifurahie shela yangu.” Wakawa wakicheka.

Mungu akasaidia, harusi ya Jax na Lara ikafungwa kanisani kama Lara alivyokuwa akitamani tokea mtoto. Hakutoa hilo gauni la harusi na shela yake ndefu mpaka Jax alipomtoa usiku huo kuanza fungate. Ukawa usiku waliokuwa wakiutizamia kwa muda mrefu hata kabla Tula hajaingilia. Wakapita walikopijipitisha, wakapata mahodari wa mapenzi, lakini wakabaki wao wawili wakikumbukana mpaka usiku huo Jax anafanikiwa kumtoa Lara nguo ya mwisho mwilini mwake kama mkewe kihalali.



~~~~~~~~~MWISHO~~~~~~~~~

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment