Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Makosa! – Sehemu ya 17. - Naomi Simulizi

Makosa! – Sehemu ya 17.

Bado Sabrina hakuwa akiamini alichosikia kutoka kwa Jack. “Si umesema Tino ni kama aliua mtoto wake na aliondoka akiwa ameridhika kuwa hana alichobakisha tena kwako?” “Ndiyo Jack.” “Basi huyo mtoto ni wangu mimi.” “Jack!” “Kubali nikuoe Brina. Tumepoteza muda mwingi sana. Huoni kama mimi ndio mumeo wengine wameshindwa kujua thamani yako? Watakuchezea, na kuendelea kukuumiza tu. Mimi nakupenda na sijawahi kubadilika.” “Itakuaje kuhusu Pam?” “Yeye shida yake ilikuwa ni biashara tu. Ameomba nisimbadilikie kwenye biashara, nimwachie wateja niliomtafutia. Ameelewa, na hata Felex na Ney walimweleza.” “Juu ya nini tena!?” Sabrina akawa ameshachanganywa. Kina Felex na Ney tena! Akawa hajaelewa wanaingiaje hapo tena.

          “Unakumbuka Ibra, Felex na Ney walifanya kazi kwa karibu sana na mimi?” “Nakumbuka.” Sabrina akakubali. “Wanajua ni kiasi gani nakupenda Brina.” Sabrina akabaki amepigwa na butwaa. “Nakupenda Brina.” “Mwenzio nilijua nimechelewa Jack! Naona mpaka aibu!” “Sio kwangu. Labda kwa mwingine na labda uwe hunipendi kabisa Brina. Hapo nitashindwa chakufanya. Lakini kukiwa hata na upendo kidogo tu, naamini hutashindwa kuishi na mimi.” Sabrina hakuamini. “Unauhakika Jack!?”  Akauliza akiwa haamini. “Nakupenda Sabrina. Nakupenda kwa moyo wangu wote, sina sababu yakudanganya. Ningeshaoa, lakini kulikuwa kama na tumaini pengine ungekuja kubadili mawazo, ndio maana niliona nisiharakishe nikusubiri mpaka nione mwisho wake.” “Asante Jack.” Jack akakaa na yeye.

          “Kwa hiyo umekubali nikuoe?” “Ndiyo Jack. Nitafurahi kuwa mkeo. Nakuahidi nitakuwa muaminifu kwako.”  Jack akamvuta mkono akamvalisha ile pete kwa haraka sana. Sabrina akacheka machozi mpaka kidevuni. “Kubwa kidogo. Nitaipeleka wapunguze.” “Lakini acha nivae kidogo Jack.” Jack akacheka. “Umeipenda?” “Sana, na nimefurahi kupita kiasi Jack, siamini!” Jack akajisogeza karibu, akambusu kwa mara ya kwanza mdomoni. Kidogo tu, kisha akamwangalia. Akambusu tena. Akaongeza tena, kisha akaongeza tena na tena ikawa mfululizo, Sabrina akamkumbatia kwa upendo, ndipo Jack akaanza kunyonya midomo ya Sabrina kwa uchu kama fisi aliyeona nyama.

          “Jack!” Sabrina akajivuta pembeni kidogo. “Ulisema utanioa?” “Si umesema ‘ndiyo’?” Na yeye Jack akauliza. “Lini? Baada au kabla ya kujifungua?” Jack akajivuta nyuma na kujiegemeza kwenye mto. “Wewe ulitaka iwe lini?”  Jack akauliza kama anayefikiria. “Vile unavyotaka wewe Jack.” Sabrina akajibu kama anayebembeleza. “Kwa hiyo hata nikitaka iwe kabla yakujifungua pia ni sawa?” “Ningefurahi Jack.  Ningefurahi sana. Sema nafikiria maandalizi. Nimebakisha kama miezi mitano na siku chache tu ili nijifungue.” “Mbona tumbo lenyewe halipo!” Sabrina akacheka. “Naomba kuona.” “Kabisa!?” Sabrina akauliza kwa kushangaa kidogo na cheko la aibu usoni. “Unamaanisha nini ukiuliza ‘Kabisa’?” “Sijui! Labda unataka kuona hapa kwenye nguo.” “Kwenye nguo ndio sioni. Ndio maana nataka kuona tumbo lenyewe.” Sabrina akajishauri.

          “Tokea nioge asubuhi, halafu nimekuwa na siku ndefu! Tumetembea sana juani na Emma. Labda nikaoge kwanza. Utanisubiri?” “Hapa au chumba kile kingine?” Sabrina akacheka taratibu. “Hapa. Si ni sawa?” “Sawa.” Sabrina akatoka kitandani, akachukua taulo na khanga. “Njoo kidogo.” Sabrina akarudi pale kitandani na kukaa. Jack akamsogelea na kuanza mabusu tena. Akambusu mpaka Sabrina akasalimu amri. Akajiachia hapo mikononi kwa Jack, asikumbuke kuoga tena. Alichofanya Jack ni kuendelea kunyonya hiyo midomo huku akipitisha mikono chini ya gauni mpaka akafika tumboni. Akaanza kumpapasa tumbo huku akiendelea kunyonya midomo yake.

Mvumilivu, Kala Mbivu.

S

abrina akahisi vidole vikipenya ndani, pembezoni mwa chupi. “Nikaoge kwanza Jack, nanuka jasho!” Sabrina akanong’ona taratibu. “Siwezi kusubiri tena.” Jack akajibu huku akimnyonya shingoni na kumbusu. “Nimekuwa na vipingamizi vingi sana juu yako Brina. Nimesubiri sana, jasho haliwezi kunifanya nikasubiri tena zaidi, tafadhali Brina.” Sabrina akajipandisha kitandani vizuri. Kwa haraka Jack akamuweka sawa. Alimbusu kila mahali kama anayebusu alumasi wakati alikuwa akitembea juani siku hiyo nzima. Kwa hakika alijua ananuka. Lakini Jack hakujali. Akaendeleza mabusu ya haja, Sabrina akayasikia katika kila mfupa wa mwili wake. Harufu ya Jack ikamwingia mpaka kwenye fahamu zake, akasikia kutulia kwa ajabu, akamvutia Jack mwilini kwake, yakaanza mapenzi.

          Wawili hao walifahamiana kwa miaka, lakini siku hiyo wakavuka mipaka. Sabrina alimsikia vile Jack anavyomfurahia, ujasiri ukaongezeka. Akajawa nguvu ya ajabu, uchovu ukamwisha. Penzi lililofanywa hapo, kila mmoja alifurahia, wakajitupa kitandani hoi. “Sasa nenda ukaoge, nije nimuone mwanangu.” Sabrina akacheka kwa furaha. Akavuta khanga yake kutoka sakafuni, akajifunga na kuelekea bafuni, akamuacha Jack amejilaza kitandani.

          Sabrina anatoka kuoga, akamkuta Jack amelala, kama aliyetoka kulima siku nzima. Akajua hakuna kuoga tena. Akamsafisha na kumfunika, Jack akiwa hana hata habari. Furaha iliyokuwa imemjaa Sabrina, alitamani apate wakumwambia kuwa amechumbiwa na Jack. Akajipaka mafuta. Akavaa tisheti ya Jack akakaa kitandani akijiangalia kidoleni na ile pete, asiamini Jack amekusudia kumuoa na ule ujauzito! Alijawa furaha, hofu ikaanza kupungua. Akamvuta mkono pale alipokuwa amelala, akaubusu mara kadhaa. “Asante Jack.” Akanong’ona taratibu. Aibu yakuzunguka mtaani na tumbo ambalo muhusika hakutaka kuzaa naye, akimtaka atoe huyo mtoto, ikaanza kupungua. “Sijui atanioa lini huyu!?” Akajiuliza akitamani iwe kabla hajajifungua. Akajilaza pembeni ya Jack, ukutani. Akaanza kumnusa mpaka na yeye akapitiwa na usingizi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alam ya kumuamsha Jack kwenda kazini ndio iliyowatoa wote usingizini. Jack akavuta boxer yake pembeni na kuivaa maana aliamka mtupu, Sabrina alimfunika tu usiku uliopita, baada ya kumsafisha.  “Ngoja nikakuandalie kifungua kinywa, wakati unajiandaa kwenda kazini.” Sabrina akataka kutoka kitandani. Akamvuta. “Unisamehe jana nilipitiwa na usingizi. Nilikuwa nimechoka! Zaidi mawazo. Sikulala vizuri tokea nimeondoka hapa. Wakati wote nilikuwa nikiamka kutoka usingizini najaribu kukupigia, na kusubiria simu yako.” “Jamani Jack! Pole. Mwenzio nilijua unafurahia na wenzio! Sikuwa hata na wazo kama utakuwa ukinikumbuka huku!” Jack akamwangalia kama anayemuuliza ningewezaje! “Kweli Jack. Nilijua utakuwa busy na marafiki zako, nikaogopa hata kukosea kupiga, marafiki zako wasijefikiri nakusumbua.” “Basi heri ungenipigia nikaacha kupokea, kuliko kuacha kunitumia hata ujumbe kutaka kujua ninaendeleje Brina!” “Naomba unisamehe Jack. Nisamehe bure.” Sabrina akakaa vizuri.

“Nimekuwa na watu ambao hawajali mawasiliano na mimi Jack. Historia ya nyumbani ni kama nilivyokusimulia. Tokea naondoka nyumbani nilipokwambia nakwenda kupumzika kwa dada Sabina, huwezi amini Jack, mpaka nahamia Moshi, muda wote hata wazazi wangu hawakunipigia simu kutaka kujua ninaendeleaje, wakati nawaona wanavyofanya tofauti kwa kina Sabina na kaka! Hazipiti siku mbili, lazima wao wenyewe wawapigie kuwajulia hali lakini sio mimi! Haya, nikawa na Emma, yeye ndio ilikuwa wakati mwingine ukimpigia anagomba kabisa ni mpaka akupigie yeye mwenyewe.” “Haiwezekani Brina!” “Kweli Jack. Mpaka nilikuwa naona aibu kuwaambia watu hivyo. Tena anakuwa mkali kabisa, anasema mpaka akupigie yeye. Kwa hiyo swala la mawasiliano halipo kwangu. Na ni kama nimeingiwa hofu, naona kupiga ni kama kumsumbua mtu!” Jack akaumia kwa kiasi fulani.

“Sio kwangu Brina. Naweza nisipokee kama nipo kwenye simu nyingine, au katikati ya mazungumzo na mtu. Lakini lazima nitarudisha, au hapo hapo nitapokea na kukwambia nitakupigia. Mimi napenda mawasiliano sana. Hata kina Ibra wanajua hilo. Na Tino naye?” Sabrina akacheka kwa kuguna. “Sasa yeye alipitiliza. Alikuwa akinifuata mpaka chooni kama nitachelewa. Na hakuna nilipokuwa nikienda bila yeye. Na hapo nafikiri ndipo nilipojichanganya Jack. Nikafikiri ni mapenzi ya dhati, kumbe ni kwa kuwa alikuwa akinitegemea, aliogopa ningeweza kumkimbia kabla hajapona kabisa na kuweza kujitegemea mwenyewe.”

“Mambo yalianza kubadilika tulipokuwa Moshi, tena alipoanza kujitegemea. Akawa ananionyesha kama si lazima tena. Wakati mwingine alipokuwa yupo gym anafanya mazoezi pale kwenye Villa, ilikuwa nikimfuata, ananiambia yeye yupo tu sawa, nirudi kwenye apartment yetu. Yaani kama anayeniambia nisimfuatefuate. Nikaanza kuumia, kwa kuwa haikuwa hivyo mwanzo. Alishanizoesha kuwa naye kila mahali. Kwa hiyo naomba nielewe Jack, na hofu pia inachangia.” “Basi sio mimi. Mimi nataka unisumbue.” Sabrina akacheka na kuinama.

“Naomba kumuona mtoto.” Sabrina akashangaa kumbe bado anakumbuka. Alishajiambia ile ya jana kutaka kuona tumbo, ilikuwa janja yakumvua chupi, kumbe nia alikuwa nayo! Sabrina akajilaza chali. Jack akampandisha ile tisheti mpaka juu kabisa. Akaanza kumshika tumbo. “Kweli ukiangalia hivi kwa karibu utagundua. Limetuna hapa chini na gumu kabisa!” Jack akaendelea kuongea huku akimshika kuzunguka tumbo. “Inauma nikifanya hivi?” “Hapana bwana. Hivyo unanibembeleza.” Wakacheka. “Anacheza?” Akauliza tena Jack. “Bado mdogo. Sijamsikia hata mara moja.” Akambusu mara kadhaa, akamsikia midomo inazidi kupanda juu. Sabrina akacheka.

Kilichoendelea Huko Dar.

“Unanitekenya bwana!” “Nataka tufunge ndoa Brina wangu. Au unasemaje?” Akawa anamchungulia kule Sabrina alipokuwa amejilaza, yeye tumboni kwake. “Njoo kwanza hapa nikuhoji vizuri. Mbona imekuwa gafla wakati uliondoka hapa na Pam vizuri?” “Kama uligundua, Ibra alilazimishia sana ile safari. Kumbe lilikuwa wazo la Pam na yeye alikuwa na yake, nitakuja kukwambia wakati mwingine, leo tubakiwe na furaha tu.” Sabrina hakuwa ameelewa. Jack akamuelezea alivyoambia na Ibra, Pam alipompigia simu na kumuomba awaalike. Sabrina akashangaa sana.

“Sasa ikawa ni kama ikatokea bahati. Yule mwanamziki akawa anafika Dar, na ombi la Pam. Ndipo Ibra akaona amtumie huyo mwanamziki kama kigezo. Wakati tupo njiani kuelekea Dar, nilimpigia simu kaka kumsalimia.” “Waziri Msindai!?” Jack akacheka jinsi Sabrina alivyoshangaa. “Nina kaka mmoja tu Brina. Huyo huyo.” Wakacheka. “Basi, nikamwambia nitakuwa Dar, nakwenda kwa huyo mwanamziki, nitakuwa na kina Ibra. Akasema na wao watakwenda kwenye tamasha na mkewe, la huyohuyo mwanamziki, wana VIP tiketi. Nikamwambia kama anaweza kutufanyia mpango na sisi tukapata tiketi angalau viti karibu na vya mbele kama VIP tutakosa. Akasema ataulizia, kisha atatujulisha.”

“Sasa siku ile ya ijumaa nakupigia simu kukutaarifu kuwa tumefika salama, tunajiandaa kwenda kula, kaka naye akapiga kutuambia amepata tiketi nne tu za VIP, akaniambia kama nataka anipitishie hotelini au kesho anipe tukikutana nyumbani. Maana tulikuwa na miahadi wote tukutane kwa wazazi siku ya jumamosi asubuhi. Sasa mimi namjua kaka, moyo wake wakugawagawa, nikajua anaweza kukutana na mtu, akampa zile tiketi. Nikamwambia anipitishie tu pale hotelini ijumaa ile ile. Akakubali.”

“Sasa alipofika pale si ndio akamkuta Pam. Akaanza kucheka sana. Maana anamjua Phina.” “Yule mpenzi wako wa chuo?” Jack akacheka. “Huyo huyo, nilimuomba amsaidie kumuunganisha na marafiki zake wampe kazi Dar. Maana Phina alisema hataki kutoka nje ya Dar. Sasa kaka akaanza kunitania kuwa, nimeamua ku upgrade. Kutoka kwa Phina, nikamtafuta mrembo Pam. Hatujakaa sawa, May msichana wa Ibra, Ibra mwenyewe, Ney na Felix wakaja. Kaka akawatania na wao wakawa wanacheka tu. Ndio akawaambia kwa nini wanataka kwenda kula mbali wakati kwenye ile hoteli napo panauzwa chakula! Ney akamwambia tunakimbia bei. Basi kaka akasema tukae tule, yeye atalipa kwa furaha ya kuletewa shemeji.” Sabrina akamuona anacheka kwa kusikitika.

“Nilishindwa kuvumilia Sabrina, palepale mbele ya kila mtu, nikajikuta nimeropoka. Mpaka baadaye nilimuomba Pam msamaha.” “Uliropoka nini!?” Sabrina akauliza akiwa hajaelewa. “Nilisema Pam sio mke wangu, ni rafiki tu wa starehe, mke wangu ananisubiri nyumbani.” “Jack!” “Kweli tena. Sasa kaka akashangaa. Akaniuliza uhuni nimeanza lini? Kuwa na wanawake wawili! Hapo nikawa nimejichanganya sasa. Kila mtu ananitizama kuona natoa maelezo gani. Kaka akawa mkali haswa, akaniambi wazazi wananiamini sana. Na popote nilipo nawakilisha familia nzima, ya Msindai. Kwa nini naishi maisha kama mnyama? Ndipo nikamuomba tuzungumze sasa. Ukumbuke hapo nishatibua hali ya hewa, kila mmoja amebaki akiniangalia mimi.”

“Nikawaambia Sabrina yupo nyumbani kwangu. Nikawaambia umekubali kuhamia Singida kwa ajili yangu. Nikawaeleza kuwa nilikufuata Moshi, sasa hivi tunaishi wote. Nikamwambia kaka, nimekuwa nikikusubiri tokea chuo. Ndio Ney na na Felix wakanisaidia kumueleza kuwa tokea nipo na Phina, wewe ulikuwepo kwenye moyo wangu hata Phina anajua hilo.” Sabrina akashangaa sana. Lakini pia akajiuliza kwa nini katika huo utetezi, Ibra kama rafiki wa karibu wa Jack yeye asimtetee kwa kaka yake! Lakini akaona anyamaze aendelee kusikiliza kilichoendelea huko jijini.

“Hao wawili wakamwambia kaka mengi wakimuaminisha, tena yatokea chuoni. Ndipo kaka akauliza sasa kwa nini awepo Phina na huyo Pam kama wewe ulikuwepo tokea zamani? Au tamaa! Kaka akidhani nitamaa. Ndio mimi mwenyewe nikamwambia nilikupenda ukiwa kwenye mahusiano. Kwa hiyo ulinikataa. Na sasa unaishi kwangu sio kama mpenzi, lakini kama rafiki. Ndio kaka sasa akasema lazima nikwambia tena. Na safari hii lazima niende umbali mrefu zaidi nikuonyeshe nia ya kuwa na wewe kwenye maisha, nifunge hilo jambo sio nionekane mahotelini na msichana huyu, kesho naonekana nimeoa mwingine. Akasema sio sawa kwangu na kwa Pam pia. Akanikumbusha ndoto nilizonazo, ninapokwenda na nilipo. Akaniambia kosa nitakalofanya sasa hivi nikiwa sijulikani, watu hawatajali. Lakini siku nitakapokuwa kiongozi mkubwa, yote hayo yatanifuata, na yatakuwa mwiba mbaya sana.”

“Huwezi amini Sabrina, akahakikisha naondoka pale hotelini, narudi kulala nyumbani kwake baada yakupata muda wa pembeni kuzungumza na Pam.” “Jack!” Sabrina akashangaa. “Kweli sikudanganyi. Wewe ushasikia skendo yake yule hata moja?” “Hata mara moja!” Sabrina akaungana naye. “Basi yule yupo kama mtumzima, mama anasema tokea mdogo alikuwa hivyohivyo. Na huo usemi wake wa popote nilipo nawakilisha familia nzima, ni wosia wake ambao haachi kunikumbusha. Aliniambia nimuage Pam vizuri na kwa amani, niondoke naye.” “Sasa Pam hakulia?” Sabrina akauliza, Jack akacheka.

“Pam!” Akawa kama anamfikiria. “Yaani palepale akasema hata yeye alijua sitamuoa. Sisi hatuendani kabisa.” Wote wakacheka. “Hata pale walicheka. Akasema yeye anazijua akili zake, haziendani na zangu kabisa. Akatuchekesha hapo, lakini akaomba tusimfukuze pale, akasema yeye Dar hapajui. Kaka akamwambia hatuwezi kumuacha hapo, atalala, na kesho kwenye tamasha tutaenda kumchukua. Akaniuliza kama anaruhusiwa kunywa, nikamwambia lakini asizidishe.” Sabrina akacheka sana. “Yaani Pam!” “Anapokwambia hapendi kumuudhi mtu, basi ndio akili yake ilivyo. Wakati naondoka na kaka nikamuomba Ibra wasimuache pale peke yake. Maana wote wanamjua Pam akilewa. Nikawaomba wakiwa wanaondoka, wahakikishe wanamfungia kabisa chumbani.” “Jack! Kwa nini?” “Wewe si utakaa hapa Singida, utasikia habari za Pam. Akilewa huwa akili haifanyi kazi kabisa. Anaweza hata kuvua nguo mbele za watu.” Sabrina akashika mdomo.

“Sikutanii. Hivi unafikiri kwa nini namkataza kunywa pombe hovyo? Ni kwa ajili hiyo. Na anapenda bia, kuliko nitakavyokwambia! Ukitaka mpatane, mpe bia. Na mbaya, huwa hakumbuki anayofanya akiwa amelewa, pombe ikiisha utamuonea huruma. Ila niliupenda moyo wake. Basi, kesho yake siku ya jumamosi kaka ndio akanisindikiza kununua hiyo pete akaniambia nije nizungumze na wewe, ukikubali, ndipo niwaambie wazazi. Basi, tukahangaika kweli kutafuta pete nzuri. Usiione hivyo hiyo, ni garama haswa. Hivi hapa ananidai, amesema nitamlipa taratibu. Lakini nimemwambia mwishoni mwa hii week nitamtumia pesa yake. Sasa kwa heshima yake ndio wakakubali hata kupunguza ukubwa, ilikuwa kubwa zaidi ya hapo.” Akamuona Sabrina amepotelea mawazoni.

“Nini tena?” “Anajua kama mimi nina mimba isiyo yako?” Sabrina akauliza kwa unyonge. “Ilibidi kumwambia Sabrina. Nikasema asije kuhangaika vyote hivyo, halafu akaja kujua baadaye, akanilaumu.” “Sasa akasemaje?” Jack akacheka kidogo kama anayefikiria. “Yule mtu amejaliwa hekima Sabrina, mimi mpaka nikashangaa. Yeye aliniambia hivi, ‘chakuokota, si chakuiba. Mwenye mali, ndio mjinga’.” Sabrina akashangaa mpaka akakaa. “Jack!” “Kweli tena. Akasema mtoto yeyote anayezaliwa ndani ya ndoa, ni wawanandoa. Mengine anajua mama. Akanichekesha kile kipindi cha mambo ya DNA, akasema ambao hawakufikiria walikimbilia kupima watoto waliokuwepo nao ndani ya ndoa wakilea kama wao, wakavunja ndoa zao, wakakosa na warithi. Wenye hekima, wakanyamaza na watoto wao. Akaniuliza, mimi najuaje kama nina kizazi? Nikanyamaza. Akaniambia hata kama Mungu atanijalia watoto wangu mwenyewe, akaniambia naweza kuja kukuta huyu mtoto ndiye akanifaa kuliko mtoto wangu mwenyewe. Akaniambia baba hakatai mtoto.” Mpaka Sabrina akajisikia machozi yakimtoka.

“Alinitia moyo, mpaka nikajisikia vizuri. Akasema ni baraka wala nisiogope. Mungu atanipa hekima juu ya hili, ilimradi tu niwe nakupenda kwa dhati. Mengine nisiogope. Nilijisikia furaha sana Brina. Maana alinipongeza na akaniambia kweli wewe utakuwa mwanamke ninayekupenda, vinginevyo nisingekuchukua na hali hiyo. Basi, jumapili tukampitia Pam hotelini, akaturudisha uwanja wa ndege.” Sabrina akabaki ameinamia magoti. “Kwa hiyo harusi si ipo, mama?” “Ipo Jack. Wala sijivungi. Mungu anipe nini tena? Hata kesho wewe nioe tu. Sitakuja kupata mtu anayenipenda hivi. Nioe tu Jack. Mimi nitataka harusi tu. Tena ndogo, wala si kubwa yakutumia mamilioni ya pesa wakati tuna shida na pesa. Na sitaki mambo ya sendoff wala kichen party.”  Jack akambusu.

“Naomba nikumbatie kabisa, ili niamini kama kweli nipo mikononi mwako, wewe Jackson.” Jack akacheka. “Hujui ni kiasi gani najisikia salama na wewe Jack.” “Nakupenda Brina. Nakupenda sana. Njoo.” Sabrina akaona atajipunja. Akasimama kwa haraka, akatoa nguo zote Jack akimwangalia kisha akaenda kumkalia Jack akiwa na yeye hana nguo ya juu ila boxer aliyoivaa asubuhi hiyo alipoamka. “Nikumbatie kabisa, nipate mwili wako mwilini mwangu.” Jack akacheka asiamini. “Napenda matiti yako Brina! Unakifua kizuri sana!” “Nikumbatie kwanza nitulie, nitakupa yote. Nitakunyonyesha huku nikikufurahisha. Ila nataka unikumbatie kwanza.” Jack aliposikia hivyo, akatoa nguo ya chini kwa haraka, akajirudisha kitandani na kumpokea Sabrina kwa mikono yote miwili.

Sabrina anamkalia miguu akaikutanisha nyuma ya mgongo wa Jack. Jackson alishakuwa amesimamisha. Akaona hatakaa vizuri. Yeye mwenyewe Sabrina akamlainisha kwanza Jack kwa midomo yake, alipoona akijiingizia hataumia, ndipo akarudi kumkalia vizuri akiwa anajipenyezesha taratibu. Jack akataka kuanza. “Tulia bwana Jack unikumbatie kwanza.” “Hata nisisogee kidogo!” “Hapana bwana. Mimi nimekuweka sawa ili niweze kukaa vizuri.” “Nitakukumbatia baadaye. Hivyo unavyonibana huko, siwezi nikakaa tu nikatulia.” “Ningejua nisinge…” “Wewe mwenyewe umeninyonya sana halafu unanibana! Malizia vyote ulivyoniahidi kwanza. Niwekee hilo ziwa moja mdomoni, niruhusu nikushike ninakotaka, nitulize kwanza ndio nitaweza kukumbatia vizuri. Sasa hivi ushanichanganya.” Sabrina akaanza kucheka taratibu na kurudi shingoni kwake, akaanza kunyonya shingo yake. Alipofika masikioni na kuweka ulimi hapo, uzalendo ukamshinda Jack akaanza kuhangaika hajui ashike wapi. Sabrina akajirudisha nyuma taratibu, akamuwekea titi mdomoni huku akimsaidia na yeye kwa kujinyanyua juu na chini akikata kiuno.

Jack akasahau kama mwenzie ni mjamzito, akaanza kuvuta matiti kama mtoto mwenye njaa, Sabrina akatulia tu akijua hakuna jinsi atamwambia apunguze kunyonya anamuumiza, akaelewa kwa wakati huo. Lakini kwa kuwa alishamgundua hajiwezi akishikwa masikioni, akaona amfupishie safari. Akamuwekea vidole masikioni akimchezea, Jack akasalimu amri bila kuchelewa. “Usingenishika tena masikioni bwana Brina! Umenikatisha!” Jack akalalamika, Sabrina akamcheka. “Ulikuwa ukiniumiza matiti. Unatumia nguvu nyingi kuyanyonya, mwenzio naumia. Yameanza kujaa.” “Samahani nimeshindwa kuwa mstaarabu, sitarudi...” “Hapana bwana hata mimi napenda. Wewe furahia ila taratibu.” Wakacheka. Sabrina akataka kuondoka, Jack akamuwahi kwa kumvutia chini asinyanyuke. “Usiondoke bwana. Niache nitulie nikiwa hukohuko ndani. Unajinsi yako unanibana, nasikia raha.” Sabrina akajiweka sawa akicheka. Jack akaweka mto nyuma yake vizuri, akamkumbatia akiwa ameegemeza mgongo ukutani, Sabrina amemlalia begani, akimnusa shingoni.  Wakatulia kwa muda. Jack akakumbuka kaka yake anasubiria jibu.

Jack kwa kaka yake.

J

ack akachukua simu yake hapohapo na kumpigia  kaka yake. “Amesema ‘ndiyo’.” Sabrina akamsikia anaongea bila hata salamu. “Nilijua umekataliwa dogo. Kimya cha jana siku nzima!” Akawasikia wote wanacheka. “Sikumkuta nyumbani. Alikwenda kanisani na huyu dogo ninayeishi naye hapa, nilikwenda kuwafuata usiku.” “Hongera sana. Sasa harusi lini?”  Kaka yake akampongeza na kumuuliza. “Sijui kama itawezekana kaka. Nilitamani tufunge ndoa kabla hajajifungua. Amebakisha miezi mitano tu!” Kimya. “Unafikiri haitawezekana?” Jack akauliza kwa wasiwasi.

“Hakuna kitakachoshindika ikiwepo pesa. Kwani mnataka harusi ya namna gani?” Kaka yake akamuuliza. “Tunataka harusi ndogo sana. Ndugu tu na marafiki wa karibu. Brina hataki hata sendoff. Harusi tu. Kwa hiyo ni swala la mahari, na hiyo harusi.” “Basi wapigie wazazi simu. Wakusikie wewe mwenyewe kuwa unataka kuoa, kisha mimi nitamfuata baba na mama, tupange. Halafu tutakwambia.” Jack akafurahi sana na kumshukuru sana kaka yake. “Pongezi bwana. Angalau unaongeza kitu kwenye maisha, sio unabaki unazagaa mtaani huna familia!” Wakataniana kidogo, wakaagana, Jack akiwa na tumaini.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~

“Huyu akishika jambo lako, ujue atakamilisha tu. Sasa kazi kwako Brina. Usiniangushe tena.” “Mimi nipo hapa na wewe Jack.” Jack akacheka. “Namaanisha kwenu. Sisi kwetu naona ishakuwa mteremko.” “Mbona utanioa tu Jack! Wapende wasipende, mimi naolewa na wewe.” “Kweli Brina? Wakiweka kipingamizi?” “Acha kunitania Jack! Kwani wao wanajua sasa hivi nilipo au hata ninachokifanya? Wanikatalie kwa sababu ipi? Hakika sitajali vipingamizi vyao. Utanioa tu, wala kwa hilo lisikutie shaka labda wewe mwenyewe ubadili mawazo.” Jack akaanza tena kumpapasa.

“We Jack! Utachelewa kazini bwana!” “Hakika leo siendi. Watanisamehe tu. Nilivyokuwa na hamu na wewe!” Sabrina akacheka sana akifurahia. “Kwa hiyo tunabaki wote?” “Siku nzima mimi na wewe tu.” Sabrina akasikika akizidi kucheka kwa furaha wazi alisikika na kicheko cha kutoka moyoni. Wakatoka kwenda kuoga. Wakapata penzi jingine tena na tena wakilipiziana kuwa nimekufanikishia safari ile, mimi sijapata kitu, wakicheka na kurudia bila kuchoka kwa uhuru wote wakijua Emma hayupo, nyumba nzima wako peke yao, hakuna wakuwaingilia.

Sabrina Kwa Familia Yake.

I

lipofika mchana, Sabrina akaamua kumtafuta kwanza Sabina. Alikuwa amejilaza miguuuni kwa Jack, akimchezea maziwa. “Wewe mtoto umepotelea wapi? Maana ulikuwa ukitafutwa na Lela karibu kuchanganyikiwa.” “Sitaki kusikia habari za kina Lela kabisa. Nishamalizana nao hao. Ila kwa sasa nipo Singida na sitaki uwaambie. Sitaki kufuatwa nyuma. Nilichokupigia ni kukutaarifu kuwa naolewa.” Kimya kama aliyepatwa na mshituko. “Unanisikiliza?” Sabrina akauliza. “Nipo, nawafikiria wazazi wako watakachosema. Habari wanayotaka kusikia kutoka kwako ni shule. Angalau ungerudi na habari ya kusema ulipata kazi, ukarudi shule, hapo mtaelewana. Wewe una diploma hata maisha yako hayaeleweki unakimbilia ndoa! Una...” “Samahani Sabina. Samahani sana dada yangu.” Sabrina akamkatisha kwa hasira na kukaa kabisa, mkono wa Jack ukatolewa kwenye ziwa alilokuwa akichezea.

“Wewe unajua sasa hivi nipo wapi na ninafanya nini? Unajua naolewa na nani? Unajua nipo kwenye hali gani?” “Si wewe mwenyewe umejificha!” “Hata wakati nipo hapo Dar na nyumbani, ulikuwa ukinitafuta mimi kama mdogo wako kunisaidia au hata kunijulia hali wakati ulijua nipo kwenye shida?” “Sasa ulitaka nifanye nini?” Sabina akauliza kwa ukali. “Sasa kama hujui chakufanya kwenye maisha yangu, nisikilize mimi ninayejua chakufanya. Wewe umesoma, ndio mtoto mzuri hapo nyumbani ridhika hivyo. Nimekupigia kwa heshima tu nikijua wewe ni dada yangu nikidhani utafurahia pamoja na mimi! Lakini..” “Wewe Sabrina, mimi nakwambia wazazi wako watakachosema.” “Sijali.” Sabrina akajibu kwa ukali Jack akimsikiliza.

“Hapa sijapiga simu kuomba ushauri. Naomba hata na wewe uelewe. Na ukiweza naomba umwambie na baba na mama, angalau kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu, wanyamaze wasiniambie vile wanavyojisikia juu yangu. Washaongea sana na kunitukana kwa kurudia rudia. Waambie sijasahau, nakumbuka. Ninachotaka nikuwapa heshima kama wazazi. Wakwe wanataka kuja kutoa mahari. Kama wapo tayari kupokea mahari yangu mimi kama mtoto wao, nitashukuru. Wakikataa, basi. Waambie lakini mimi naolewa baada ya miezi miwili kuanzia sasa.” Sabina kimya.

“Sijui kama unanisikiliza?” “Nakusikiliza Sabrina. Lakini mimi sio kwamba sijakufurahia.” “Basi kama umenifurahia, naomba usimame na mimi katika hili. Angalau mara moja tu kwenye maisha yangu. Hili ni muhimu sana kwangu. Linaweza lisilete maana kwenu, lakini kwangu linamaana sana. Sasa kwa nini nimekupigia wewe kwanza simu?” “Umekuwa mkali Sabrina!” “Nimechoka dada. Nimechoka kudharauliwa na kunyanyaswa kwa maneno machungu. Inakuwa kila mtu anajua ni nini nahitajika kufanya! Nini natakiwa kufikiri na ni nini natakiwa kujisikia isipokuwa mimi mwenyewe! Nahisi ninahaki na mimi yakupendwa na kuthaminiwa kama wanadamu wengine. Sasa nimepata mtu wangu, mnataka tena kuniwekea vikwazo! Hapana jamani.” Sabrina akawa mkali haswa.

“Ulitaka mimi nifanye nini?” Akamsikia Sabina ametulia. “Kwa kuwa wewe huwa wanakuheshimu sana. Wanakupenda na lolote ukizungumza huwa wanakuelewa, naomba nisaidie kuwafikishia huu ujumbe kwanza kuwa naolewa. Ili mimi mwenyewe baadaye nitakapowapigia simu kuwataarifu waweze kuelewa nini nazungumzia. Maana kwao mimi nakuwa kama nazungumza nao kichina, huwa hawanielewagi. Kwanza hawajawahi kuwa tayari kunisikiliza, wakati wote wanataka niwe nawasikiliza tu wao. Ndio maana nimekupigia wewe simu, uwaambie ambacho ningeweza kuwaambia mwenyewe, lakini najua kwa hakika hawataelewa kwa kuwa huwa hawanielewagi.” Sabrina akaendelea.

“Kwa hiyo da Sabina, naomba ujue hili na uwataarifu kuwa, NAOLEWA.” “Nimeelewa Sabrina! Na mimi nitampigia baba simu kumwambia, nimsikie.” “Sawa. Lakini waambie nitasikitika kuwakosa kwenye harusi yangu kama watakataa, lakini mimi naolewa.” Akamsikia Sabina anacheka. “Sasa unacheka nini?” “Ungeanza ukali huo tokea zamani, wangekuheshimu.” Ikabidi Sabrina acheke tu.

Wakataniana kidogo. “Sasa hii ndio namba yangu mpya, ukitaka kuwasiliana na mimi juu ya hili, unaweza kunipigia.” “Sasa mbona hata shemeji mwenyewe hujaniambia jina?” Sabrina akaanza kucheka. “Unataka kumsalimia?” “Kumbe yupo hapo!?” “Ndiyo! Kwani vipi?” “Mama wewe umekuwa mkali! Mimi nimeuliza tu! Naomba nimsalimie shemeji.” Sabrina akamgeukia Jack aliyekuwa akimpapasa taratibu mgongoni baada ya mkono kutoka ziwani. “Sabina anataka kukusalimia.” “Hamna shida.” Jack akapokea simu.

“Halow!”  Akaanza Jack. “Halow, naitwa Sabina. Dada yake Sabrina. Sijui kama amekutambulisha kama kuna dada au imekuwa harakahara hata hufahamu ndugu!” Jack akacheka kidogo, akielewa anachomaanisha. Hao ndugu aliwafahamu kwa kuwasikia kwa muda mrefu sana. “Nakufahamu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa, sema hatukubahatika kukutana tu, lakini nawafahamu ndugu wote wa Sabrina. Kuanzia wewe Sabina dada mkubwa, Seba ambaye yupo katikati yako na Sabrina, halafu wadogo zenu wa mwisho wa kiume. Sethi na Simon.” Sabina akashangaa sana. “Haiwezekani! Kumbe mnafahamiana kwa muda mrefu hivyo! Ndio unaitwa nani!?” Sabina akaonekana kushangaa sana. “Jackson.” “Hamna jina la pili?” Jack akacheka kidogo. “Jackson Msindai.” Pakazuka ukimya. Jack naye akanyamaza akijua ameshituka kusikia Msindai.

“Unamaanisha Msindai! Msindai!  Msindai waziri!?” “Hapana. Mimi ni Msindai Jackson.” Jack akajibu akicheka taratibu kiungwana. “Nimeelewa. Lakini Namaanisha kwani hamfahamiani na waziri Msindai?” “Yeye ni kaka mkubwa, mimi ndio wa mwisho kwenye familia.” “Acha masihara! Kwahiyo Sabrina anaolewa na Msindai au sijaelewa vizuri?” “Mimi Jackson ndiye namuoa Sabrina.” Sabina akaanza kucheka, wazi alisikika kubabaika.

“Ndio maana mnajeuri yakufanya harusi ya haraka! Mama yako si ndio alikuwa waziri wa afya awamu ya Mkapa?” Jackson akacheka kiuungwana tu na kukubali. “Ndiyo. Nikurudishe kwa Sabrina?” “Subiri nishangae kidogo bwana! Kwani mnaharaka ya kwenda wapi jamani! Mimi nataka kukufahamu zaidi. Au kuna tatizo?” “Hamna shida. Karibu.” Jack akakubali. “Kwa hiyo mmefahamiana na Sabrina kwa miaka mingapi?” “Mitano sasa. Hatujakukurupuka tu. Namuoa mtu ninayemfahamu vizuri sana.” Jack akajibu kwa uhakika mpaka Sabrina akamgeukia.

“Kwa hiyo muda wote huo mlikuwa kwenye mahusiano na Sabrina?” “Nililo nauhakika nalo, ni mapenzi yangu kwake kwa muda wote huo. Maana tulipokuwa chuoni nilimuomba mahusiano, akanikataa. Lakini bado nilikuwa na matumaini. Aliondoka na kuniacha chuoni, lakini tukaendela na mawasiliano. Kwa hiyo nimekuwa nikimsubiri anikubali ili tu nimuoe yeye Sabrina. Kwa kuwa kwa hakika nilijua moyoni, Sabrina ndiye mke wangu. Ukiniuliza kivipi, mimi mwenyewe sikuwa nikijua, lakini kwa miaka yote nilikuwa nikisubiri mke wangu, ambaye ni Sabrina.  Kwa hiyo kwa mara nyingine tena, jana ndipo nimemuomba aje awe mke wangu, kwa mara ya kwanza amekubali na ndio maana sitaki tena kusubiri. Nataka nimalize kabisa, nijue natulia, Sabrina akiwa mke wangu mimi.” Mpaka Sabina ikamgusa.

“Kweli simfahamu Sabrina! Au niseme yupo sahihi. Tumekuwa kama tumemtelekeza. Amekuwa kwenye maisha yetu, lakini sisi tumeshindwa kuwa kwenye maisha yake!” Kimya. Jack hakutaka hata kuongeza hapo. “Haya Jack. Nimefurahi kukufahamu zaidi ya jina. Angalau tumeongea kidogo nimeelewa sio kwamba Sabrina amekurupuka tu. Anaolewa na mtu anayemfahamu na kumpenda. Kwa hiyo hata nikizungumza na wazazi, nakuwa na kitu chakuongea zaidi.” “Nitashukuru ukiturahisishia, na kukuona kwenye harusi yetu.” “Oooh lazima. Najua huko nitakutana na wakubwa wa hii nchi.” Ikamuumiza kidogo Jack kuona lengo si kuja kujumuika na mdogo wake ila kukutana na watu wengine! “Na Sabrina atakuwepo kama mlengwa mkuu na sababu yakutukutanisha wote.” Jack akaongeza taratibu tu na kumfanya Sabrina ajisikie vizuri.   Sabina akacheka. “Kweli naona unampenda Sabrina! Nawatakia kila la kheri. Nitawataarifu kile wazazi watazungumza.” “Asante sana.” Jack akashukuru na kukata simu.

Sabina Kwa Wazazi.

S

abina akabaki ameshikilia simu, haamini! Ikabidi kuanza kutafuta habari za familia kiyo ya Msindai kwa haraka mpaka akazipata kwa kina. Ndipo akampigia baba yake simu baada ya kumpata kaka mkubwa, yaani anayemfata huyo Sabina ndio Sabrina. “Upo na mama?” “Yupo karibu. Kwani vipi?” Baba yake akauliza. “Naomba mkae karibu muweke simu kwenye spika, hapa nipo na Seba kwenye line pia.” Wakashituka. “Kwema?” Baba yake akauliza kwa wasiwasi. “Ushaweka kwenye spika, mama anasikia?” Sabina akauliza. “Nipo. Kwema?” Akauliza mama yao. “Kwanza shikamooni?” Na Seba naye kaka yake Sabrina akasalimia. Wazazi wakaitika. “Kuna nini!?” “Mnawafahamu kina Msindai?” Akauliza Sabina. “Yule ambaye mama alikuwa waziri wa afya? Baba daktari wa watoto wa muda mrefu sana alikuwa pale hospitali ya taifa Muhimbili? Nafikiri amefungua hospitali yake sasa hivi yule mzee, au sijui!” Baba yao akawa kama anajaribu kuwatambua. “Au unamzungumzia huyu wa sasahivi?” Akauliza Seba.

“Ewaa! Naona wote mnawajua. Yule aliyekuwa waziri wa afya awamu ya Mkapa, ni mama na huyu waziri wa sasa hivi ndiye mtoto wake wakwanza. Anao watoto wa nne. Imebidi kuanza kutafuta habari zao.” “Kwa nini?” Akauliza mama mtu. “Subiri kwanza mama. Sasa mtoto wao mkubwa au wa kwanza ndio huyo waziri, wanafuata wakike wawili, mmoja anayemfuata huyo waziri huyo dada mkubwa wa kike yeye yupo Usalama wa taifa pale, ndio nasikia ndio mkubwa wao pale. Halafu anayemfuata tena huyo wakike wa pili nasikia ni daktari pia wa watoto, anafanya hapohapo Muhimbili na kwenye hospitali ya familia. Halafu wanaye mtoto wa mwisho au mdogo wao anaitwa Jackson, yeye anafanya wizara ya fedha, kama muhasibu Singida mjini.” “Ni familia iliyoendelea sana!” Akasifia baba yake.

“Wewe mbona unawafahamu sana hivyo!? Kuna nini?” Mama yake akazidi kudodosa. “Imebidi kutafuta habari zao kwa haraka. Maana Sabrina kanipigia simu muda si mrefu akiwa na huyo Jackson. Wanafunga ndoa ndani ya miezi miwili kuanzia sasa, tarehe wamesema watatujulisha.” Pakazuka ukimya wa hali ya juu. “Sasa huo mshangao mimi ikabidi kumuhoji sana huyo Jackson Msindai.” “Umezungumza naye huyo mtoto wa Msindai!?” Akauliza baba mtu kwa mshangao sana.

“Ndiyo. Sasa si ndio maana ikabidi kuanza kutafuta habari za hiyo familia vizuri ili kujua kama ni kweli au utapeli tu. Ndio nikaambiwa ni kweli hiyo familia kijana wao wa mwisho yupo Singida, anaitwa Jackson.” “Makubwa!” Mama mtu akahamaki. “Wala si madogo. Nikamuuliza huyo Jack juu yake na Sabrina. Akasema walikutana chuoni. Akamtongoza Sabrina, Sabrina akamkataa. Lakini baadaye wakarudi kwenye mahusiano yakawaida. Anasema Sabrina yeye alimwacha chuoni, lakini wakaendelea kuwasiliana. Anatufahamu sisi wote mpaka kwa majina yetu! Tena kwa muda mrefu tu. Anasema lakini yeye alijua Sabrina ndiye mke wake, akawa anaendelea kumsubiri. Jana, siku ya jumapili anasema akamjaribisha tena kumuomba safari hii sio tu mahusiano, ni kumtaka aje awe mkewe. Anasema kwa mara ya kwanza Sabrina amemkubali. Hivi amemvalisha pete ya uchumba. Na amesema hasubiri tena. Alichokuwa akisubiri ni Sabrina kukubali. Maadamu Sabrina ameshamkubali, wanaoana kwa haraka sana.” “Hawana sababu yakusubiri, si pesa ipo!” Akaongeza Seba. Wazazi kimya wapo kwenye kutoamini.

“Alichosema Sabrina, anachoomba kutoka kwenu ni mpokee mahari yake. Mseme lini mtakuwa tayari, waje hao kina Msindai kutoa mahari. Mimi nikamwambia mnaweza kukataa kwa sababu mnataka...” “Hee! Wewe Sabina vipi?” Mama yake akashangaa sana kwa kuhamaki. “Subiri kwanza mama. Maana ni juzi tu ulikuwa ukimlalamikia Sabrina na maisha yake mabovu ukitaka arudi shule angalau asomee ualimu. Ndio nikamwambia labda mnaweza kukataa. Hapo nilikuwa sijajua kama anaolewa na kina Msindai.” Wote wakacheka sana.

“Kumbe! Nyinyi mngekubali alete mchovu kama yeye!?” Wote wakazidi kucheka. “Lakini bwana Sabrina amebadilika! Sio yule mnayemfahamu nyinyi. Amenijibu kwa wazi kabisa, yeye hajapiga wala hatawapigia kuomba ruhusa. Nikututaarifu tu. Kwa heshima anataka asipite kipengele cha mahari. Lakini amesema, sisi tuwepo, tusiwepo. Tukubali, tukatae, yeye anaolewa. Tena kwa ukali kabisa kama asiyejali tena.” “Makubwa! Sasa na sisi atatupigia lini simu atuambie au ndio ametukasirikia kwa kuwa hatumpigii simu kama tunavyokupigia wewe?” Sabina alishawaambia malalamiko ya Sabrina. Wakayapuuza. Lakini sasa hivi mambo yamebadilika. Sabrina anaolewa na kina Msindai.

“Maana sisi ni wazazi. Hata kama tulikosea, bado anatakiwa atupigie sisi simu atuambie yeye mwenyewe.” Akaongea kwa kulalamika baba yao. “Amesema atawapigia, lakini alisema anataka mimi ambaye mnanielewa kwa haraka na mnanisikiliza ndio nianze kwanza.” Pakazuka ukimya. “Sasa mnasemaje?” “Ndio atupigie yeye mwenyewe.” Akaanza kibabe baba yao. “Yeye atupigie sisi simu, atutaarifu mwenyewe. Hiyo ndio heshima” “Sawa baba, lakini nataka tu kuwatahadharisha. Sabrina anao mtazamo wake juu yenu. Anajua nini mtazungumza na anajua huwa hamumsikilizi na hamjali anachojisikia.” Sabina akaanza taratibu tu.

“Nilizungumza naye alipokuja hapa kwangu, na leo nimemsikiliza kwenye mazungumzo yake. Tabia yakumkosoa na kumsema vibaya hata mbele yakina Simon, ambao anaona ni wadogo sana kwake, inamuuma sana. Anajua wazi kuwa huwa hatumfuatilizi, nyinyi kama wazazi mnamdharau na bado anao ule usemi uliokuwa ukimwambia mama.” “Usemi gani? Kama sio ananitafutia tu sababu!” Akakana mama yao bila hata kujua ni usemi gani yeye kama mama aliokuwa akiusema na kumuumiza mwanae huyo, Sabrina. “Vile ulivyokuwa ukisema yeye ni fungu la kukosa.” “Halafu nilikukataza mama. Sijui kama uliacha! Hata mimi alinilalamikia na kusema ilibidi mpaka aende akaombewe ili kutoa hilo jina kwenye maisha yake.” Seba kaka yao akaingilia. “Mimi nilishaacha. Kama anashindwa kusamehe ni yeye tu.” Mama mtu akazungumza kwa jazba.

“Hapana mama. Naomba katika hili kama mnamtaka Sabrina arudi kwenye maisha yenu, mjishushe. Ameondoka zaidi ya miezi minne sasa, na wala haonekaniki kutaka kurudi nyumbani, bado anamalalamiko na nyinyi. Ameniambia kwa ukali kabisa, amechoka kutukanwa na kunyanyaswa. Wote tumekuwa tukidharau alichokisoma, lakini ndio kinampa mume! Tena huyo kijana anaonekana anampenda na kumthamini sana Sabrina.” Kimya.

“Binafsi nimejisikia vibaya sana mbele ya huyo kijana. Anatufahamu sisi wote mpaka Simon, lakini mimi kama dada yake Sabrina, simfahamu kabisa wakati anasema amekuwa na Sabrina kwa miaka mitano! Hakika nimejisikia vibaya na aibu. Hata yeye amejua Sabrina ni mtoto kwenye familia ambayo yupo mpweke. Anasema amechelewa kuoa kwa kuwa alikuwa akimsubiria Sabrina. Anasema anaoa mwanamke anayemfahamu na kumpenda. Sasa kazi kwenu. Mnaweza kuwa wageni kwenye harusi ya mtoto wenu au walengwa. Mimi nimefikisha ujumbe, mtoto wenu anaolewa na mtu maarufu sana hapa nchini. Mjipange.” Sabina akawaaga na kukata simu.

Wazazi hao wawili wakabaki kimya kila mmoja akiwaza lake. Wamdhaniae ndiye, siye. “Sabrina!” Wote ikawa haiwaingii akilini. “Msindai!” Bado haikuwa ikileta maana. Kwa jinsi wanavyomuelewa Sabrina, lilikuwa jambo ambalo haliwezekani. Heri ingekuwa Sabina! Sabina anakutana na wasomi wengi. Anasafiri nchi mbali mbali. Anahudhuria mikutano ya wakubwa. Yaani Sabina ndiye angestahili kuolewa na watu kama kina Msindai, lakini si Sabrina!

Kwa Kina Msindai.

J

ackson huyu, ni mtoto wa mama haswa. Kiziwanda ambaye kabla hajaimaliza siku yake, basi lazima amalize na mama yake pia. Hajawahi kukua kwake. Swala lakuuliza kama amekula au amekumbuka kunywa maji siku hiyo lilikuwa jambo la kawaida sana. Jumbe katikati ya siku akiambiwa na mama yake, ‘Jua kali sana huko nje, kunywa maji sasa hivi kabla hujasahau.’ lilikuwa jambo la kawaida. Kupigiwa simu kwa video ili amuone alivyopendeza siku hiyo kazini, huku akimtaka arekebishe tai hivi au vile, lilikuwa jambo la kawaida sana tu. Hata kazini walishamzoea kumsikia mama Msindai kwa njia ya simu akizungumza na huyo mwanae. Jack mziwanda wa mama Msindai.

Akampigia simu mama yake. “Nilikuwa nakuwaza sasa hivi. Nimekununulia soksi nzuri sana, nimesahau kukupa juzi ulipokuja nyumbani. Kwanza weka video nikuone.” “Nisikilize kwanza mama.” “Umepata mchumba?” Akamtania asijue kama safari hii amepatia. “Ndiyo.” Jinsi Jack alivyojibu, mama yake akajua ni kweli sio utani. Akanyamaza. “Mama, umenisikia?” “Usinitanie Jackson!” Jack akaanza kucheka. “Kweli mama. Nataka kumuoa Sabrina.” “Wewe si ulisema Sabrina amekwambia uendelee na maisha yako haji tena Singida!?” Sabrina akashituka mpaka akakaa akiwa ametoa macho.

“Nipo naye hapa?” “Kwa nini alikataa kwa mara nyingine tena na kwa nini sasa hivi amekubali?” Likawa swali zito na la kumshitua zaidi Sabrina. Akaishiwa nguvu kabisa. “Jackson!?” Wakamsikia mama yake akiita, tena si kwa utani. “Nakusikiliza mama.” “Maana kama kumbukumbu zangu bado zipo sawa ni kama miezi minne tu imepita, alipokwambia hatakuja Singida, uendelee na maisha yako. Au naongopa?” “Ni kweli.” Jack akajibu akisikika kuishiwa nguvu. “Sasa kipi kimebadilika!?” Mama huyo, aliyeshika wadhifa wa juu mpaka kuwa waziri, ameongoza madaktari bingwa wa nchi nzima, muelewa mambo, akataka majibu ya kueleweka akilinda kiziwanda chake. Sabrina hakujua kama Jackson ndio anazungumza na mama yake kila kitu! Na yeye akahisi mwili unakufa ganzi, akasimama na kuondoka hapo kabisa kama kuwapa nafasi Jack na mama yake.

~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kila kazi, inamalipo yake. Kile pando, lina mavuno yake.

Nini kitaendelea?

Mizani  ya Tino Ililemea kwake, akatoa muhanga mtoto na Sabrina. Sasa safari hii Jackson Msindai. Atahimili joto ya jiwe?

Kila Baraka Ina Changamoto zake na ni Ngazi ya Kupanda Maishani.

Wenye nguvu wanahimili, wanapanda kwa machozi na kuvuna kwa shangwe. Wadhaifu huishia katikati wakiyumbishwa.

Simulizi ndio Inaendelea.

Usikose kufuatilia Mapenzi, Uzazi, Siasa, Ya nyuma na Yajayo mbeleni 

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment