“Sasa kipindi kile alikuwa amepata kazi ya muda mfupi. Nakumbuka hata
wewe nilikwambia mama. Nikakwambia amesema hana uhakika itaisha lini, kwa hiyo amenishauri
niendelee tu.” “Alipata kazi gani?” Mama yake
akauliza. “Alikuwa akimuuguza mtu. Wakahamia kwa
matibabu KCMC, alipopata nafuu akamuacha Sabrina, Moshi akiwa amemruhusu na
kumlipa. Kwa hiyo Sabrina aliponiambia yupo Moshi anatafuta kazi, akijua
ameshanichelewa mimi, pengine nilishaanza biashara na mtu mwingine, ndipo
nikamfuata. Mimi ndiye nilimfuata Sabrina, Moshi na kumuomba aje na mimi huku.
Nilimfuata ijumaa iliyopita. Amekaa hapa kama week moja ndio jana nimemuomba
nimuoe.” Mama Msindai kimya akisikiliza.
“Sabrina ananielewa mama yangu. Huku kuishi naye hapa kwa juma moja
tu, tena kama rafiki wala si mpenzi, nikiwa bado na Pam, nimegundua kwa nini moyoni
nilikuwa nikimsubiri Sabrina.” Jack akaendelea
taratibu. “Inamaana anamfahamu Pam!?” “Alikuwa akiishi
hapa huku akimjua Pam kama ndiye mpenzi wangu na akaheshimu hilo. Ila mimi
mwenyewe ndio nimeshindwa mama yangu. Sabrina ananikamilisha kwa namna ya ajabu
sana.” Jack akaanza kumsimulia mambo aliyomshauri na jinsi alivyomtia
moyo akiamini kile anachokipenda Jack, mama yake akimsikiliza tu.
“Kama ukitaka kuniona ninafuraha daima, nisaidie nimuoe Sabrina.”
“Kwani mimi nimekataa! Ninachotaka upate mtu anayekupenda Jack, sio mtu ambaye
atakutumia tu. Yaani awe ameshindwa huko maisha ndio ukawa wewe kimbilio! Mambo
yakimnyookea mbele ya safari, anakukimbia.” “Sio Sabrina mama. Ninauhakika na Sabrina.
Akiamua kusimama na wewe, au akisema ‘ndiyo’ kwako, hayumbishwi. Unakumbuka
chuoni?” “Nakumbuka.” Mama Msindai akajibu. “Ule ndio wakati ambao nilimpenda Brina zaidi, mama. Japokuwa
nilikuwa na sifa zote. Wengine wakinitetemekea, lakini Sabrina alinikataa
sababu alikuwa kwenye mahusiano mengine, tena sio hata kwamba yalikuwa
mahusiano mazuri, ila bado aliyaheshimu hakutaka kumsaliti mwenzie kwa ajili yangu.”
Jack akaendelea.
“Sabrina ana msimamo, mama. Halafu kingine kikubwa, anaheshimu
maamuzi yangu na anataka niwe na furaha. Amekuja kuishi na mimi hapa, akijua
nipo na Pam kwenye mahusiano, akaliheshimu hilo japo alikuwa akitamani kama
angerudisha miaka nyuma, wakati ule angekuwa hayupo kwenye mahusiano,
akanikubali.” “Umejuaje Jack mwanangu?” “Ameniambia mwenyewe mama. Brina mwenyewe
aliniambia tena hata kabla yakuniambia niendelee na maisha yangu hivi karibuni
tena. Kuna siku alinitumia ujumbe, sema sikukuonyesha. Alikuwa bado yupo kwao.
Aliniambia kama angekuwa na uwezo wakurudisha miaka nyuma, angerudisha mpaka
siku aliyosema ‘ndiyo’ kwa mwanaume aliyekuwa naye siku mimi nikimtongoza
chuoni, ili aseme kwake ‘hapana’, ili wakati ule mimi namtongoza, angekuwa hana
mtu, ili anikubali mimi. Akaniambia kabisa, lakini hawezi tena, na anasikitika
amechelewa. Nakumbuka sikuujibu ule ujumbe, na wala sikuuzungumzia hata na yeye
mwenyewe, yaani leo ndio nakwambia wewe.” Jack
akaendelea taratbu akimuaminisha mama yake.
“Na ndio baadaye nilipokuja kuwa naye kwenye urafiki tu wakawaida, ndio
nikaja kugundua wakati ule akinikataa mimi sio kwamba alikuwa kwenye mahusiano
mazuri sana. Lakini nilimsikia akikiri alikuwa kwenye manyanyaso makali sana
huko kwa huyo mwanaume mwingine, lakini hakumsaliti mpaka yule kaka mwenyewe
alipoamua kumuacha, ndipo Sabrina akachora mstari kwenye hayo mahusiano, hata
yule kaka alipomrudia na kumuomba msamaha akitaka kumuoa, Sabrina alimkatalia.
Lakini hakumsaliti. Sabrina anamsimamo mama. Akisema ‘ndiyo’ yake ni ndiyo, sio
mbambaishaji. Ukiwa naye, unauhakika na mtu wa kusimama na wewe kwa hakika.” Jack
akaendelea, mama yake akimsikiliza tu.
“Nampenda Brina, mama. Kama ukitaka kuniona nafuraha wakati wote,
nipe baraka zako nimuoe Brina wangu. Ni mwanamke niliyekuwa nikimsubiria kwa
muda wote huo, na wewe unajua. Tafadhali mama yangu.” “Lini unataka kuoa?”
Mama yake akamuuliza. “Haraka iwezekanavyo. Sitataka
harusi kubwa na ya garama sana. Tuna mipango mingi sana mimi na Brina, na yote
hiyo inahitaji pesa. Hatutaki kupoteza pesa kwenye harusi wakati tunaweza
kutumia hiyo pesa kusaidia maisha ya watu huku. Brina amepitia miradi mingi ya chama
ambayo imekufa. Amenishauri mimi kama mwenyekiti wao, niifufue tena.
Tumeshauriana njia ya kuifufua, tumepiga mahesabu tumeona tutahitaji pesa
nyingi. Sasa najua watu ambao nitaomba michango yao kwenye hili la chama, ndio
haohao nao tutawachangisha kwenye harusi. Sasa ndio maana tunaona tufanye kitu
kidogo cha pesa ndogo kutoka kwetu sisi wenyewe. Kisha baada ya harusi
tutafanya harambee kubwa ili kupata hiyo pesa.” Akamsikia mama yake
anacheka taratibu. Akajua amegusa moyo wa mama yake.
“Sasa hiyo ndiyo roho ya uongozi. Kufikiria wengine sio wewe tu.
Sasa hiyo harusi itafanyika huku au huko?” “Nafikiria huko nyumbani ambako
ndugu wengi wapo huko.” “Umpigie simu na baba yako umtaarifu ili tuanze mipango.
Umemwambia Junior?” “Nimezungumza naye, na yeye ndiye aliyenisaidia kutafuta
pete ya uchumba. Na kuniambia nisisubiri tena. Nimwambie Sabrina kwa wazi ili
nijue kwa hakika kama ni wangu au niendelee na maisha yangu.”
Jack akaharibu bila kujua. “Kumbe umeshachumbia!?”
Mama yake akaulizi kwa kulalamika akishangaa sana kwamba amepitwa!
“Sikujua kama Sabrina angekubali, mama!” “Sawa.” Jack
akajua ameumia. “Sikutaka ujue kama nimekataliwa tena mama
yangu. Nilijua ungeumia.” “Mimi ni mama yako Jack. Na hatujawahi kufichana
jambo lolote. Unafikiri mimi ndio napenda kusikia tu habari njema kutoka kwako
halafu mbaya uwe unaumia mwenyewe?” “Basi nisamehe mama yangu. Sitaki kukuudhi
na sitaki tukosane hasa kipindi hichi ninachotaka kuoa. Si unakumbuka
ulivyokuwa unataka nioe?” “Naona mambo yenyewe yameanza kwa vificho vificho!
Nakuwa kama mtu wa pembeni tu!” “Mama!” “Naelewa, wala silalamiki. Nishaelewa
kuwa mambo ya muhimu kama kuchumbia, unamuhusisha kaka yako. Mnaenda kutafuta
naye pete. Mimi ambaye nilikuwa nakuombea, na kukutafutia wasichana, japo
umekuwa ukiwakataa, na sikuwahi kulalamika wala kuchoka, ukaniacha, nakuja
kusikia tu kwamba umechumbia! Tena kwenye stori tu! Lakini naelewa.”
Jack akajua kumeshaharibika, si kitu kidogo kama alivyodhania mama yake
atachukulia.
“Kaka alisema safari hii niende umbali mkubwa zaidi mama. Hata
sikuwa na wazo lakuchumbia. Alinikuta hotelini na mwanamke.” “Pam?” “Si unaona
hata Pam unamjua! Mimi sikufichi mama yangu kipenzi.” “Mmmh!”
Akaguna kwa kulalamika. “Mama! Nilimuaga Brina nakwenda
mapumzikoni na Pam! Hebu fikiria mama yangu, halafu nije kumuomba kumuoa!
Sikujua kama angenikubali.” “Narudi kwenye pointi yangu ile ile Jack. Wewe ndio
katoto kangu kamwisho. Sitakiwi kusikia mambo kutoka kwa watu. Mimi ndio
natakiwa kuwaambia watu mambo yakiziwanda wangu! Sio vinginevyo.” “Nisamehe
mama yangu kipenzi. Nimekosa.” Jack akambembeleza hapo kama dakika tano
mbeleni ndipo marafiki hao wapenzi wakapatana.
“Kuna kitu kingine nitakuja kukwambia mimi mwenyewe siku ya
jumamosi. Hicho nichamuhimu sana. Nataka nikwambie tukiwa tunaangaliana
machoni.” “Ni nini?” “Mama Msindai!” “Nidokeze tu.” “Hapana mama. Nataka
kukwambia nikiwa nakutizama hivi. Sio kwa simu.” “Basi mimi sitakaa kwa amani.
Nitakuwa nikiwaza tu. Mpaka jumamosi kote huko!” “Mama, kwaheri. Nitakuona
jumamosi.” “Nikupikie nini ukija?” “Nina hamu na ndizi za nyama. Weka nazi
nyingiii.” Mama yake akacheka, wakaagana.
Jack kwa
baba yake.
K |
wa baba yake
hakuchukua hata muda mrefu. Akampongeza sana na kumwambia itamuongezea heshima
kwenye jamii. “Hata mtu akitaka kukupa majukumu mazito,
anakuwa na imani na wewe kwa sababu anakuona umekuwa mtu mzima. Ni uamuzi wa
busara sana.” “Asante baba. Lakini nataka kuoa hivi karibuni. Ndani ya miezi
miwili.” “Kwa nini haraka hivyo!? Umeshamfahamu huyo mwenzio!?” Hapo
Mzee Msindai akashituka kidogo. “Tokea nipo chuoni nilikuwa
naye na tukaendelea kuwasiliana. Kwa hiyo namfahamu vizuri tu.” “Ooh! Kama ni
hivyo huna sababu yakuendelea kusubiri. Nitazungumza na Junior, ashauri tufanye
nini kwa harusi hiyo ya muda mfupi, lakini iwe nzuri.” Mzee huyo alishamjua Jack na mama yake. Akajua
jambo litakapomfikia yeye, basi limeshapita kwa mkewe na lina baraka zake. Hata
akitaka kupinga, mkewe hawezi kukubali. Lazima atamlazimisha mpaka hilo jambo
la Jack alipitishe, lakini si kwa watoto wao wengine. Na ukimsikia huyo mama
akisema, ‘mtoto anataka au mtoto amesema’. Familia nzima wanajua
anayezungumziwa hapo ni Jack.
Mzee
Msindai hakuwa na mengi sana. “Asante baba. Na mimi
nitakuja huko jumamosi.” “Hiyo itakuwa vizuri, ili tuzungumze na kupanga
pamoja.” Wakazungumza kidogo tu, wakaagana. Akawa amemaliza kwa wazazi,
kwa upande mmoja kuwataarifu juu ya harusi tu wala si ujauzito wa Sabrina ambao
si wake. Lakini mama yake alishaanza wasiwasi juu ya Sabrina! Jack akajua
kutakuwa na ugumu zaidi atakaposikia ni mjamzito. Jack akabaki akiwaza hapo
kwenye kochi, Sabrina chumbani.
Kwa kaka
yake.
B |
aada ya
kujiuliza na kujijibu kwa muda mrefu pale, akaishia kujiambia nilazima amuoe
Sabrina tu. Akaweka hasara na faida za kumuoa Sabrina akiwa na mwanae, faida
zikazidi. Akajiambia mvua inyeshe jua litoke, atamuoa tu Sabrina. Akaamua kumpigia simu kaka yake ili kumtaarifu kila
kitu na malalamishi ya mama yake. Kaka yake akacheka. “Mama
hataki ukue yule! Na wala hataki kusikia umekua! Anakuona kama mtoto wakulilia
nyonyo, ambalo analo yeye tu. Kila kitu umlilie yeye kwanza, kiziwanda wake. Na
hataki akushiriki na yeyote yule!” Jack akaendelea kucheka. “Lakini naomba swala la Brina kuwa mjamzito naomba hilo nimwambie
mimi kwanza. Anaweza kuanguka kwa mshituko.” “Kabisa. Ni heri akusikie mwenyewe.
Mimi sitakuwa na maelezo yakutosha.” Wakanyamaza kwa muda. “Nampenda Brina, kaka yangu. Ananikamilisha kwa kila eneo la
maisha yangu.” “Hata kama ni harusi ya haraka, lakini tutakuandalia harusi
nzuri tu, mshindwe wenyewe.” Jack kusikia hivyo, akafurahi sana. Alimjua
kaka yake. Akisema atafanya jambo. Huwa anasimamia mpaka likamilike.
Akamshukuru na kukata.
Kili Kazi
Na Malipo Yake.
J |
ack
akaamua kumfuata chumbani. Akamkuta amepiga magoti pembeni ya kitanda
amejifunika na mto kichwani analia kimyakimya. Akasikia tu akivuta kamasi ndipo
akajua analia. Akaenda kukaa pembeni yake. Kitandani na kutoa mto kichwani.
“Naomba tuzungumze Sabrina.” Sabrina akajifuta machozi, lakini akabaki amepiga
magoti vilevile akiendelea kujipangusa uso. “Haya maswali uliyoyasikia, hatuwezi
kuyaepuka. Yatakuja na yatataka majibu. Leo nimebabaika sana kwa kuwa
sikutegemea swali kama hilo kutoka kwa mama ambaye ananifuatilia kwa karibu
sana. Kila siku asubuhi nikitoka hapa nyumbani kuelekea kazini, lazima kumpigia
na kumsalimia kumtaarifu nimeamka salama na ninakwenda kazini.” Sabrina akabaki
akisikiliza.
“Maswali
yake kwangu ambayo najua itakuja kuwa ngumu sasa hivi ni kama yale ya mama kwa
mtoto wake wa miaka 5. ‘Umekunywa maji, na kwa kiasi gani? Umekumbuka kuweka
chandarua? Umekumbuka kubadilisha mashuka weekend hii? Umekumbuka kupata
kifungua kinywa? Kuna vumbi sana huko, usisahau kunywa maziwa.’ Hayo ndio
mahusiano niliyonayo na mama hata nilipokuwa chuoni ilikuwa hivyo hivyo.
Anaweza akaja hapa Singida kunitembelea ofisini, anaanza kunifunga tena kamba
za viatu miguuni.” Sabrina akashangaa sana. “We Jack!” “Wewe utamuona tu. Mpaka
kina Ibra wanamfahamu na ilibidi niwaambie wamzoee tu. Pale chuo alikuwa akija,
anaanza kunichomekea shati vizuri, tena mbele za watu.” Sabrina ilibidi acheke
tu.
“Sasa
unasemaje?” “Namuacha tu. Sasa nisemeje? Na anafanya bila hata kujijua. Upo
mbele ya marafiki, unamtambulisha, anaanza kukutengeneza hiki na kile kama
mtoto mdogo. Ilimradi mikono yake iwepo mwilini mwangu. Zawadi zake ndio
utachoka. Yeye ndio atakumbuka kuninunulia soksi na nguo za ndani. Sasa
amenilemaza hata sijui kununua hivyo vitu. Leo ananiambia ameninunulia soksi,
ila alisahau kunipa. Sasa hapo inaweza ikawa kweli au nia nirudi tena nyumbani,
anione tu.” Sabrina akajua hapo kazi atakuwa nayo.
“Akipiga
simu, ile tu nikipokea simu nikimwita mama, anajua kama nipo sawa au la. Na
hajui kuachia jambo, atakukera mpaka umwambie kila kitu. Kwa hiyo anafahamu asilimia
89 ya kila kinachoendelea kwenye maisha yangu. Siwezi na sijui kujificha kwake.
Mbaya zaidi akiwa amenipigia nikiwa na hasira, au jambo limeniumiza, ndio
najikuta namwambia yeye kila kitu kama kujituliza. Kwa mara ya kwanza tokea
nazaliwa ndio leo naanza kuona athari yake. Narudije nyuma na kutengeneza
malalamishi yangu juu yako Brina, kuwa hunipendi mimi?” Sabrina akaumia sana.
“Kumbe
ulishamwambia kama sikupendi?” “Wala sitakudanganya Sabrina. Ulipobadili mpango
wa kuja huku, nikiwa nimeshamwambia mama naandaa nyumba Brina anahamia Singida,
nataka kuweka mazingira yakumkaribisha aje aishi kwangu. Nikahangaika usafi
wanyumba. Hata hii rangi unaona ya ukutani nilipaka upya kwa ajili yako.
Nikabadili nyavu za madirisha na kuweka hayo madirisha ya Aluminium unayoyaona
na kujengea mafeni ya juu kila chumba. Yote hayo mama alijua nafanya kwa ajili
yako. Kuja kupata ujumbe wako eti huji tena, umeamua kuanza maisha yako huko,
mimi niendelee tu na biashara nisikusubiri tena, ikaniumiza sana. Nilishindwa
hata kulala Brina. Nilikuwa nikikusubiri online usiku kucha angalau
kukupata nikuulize ni nini nilikosea! Nini kimekufanya ubadili mawazo kwa kazi
itakayokuja kuisha, na huna kazi nyingine! Kumbe mimi nasubiri huku, wewe
ulishani block! Mimi sijui kama umeni block, najua upo
matatizoni. Ndio Ibra akanielewesha kuwa mtu akikublock Whatsapp huoni profile
picha yake kama alikuwa anayo, na simu ukipiga humpati.” Sabrina akajisikia
vibaya sana. Akainama.
“Sasa
siku ile uliponitumia ujumbe na kunibock, katika hangaika hiyo ya kukusubiri online,
mama naye akaniona nipo online usiku, akanipigia. Nikamueleza ukweli,
kuwa nimekata tamaa na nimejua wewe hunipendi kimapenzi labda urafiki ambao
nikionyesha naingia ndani sana ni kama nakuogopesha unanikimbia. Nikazungumza
na mama karibu usiku kucha maana Ibra alishaniaga akasema yeye analala sababu
ya kazi kesho. Nikakaa na mama kwenye simu mpaka nikalala. Simlaumu anapoonyesha
wasiwasi sasa hivi. Anayo haki yakuhoji. Na lazima niwe na majibu ya wazi. Mama
anayo haki Brina. Nilimtwisha malalamiko yangu, sasa hivi hata kama
nimetengeneza na wewe, siwezi kumpuuza tena.” Sabrina akakaa.
“Naelewa
Jack, na wala sikulaumu. Makuzi yako na yangu yapo tofauti sana. Wewe umelelewa
ukiwa karibu sana na familia, zaidi mama. Mimi imekuwa tofauti. Kadiri
nilivyoendelea kukua, ndivyo nilivyozidi kuwa mbali na familia, zaidi mama.
Nimekuwa ni mtu ambaye ananilalamikia sana. Amekuwa akinipa maneno machungu mno
jinsi ninavyomkatisha tamaa kwenye kila kitu. Nafikiri nilikwambia jinsi
alivyoumia baada yakujua sipo tena na Emma ambaye alijua nikimaliza chuo pengine
angenioa. Bila kujua sababu, mama aliumia sana na kulalamika kwa wazi hata
mbele za wale wadogo zangu wa kiume ambao kwanza niliona ni wadogo zangu, pili
ni wakiume Jack. Anataka kuwafundisha nini kwa kuachwa kwangu! Sasa
ikawa hivyo hata kwa Sabina na yule kaka yangu. Wakipiga simu hizo ndio zikawa
habari wanazopewa. Nimesoma kitu cha ajabu, na mwanaume pia nimeshindwa
kumtunza. Akawa akinilalamikia kwa kila mtu, hakuna ninachoweza kufanya vizuri
kwenye maisha na ikawa sasa nafikiri imemuingia akilini, hata nimfayie kitu
gani kizuri pale nyumbani, hawezi kushukuru kama akijua ni mimi nimefanya,
lazima atatoa kasoro tu.” Sabrina akaendelea taratibu tu.
“Hiyo
kitu ikawa inaniumiza sana na kunimaliza nguvu kupita kazi nyingi nilizokuwa
nikifanya pale nyumbani. Nikawa sina kimbilio, na simu kama nilivyokuwa nikikwambia
wakati ule ulipotaka kuniletea simu. Ilikuwa napata mawasiliano pale wadogo
zangu wanapokwenda shule. Kwa hiyo ninapokuwa nao nyumbani, wale wadogo zangu
ambao nao wakajifunza kunidharau kwa kejeli kutoka kwa mama aliyekuwa
akinifananisha nao. Kuanzia matokeo shuleni, kuwa wao wanaakili kuliko mimi na
utendaji kazi wao pale nyumbani na uwezo mkubwa wakufikiria walio nao kuliko
mimi mjinga.” “Sabrina! Alikuwa akikwambia hivyo!?” Jack akaumuuliza kwa
kuumia.
“Kabisa
Jack. Tena si kwa kujificha, mbele yao. Tusi lake kubwa ilikuwa, ‘mjinga
kabisa wewe’. Kwa hiyo hata wale wadogo zangu walikuwa wakiniita mjinga.
Utasikia wakiniambia, ‘wewe si mjinga tu’. Hapakuwa na heshima hata
kwao. Sasa ukumbuke hapo wao ndio nilikuwa nikiishi nao. Baba kunichapa hata
mbele yao lilikuwa jambo la kawaida sana tu. Nikitumwa sehemu nikachelewa, au
ng’ombe wakimwaga maziwa, watasahau yote niliyofanya mazuri siku hiyo,
nitachapwa mbele ya wale watoto, tena na matusi juu. Zaidi nikichelewa kurudi
nyumbani hapo baba alikuwa akinitandika, anasema nimeanza mambo ya wanaume,
nataka kuleta watoto pale ndani wasio na baba. Nilikuwa natoka kwa shida Jack!
Hata kusuka ilibidi nijifunze kujisuka mwenyewe, tena usiku maana kwanza sikuwa
na hela, pili muda sikuwa nao. Kwahiyo ukisema niende nikimaliza kazi, ni
jioni. Kusukwa mpaka nimalize, tayari giza limeshaingia, nikirudi nyumbani ni
kuchwapwa.” Sabrina akainama.
“Unaona
huu upande wa kushoto? Kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Nywele zake ni nusu ya
upande huu kwa kuwa nilichelewa kurudi nyumbani, nilikwenda kusukwa rasta za
mabutu, siku karibu na ya chrismasi. Nikasema angalau siku hiyo na mimi
nipendeze. Kina Sabina na kaka walikuwa na wao wanakuja nyumbani. Ndugu wa
vijijini walikuwa pia wanakuja. Nikasema na mimi angalau nijipendezeshe. Sikuwa
na wasiwasi kwa kuwa kulikuwa na watu kutoka kijijini, nasaidiwa kazi pale.
Nikatoka kwenda kusuka. Rasta huwa zinachukua muda mrefu kusukwa. Basi kipindi
hicho nikasema ndio kipindi muafaka kwenda kusukwa kwa kuwa kuna watu pale nyumbani,
kama kuna kitu chakufanywa, basi watatumwa wao. Lakini ikawa kinyume kabisa. Sitasahau
jinsi nilivyodhalilika siku ile Jack. Nilitoka nyumbani mchana, nikarudi saa
moja usiku.” Sabrina akainama, akamuona anacheka kwa kuguna.
“Nilipokelewa
mlangoni. Ngozi ya kichwa ilikuwa ikiuma sababu ya kuvutwa wakati wakusukwa.
Mama akanishika kichwa na kunivutia ndani. Mbele ya wadogo zangu na wageni.
Jack, nilichapwa kama mbwa. Hapo hapo akanikata huu upande wote, akaniambia
anione sasa kama nitapata sababu ya kwenda kuzurula. Hapo wadogo zangu
wanacheka na kushangilia.” “Haiwezekani Sabrina. Kwani hukuomba ruhusa?” “Jack,
natokaje kwenye ile nyumba bila kuomba ruhusa? Tena sio mimi, Sabina ndiye
aliyeniombea. Niliomba simu ya mama mdogo, alikuja hapo nyumbani kwa ajili ya
sikukuu, nikampigia Sabina. Nikamuomba hela ya kusukwa, na nikamuomba aniombee
ruhusa kwa baba, nikasukwe. Tena baba akiwa na mama wakasema, kama nikimaliza
shuguli zangu zote, ndio niende. Nikafanya shuguli zangu zote, ndipo nikaenda.
Kaka anakuja nyumbani na Sabina, wanakuta upande mmoja nywele zipo nusu. Na
mimi pale nyumbani ndio wananisifia kwa nywele nzuri. Zinakuwa kwa haraka,
halafu laini. Nikifumua hizi nywele utaona. Ni ndefu sana japo zimepishana.
Sabina akashangaa sana. Akaniuliza kwa nini nipo vile! Wale wadogo zangu wakawa
wanasimulia pale mbele za watu huku wanacheka. Nakumbuka kaka alikasirika sana
nakushindwa hata kuvumilia. Akaongea palepale tena kwa kugomba sana. Ilibaki
kidogo awachape wale watoto ila akawakemea sana. Lakini na yeye siku zilipoisha
akaondoka kama Sabina ambaye ni kama Mungu mtu pale nyumbani, nikaachwa na watu
walewale, maisha yangu yakaendelea vilevile.” “Daah!” Jack akashangaa sana.
“Tuache
hayo, lakini ile hali ikanifanya nianze kumuuliza Mungu ni kwa nini mimi
anaruhusu kudhalilika kiasi hicho na nipitie hapo? Katika kuendelea na hayo
maswali, ndipo nikakutana na Yesu. Jack, Yesu yupo. Mwenye nguvu na
mamlaka yake.” Mpaka Sabrina akaanza
kutokwa na machozi. “Nikataka kumfahamu Mungu
aliyeniumba. Yale manyanyaso, yakanifanya nitumie bibilia ya baba, nikaanza
kumsoma na kutaka kumtambua Mungu. Kumbuka sikuwa na rafiki wala mawasiliano
mpaka wale watoto waende shule ndio angalau ulikuwa unaweza hata kunipata kwa
simu tena mama akifurahi. Nikimuudhi, ujue napokonywa simu. Siwezi kukaa nao sebuleni
kuangalia tv, ni jikoni kama nimemaliza kazi. Hapo ndipo nikakutana na Yesu.
Bila kuhubiriwa na mtu, mimi mwenyewe tu.”
“Anyways.” Sabrina
akajifuta machozi vizuri. “Mambo hayakubadilika pale nyumbani. Lakini nikapata
nguvu za ajabu sana Jack. Furaha ambayo sikuwahi kuwa nayo. Amani na utulivu
nikimsubiria Mungu bila malalamiko huku nikimkumbusha ahadi zake kwenye bibilia
juu yangu. Sikumwambia mtu kitu kinachoendelea kwangu, lakini nikawa najitahidi
kufanya kazi bila kuchoka. Lengo likawa limebadilika sasa, nafanya kwa bidii
ili Mungu anione wala si wazazi tena. Hata wakinitukana, nikawa sina shida.
Ilimradi nimefanya kwa uaminifu, Mungu wangu ameniona, nikawa sijali. Ila
nilimwambia hivi Mungu, kwa kuwa nafanya sana kazi. Nataabisha huu mwili,
nikamsihi Mungu asiruhusu kuchapwa tena. Na kweli Jack, ikawa kama muujiza
kwangu. Wakati mwingine mama au baba unakuta ametoa kabisa mkanda kiunoni ili
anichape, moyoni naanza kumlilia Mungu na kumkumbusha, basi unashangaa baba
anagari kunichapa. Anarudisha mkanda wake kiunoni, au kama ni mama, ananitukana
tu, nakuishia kutupa fimbo.”
“Napo
hayo maisha yakaendelea, nakumbuka nikamuomba tena Mungu anisaidie kulainisha
mioyo ya wazazi, waniruhusu kwenda kwa Sabina, angalau nikapumzike kidogo. Nayo
hiyo ni habari ingine, tuache. Ila Mungu akafanya. Lakini nilipofika kwa Sabina,
ili nipumzike, rafiki yake ambaye ni mke wa Tino aliponiomba nikamsaidie kukaa
na mumewe. Nikisema kukaa, namaanisha kukaa haswa. Hakutaka hata nimguse Tino.
Alikuwa amemfungia kama mnyama. Alinifungulia tu mlango kunionyesha
alipomfungia, yeye mwenyewe yule dada alikimbia. Chumba kilikuwa kinanuka Jack!
Sio kinyesi tu, yaani kama kitu kilichooza. Lela alikuwa anakwenda kupumzika na
mwanaume wake, na kina Sabina. Sasa ili watu wasimuone amemtelekeza mumewe, akataka
mtu wakuwepo pale ili tu awaambie watu hajamuacha Tino peke yake nyumbani,
amemuachia mtu wakumuhudumia. Lengo lake sio Tino apone, ilikuwa ni aendelee
kuwa mdhaifu vile vile ili yeye aendelee kula pesa ya Tino.” Sabrina
akamuelezea mkasa wa Lela na Tino kwa kifupi ila kwa undani, Jack akabaki ameshangaa
na kuumia sana.
“Sasa
kwa nini naye Tino alioa mwanamke wa namna hiyo akijua hana mapenzi ya dhati
kwake?” Sabrina akacheka. “Unamuona hivyo alivyo Pam?” Jack akanyamaza asijue
kwa upande upi. “Basi uzuri aliokuwa nao Pam, ndio kama Lela, sema yeye Lela ni
mwembamba zaidi juu halafu Pam mwili wake mnene zaidi. Mweupe kama anakwenda
kuwa muarabu hivi, halafu mtoto wa mjini anayejua kujitengeneza. Ukimwangalia
Lela, hutachoka kumtizama Jack. Mzuri kama hivyo Pam, na maneno mengi hivyo
hivyo kama mapacha sema angalau Pam huwa angalau akiteleza anajirudi, ila si Lela.
Lela ni mkatili, katili ambaye hana aibu. Msafi na anapenda vitu vizuri.
Nafikiri hapo ndipo walipoendana na Tino. Tino ni msafi kwa kumwangalia. Kitu
kisocho na hadhi hanunui wala hamiliki. Hiyo nyumba yao ni safi Jack, imepangiliwa
mpaka vijiko vipo vimewekwa kwa mstari na kwa ukubwa wake. Masufuri na miko vimepangwa
hivyo hivyo.” “Kama wewe huko jikoni?” Sabrina akacheka. “Ilibidi niige Jack.
Wewe mwenyewe utaona aibu jinsi kulivyo pangiliwa. Kila kitu kipo sehemu yake
wakati wote. Ukiingia ndani kwao, hakuna mbu wala nzi, utafikiri upo nchi
nyingine. Wewe fikiria mpaka bafuni na chooni ni pakavu!” Wakacheka.
“Sasa
aliponiacha Lela huku akiniambie nisihangaike kabisa na mumewe, mimi nikaingiwa
huruma. Nikajiambia Mungu ananiona pale nilipokuwa nimekaa tu sebuleni wakati
kiumbe chake kinaangamia ndani. Nikasema hapana. Nipo pale kwa sababu. Mungu
hakuwa amenipeleka pale kwa bahati mbaya. Ndipo nikaingia kwenye kile chumba na
kuanza kumsaidia Tino. Mashuka aliyokuwa nayo kitandani yalikuwa yameganda
kwenye vidonda. Uzuri au ubaya godoro liliwekwa plastiki. Kwahiyo uchafu na unyevu
haukuwa ukienda kwenye godoro, mashuka yanafyoza kinyesi na mikojo, vinaishia
mwilini mwake. Alijawa madonda ya kuungua, sina jinsi nikakueleza ukaelewa. Halafu
Tino alizaliwa na mama mwitaliano. Kwa hiyo ni mweupe haswa, na ana manywele
kila mahali. Nikisema kila mahali, ni mwili mzima.”
“Nikaanza
kazi yakumsafisha yeye kwanza, na kitanda chake. Alikuwa na kila kitu lakini
hakuna wakumsaidia kuvitumia. Alikuwa akitetemeka baridi, maumivu na homa
ilikuwa juu sana. Nilikuja kumtoa manywele mwilini, nahisi yalijaa mfuko. Hapo
ni kuanzia shingoni tu mpaka unyayo. Maana ananywele mpaka vidoleni.” Jack
akashangaa kidogo. “Alikuwa akitisha Jack, kama mnyama wa porini. Kama una roho
ndogo, Tino niliyekutana naye mimi siku ya kwanza, usingemsogelea. Alikuwa akitisha
sana. Nikaanza kumpa chakula na kumuhudumia bila kumsikia mkewe aliyeniambia
nisihangaike naye yupo mtu huwa anamuhudumia, kumbe muongo. Nimekaa hapo nikimuhudumia
Tino bila kuona yeyote mpaka aliporudi siku ya jumatatu usiku maana nilikwenda
pale kwao siku ya jumamosi, na yeye akaondoka siku hiyohiyo na kurudi jumatatu
usiku. Ninachotaka kusema, niliendelea kumsaidia Tino si kwa ajili ya Tino
mwenyewe, ila Mungu. Muda wote huo namuhudumia Tino, wala hakuwa akizungumza.”
“Kwa nini?” Jack akauliza.
“Tino ni wale vijana walioumbwa na Mungu wazuri sana kwa muonekano. Halafu anajipenda na kujijali kupita nitakavyokwambia hapa. Stoke aliyokuwa ameipata, ilimfanya mdomo upinde. Alikuwa akiongea mate yanamwagika, halafu maneni yanatoka kwa shida. Nafikiri hiyo ikamkatisha tamaa yakuzungumza, halafu hakuwa na nguvu kabisa sababu ya ukosefu wa chakula. Mimi mwenyewe nilikuwa nikimuhudumia siijui sura yake anafananaje. Alijawa ndevu uso mzima na nywele.” “Hata hukuona picha!?” “Huwezi amini Jack, hapakuwa hata na picha. Nilipomuuliza mkewe hakutaka kunipa akanijibu hata hajui zilipo. Nilikuja kumfahamu sura alipopata nafuu, nikaamua kumpeleka kwa kinyozi kwa kuwa alikuwa na mba ule ambao ngozi ilikuwa inatoka kichwani. Ndipo nikashangaa uzuri wa yule kijana.” Sabrina akafikiria kidogo, Jack akimtizama.
“Anyway,
turudi kwenye hili ninalotaka kukwambia. Nilipokuwa nikimuhudumia Tino,
nilifanya kama nafanya kwa Mungu wangu kwa asilimia 100. Hapakuwa na mapenzi
wala sikujua kama kunanitakachopata. Kama nilivyokwambia tuliachwa peke yetu
hata pesa aliyonilipa mkewe, nilianza kuitumia kwa matumizi ya pale nikiwa
sijui atarudi lini, huku nikimuomba Mungu na pale asiniache. Tino apone,
aendelee na maisha yake na mimi nije huku kwako. Na ninaomba niwe mkweli Jack,
lengo lakunileta huku kwako tokea mwanzo ilikuwa nikuja kujikwamua kiuchumi
wala si mapenzi.” “Nilijua hilo.” Jack akajibu.
“Kabisa.
Kwanza nilishakuonea aibu. Hata Tino nilimwambia. Nitakwenda kwa Jack sio kwa
mapenzi kwa kuwa kwanza nakuonea aibu. Nilikukataa vibaya sana. Halafu nikajiuliza
swali kama alilokuuliza mama yako. Na Tino nikamwambia. Jack ni mtu mzuri sana
na mstaarabu mno. Nikamsimulia jinsi ulivyonisaidia bila kinyongo chuoni
nilipoachwa na Emma kwa fedheha kubwa vile. Ukanirudishia heshima pale chuoni,
ukahakikisha namaliza chuo. Nikamwambia Jack anastahili mwanamke atakayempenda
kwa dhati na kumuheshimu. Nikamwambia Tino, hata iweje, siwezi kurudi tena kwa
Jack na kumwambia nampenda! Nikamwambia atajua namdanganya. Ni kwa nini
nilimkataa tokea mwanzo, na kwa nini sasa hivi nirudi tena nimwambie nampenda?
Nikamwambia tokea chuo aliponisaidia, nilishajiambia hata ikitokea anaachana na
yule msichana wake wa pale chuoni, sitajisogeza sababu nilishamkataa hata yeye
alishaendelea na maisha yake. Anao wasichana wake.” “Lakini mwishoni
nilikukaribisha na kukwambia zile hisia nilizokuwa nazo chuoni bado zipo,
Brina! Au hukuelewa?” Jack akauliza.
“Ni
kama nilielewa, lakini kwanza nilijikatisha tamaa Jack. Nikasema labda hisia
zakutaka kunisaidia tu au..” “Hisia za kutaka kukusaidia! Come on Brina!”
“Najua Jack, lakini kumbuka na aibu pia. Na kujiuliza na kujiona sitakutendea
haki. Kumbuka hapo nilishamuona Lela na Tino wanavyoishi, tena hata Tino
nilimwambia. Jack ni mtu mzuri sana. Nasita kukurudia sasa hivi sababu ya ugumu
wa maisha na mazingira yangu nikiogopa kurudi nyumbani. Nikaja kwako
nikakukubalia unioe, halafu badaye nikakutenda kama Lela wake! Nakumbuka mpaka
Tino akanyamaza. Nikamwambia ingekuwa mtu mwingine, wala nisingejivunga, ila
sio Jack. Nikamwambia Jack namthamini sana, siwezi kuja kumuumiza. Na yeye
baadaye nilipomueleza juu ya kilichompata yeye sitaki kikupate na wewe kupitia
mimi, akasema anaelewa aina ya ndoa aliyo nayo. Ni kweli.”
“Anyway. Tukaendelea na Tino mpaka tukaondoka naye pale nyumbani. Tino akanipa kitu pekee kilichonifanya kumkimbilia Mungu, na baadaye kumuacha huyo Mungu.” “Kitu gani?” Jack akauliza. “Kunihitaji kwa hali ya juu. Tino alinionyesha hawezi kuishi bila mimi.” “Ambayo ilikuwa ni kweli.” “Kweli kwa uhalisia kuwa alinihitaji nimtumikie sio kama nilivyojiaminisha Jack. Tino alikuwa akinililia nisimuache popote. Hakuwa akitaka niwe naye mbali hata kwa nusu saa! Akanipa kile ambacho hata Emma hakuwahi kunipa. Tino akajaa kwenye maisha yangu na kuniahidi kuwa na mimi daima. Akasema hatutashindwana. Yeye sio mbishi japo ni mkubwa kwangu na amenitangulia kimaisha. Tino alikuwa akiniweka kifuani Jack. Usiku nilale akiwa ananisikia. Tukikaa, anataka japo nimshike. Mpaka analilia penzi langu! Nikalewa, nikamsahau Mungu wangu, nikarukia mapenzi nikijua wazi Tino ni mume wa mtu, na bado hajaachana na mkewe! Na wanayo ndoa ya kanisani.”
“Nikikusimulia
jinsi nilivyoishi na Emma, unaweza kudhani nilikuwa mjinga. Kuna mambo alikuwa
akinifanyia yule kiumbe, mpaka naona aibu kusimulia. Ni manyanyaso ya namna
yake. Niliacha anitumie na kuninyanyasa vile atakavyo huku nikikataa wanaume
wazuri kama nyinyi. Nikajifunga kwake tu, kama niliyechukuliwa ufahamu. Haya, kama
ambaye sina akili, nikijua wazi kabisa nafanya kosa, nikashindwa kusubiri
malipo yangu kutoka kwa Mungu baada yakufanya kwa uaminifu kwa Tino ambaye ni
mtoto wake, nikaamua kujipunja kwa kujilipa mimi mwenyewe. Nikaona Mungu
atanichelewesha, nikajilipa mwenyewe. Nikajilipa kirahisi sana, na shetani
akapata mlango hapo hapo wakunifedhehesha.” “Acha kumwita mtoto ni fedheha
Brina. Usirudie hiyo kauli.” Mpaka Sabrina akalia.
“Hapa nilipo Jack, sipo kwa kuwa nina mkosi wala kauli za mama
yangu ni kweli kwangu. Naanza kuamini natoa mwanya mimi mwenyewe wa kukosea.
Somo nililofundishwa kwa Tino, halijatosha, jana nikiwa hata sijatengeneza
kwako, hatujapanga, wewe si mume wangu Jack, lakini ona nilivyokimbilia
mapenzi! Natoa wapi kibali cha kulala na wewe wakati wewe bado si mume wangu!?”
Jack akashituka sana hakujua kama kibao kitakuja kupindukia kwake. “Nani amenikabidhi
wewe kama ni mume wangu? Baraka za Mungu nimezipata wapi katika hili? Wakati
gani nimerudi kwa Mungu nikamuuliza Mungu juu ya hili? Sio wewe uliyenitoa
Moshi, Jack. Ni Mungu. Nilikaa pale ndani siku tatu bila kula wala kunywa,
nikimlilia Mungu anisamehe na anitoe kwenye ile hali. Nikamlilia Mungu
nikimsihi aniguse tena, anipe tena nafasi ya nyingine na nikamuahidi safari hii
nitaitumia vizuri.” Sabrina akajifuta machozi.
Ndoto ya Sabrina Akiwa Shidani, Mfungoni….
“Siku
ya tatu kwenye mfungo wangu, nikiwa na hili tumbo usiku nikiwa nimelala nikaota
ndoto hii. Nilikuwa nimekodisha gari kama hiace. Daladala kwa matumizi yangu
mimi. Sasa nikawa natumia na nimepewa na dereva. Dereva anafanya kile
ninachomuamuri kwa kuwa kwa wakati ule gari ilikuwa chini ya mamlaka yangu.
Sasa kufika maeneo kama ya pale fire, Dar. Nikawa tumeegesha hilo gari. Wakaja
kina mama wakawa wanapanda. Mimi nikawaambia shukeni, hili gari sio kwa bishara,
nimekodi kwa matumizi yangu. Wakanishawishi sana huku wakitia huruma, kuwa
niwapeleke mpaka hospitali ya Muhimbili, watanilipa. Nikagairi safari zangu na
mipango, nikawapandisha kwenye gari huku nikijua navunja sheria. Haikuwa gari
ya biashara, ila nikawapanga ili trafic wasituone ndani. Tukawapeleka mpaka
Muhimbili, lakini njiani nikaamua kukusanya sasa pesa kwa kila abiria.” Sabrina
akacheka.
“Kila
niliyemsogelea kumuomba nauli, alinipa kikaratasi kimechapishwa na mamlaka kuwa
hatakiwi kutozwa nauli. Wengine ni watoto, kwa hiyo ni wanafunzi, wengine eti
ni watu wazima, ambao hawana kazi kwa hiyo eti mamlaka au serikali imewapa
kibali cha kutotozwa nauli, wasafiri bure. Mmoja tu akanilipa, wakati basi
lilikuwa limejaa watu. Nikawashusha nikiwa nimeumia sana, kuwa nimewapeleka na
kuwafikisha pale halafu mimi sikufaidika! Ikaniuma sana, nikawa namwambia yule
dereva, yaani nimelipwa na mtu mmoja tu tena aliyekuwa amekaa nyuma kabisa,
wengine wote hawajanilipa! Nikahesabu garama niliyolipa kuwafikisha pale.
Kutumia mafuta yangu, gari yangu na mpaka kuvunja sheria na sikulipwa ila mmoja
tu tena ambaye alikuwa kimya kabisa! Nikashituka kutoka usingizini, nisijue
maana ya ile ndoto kabisa.” Jack akabaki kimya akitafakari.
“Naweza
nikawa sikupatia tafsiri nzima ya hii ndoto lakini mimi nikachukulia gari ni
huu mwili wangu ambao ni kama tumeazimwa tu Mungu. Tukifa huu mwili tutauacha
mavumbini. Huu mwili ni mavumbi Jack. Unatuponza tu kumkosa Mungu kwa mahitaji
yake mengi yasiyoisha. Nikajiangalia maisha yangu na jinsi nilivyokwenda umbali
mrefu kuwekeza kwenye maisha ya watu. Nikaanza na Emma. Sijisifii Jack, lakini
nilimbemba Emma bila kuchoka. Siku uliponifuata pale chuoni, ukanikuta nimekaa
peke yangu, nilikuwa nikimfikiria Emma na kule nilikopita naye bila kuchoka
huku akininyanyasa sana. Kile alichokifanya pale chuoni kuninyang’anya vitu halikuwa
jambo geni kwangu kufanyiwa na Emma. Sema alivuka tu mipaka kufanya hadharani,
ila yupo rafiki yake alikuwa anajua ubaya anaonitendea Emma na kumvumilia mpaka
akawa ananishangaa ananiuliza tatizo ni nini! Kwa nini namruhusu Emma kunitenda
vile!”
“Haya,
nikakumbuka jinsi wanavyonitenda nyumbani huku nikiwatumikia kupita kiasi.
Wadogo zangu wakiwa likizo, mama alikuwa akiniambia niwafulie nguo kwakuwa wao
wamechagua kusoma, basi mimi niwafulie, wao wasome au waende tuition,
wakati mwingine nawafulia wao wakiwepo tu hapo hapo nyumbani hata hawasomi.
Nikamkumbuka Tino. Vile nilivyomtoa kwenye hali ya kufa. Nikahangaika naye kwa
garama kubwa nikitumia nguvu zangu, utu wangu, kwa garama kubwa mpaka yakumkosa
Mungu wangu, na mwishoe ninaishia tu mimi kuumia na kukosana na Mungu ambaye
ananipa faraja nikiwa naachwa peke yangu!”
“Nakumbuka
baada ya hapo nikamuahidi Mungu kuwa, endapo atanitoa kwenye ile hali ya
upweke, akanipa nafasi ingine tena, sitamkosea. Nikamlilia mno nikimuomba
msamaha. Nikamwambia narudi kwake nikiwa kwenye hii hali ya ujauzito usio na
baba, nikamwambia yeye ndio atakuwa baba wa huyu mtoto. Atanificha aibu yangu,
nikamkabidhi huyu mtoto. Nikamwambia anitunzie, anisomeshee. Isitokee anataka
kusoma popote, akakosa ada, kwa kuwa nitamdai yeye kwa kila hitaji la huyu
mtoto. Amlinde asiugue na wala asinipokonye. Mimi niondoke kwenye huu ulimwengu
nimuache akitumikia kusudi la kutungwa mimba yake. Nikamlilia sana Mungu,
nikamaliza mfungo wangu, nikiwa sijapata jibu lolote.”
“Nakumbuka
siku ya tatu yake, nikaamka nikiwa nakukumbuka mno. Nikalia kwa uchungu.
Nikarudia ujumbe wa mwisho niliokutumia. Nikalia sana. Usiku nikasema niku
unblock tu, angalau niione sura yako pengine nitalala. Maana nililia sana siku
hiyo nikikukumbuka na kuumia kwa nini nimempoteza mtu mmoja tu ambaye alikuwa
faraja yangu! Ndio nikaku unblock Whatsapp
na kila mahali. Hapo ndio nikamuona Pam kwenye profile yako.” “Ile picha
aliweka Pam mwenyewe, wala sikuwa nikijua kama ilikuwepo. Yaani wewe
ulinishitua nakunifanya nijiulize ulitoa wapi ile picha, ndio baadaye
nikagundua ulitoa kwenye profile yangu. Na nafikiri aliiweka jioni ileile nilipokuwa
naye. Kwa hiyo hata uliponiambia hongera, nikaanza kujiuliza umejuaje habari za
Pam na ile picha wakati sijawahi hata kukwambia! Ndipo wakati tuna chat nikaona
hiyo picha.” Jack akaongea kwa kujitetea kidogo.
“Anyway,
wewe ukanikaribisha tena huku. Nilikataa sababu ileile. Nilikataa nini na sasa
hivi nakubali nini? Aibu! Nikajiambia ni kama ninakufuata sasa hivi kwa kuwa
nimeshindwa huko kwengine, nakukimbilia wewe! Nikasema hapana. Kwanza itakuwa
nikukuchanganya tu, upo na mpenzi wako na mimi nakuja na tumbo langu!
Nikamkumbusha Mungu kuwa huyu mtoto ni wake, siwezi nikampa mtu mwingine mzigo.
Sasa kule kunifuata kwa nia ya kutaka uwe tu na mimi si kwa mapenzi, kuwa utanisaidia
kutafuta kazi, nikakubali kiharaka bila wasiwasi.” Sabrina akakaa vizuri.
“Unakumbuka
ule usiku umelala na mimi pale Moshi na kunikumbatia?” Jack akatoa tabasamu.
“Mungu ndiye anajua Jack.” “Na mimi nataka kujua.” Sabrina akacheka. “Nilijuta,
kwa nini sikukubali tokea siku ya kwanza.” Jack akacheka. “Kuna jinsi
ulinishika Jack, nikapata ulinzi wa ajabu. Harufu yako ikawa kama ndio kitu
pekee nilichokuwa nikikihitaji au nakikosa wakati wote. Kwa miezi yote
niliyokuwa nikilia na kulala usingizi wa mang’amung’amu, lakini siku ile
nikaanza kulala. Na kila wakati ninapokuwa na nguo yako nalala bila shida.
Sikujali tena kuwa unaye mtu wako, ila ile kujua nitakuwa na wewe huku,
kukanifanya nitulie kabisa, nikajiambia sitatembea kesho. Nikajiambia
nitatembea kwa hatua, ila sio mbali na wewe na ndio maana nilikuwa tayari
kutafuta chumba hapahapa Singida ilimradi niwe na wewe karibu lakini sio mbali
na wewe tena. Nikajua wewe ndiye ninayekutaka na ndiye ninayekuhitaji.
Nikamshukuru sana Mungu. Hata siku ile ya jumapili ndio ilikuwa sababu ya mimi
kwenda na Emma kanisani. Nilikwenda kumtolea Mungu sadaka ya shukurani. Kimya
kimya. Nikamwambia Mungu asante. Kwanza, kwa kunitoa kwenye ile hali ya
upweke kule nikiwa sijui nitakwenda wapi, na kunirudishia Jack japo si kama
mpenzi, lakini kama mtu wa karibu yangu sana. Nikatoa ile sadaka ya shukurani
jana.”
“Wala
si mwenzi uliopita Jack. Jana! Ni jana ndio nilikumbuka makuu Mungu
aliyonitendea. Mimi Sabrina ninapakuishi, nina Jack, kama haitoshi, nina
milioni za pesa benki! Zangu mimi! Natoka na kurudi nitakavyo! Sina
wakuninyanyasa wala sina maombi yakutopigwa!” “Ndio maana ulikuwa mkali kwa
Pam?” Jack akamuuliza na kumfanya Sabrina kuanza kucheka. “Nilijiapia
sitafungua mwanya kwa yeyote kinitumia na kuninyanyasa tena Jack. Nilijiapia na
kumwambia Mungu, chochote nitakachofanya sasa hivi, kiwe kwa ajili ya kujenga
ufalme wake na nitamdai yeye wala si wanadamu wasio na shukurani na ambao
wanabadilika.”
“Uliponikuta
nimepiga magoti hapa nikilia, wala si kwa alilosema mama Msindai, Jack. Mama
yupo sahihi kabisa. Hata mimi nilishajiuliza hilo swali. Mimi nilikuwa nikitubu
Jack. Hakika nimemkosa Mungu wangu na nimejichukia kwa nini nakuwa narudia kosa
mara kwa mara! Namtaka Mungu anifanyie nini ili nimtangulize yeye? Sijui imani
yako Jack, lakini mimi najua kwa hakika tulichofanya mimi na wewe ni dhambi.
Mimi si mkeo Jack. Mungu hajanipa wewe. Mbaya zaidi hatujaweza hata kujibu
maswali ya watu wa karibu kama mama yako, tumekimbilia kitandani! Sio sawa
kwako Jack.” “Mimi sijutii Brina. Ninahamu na wewe kupita nitakavyokwambia au tulivyofanya.
Ndio maana imekuwa ngumu kukuachia asubuhi ya leo, mpaka uliponiambia njaa
inauma. Unaladha ya ajabu sana! Matiti yako mazuri, natamani kukushika kila wakati
ndio maana pale kwenye kochi nilikuwa sitaki ukae, unilalie tu ili mkono wangu
uchezee hayo matiti yako.” “Bwana Jack!” Akamsukuma kwa nguvu.
“Mimi
nasema ukweli kile ninachojisikia.” “Tunamkosea Mungu Jack. Usifikiri nakwambia
hivi kwa kuwa sijakufurahia! Nimekufurahia sana tu. Hata sasa hivi nakutaka
tena. Si unakumbuka mimi ndiye niliyemwambia hata dada Imani asije leo,
nitamtafuta kesho?” “Nakumbuka.” “Kwa sababu nilitaka uendelee kunifanyia
uliyokuwa ukinifanyia Jack, lakini si sawa. Kazi ya mwili ndio hiyo. Kutaka
zaidi na zaidi, na wala hautosheki. Hali ninayojisikia hapa, ni kama ulinigusa
miezi mingi iliyopita, nina ukame sana, kumbe asubuhi tu.” “Basi tuagane.” Jack
akamgusa. Sabrina akamkwepa.
“Hapana
Jack. Tunakaribisha laana na mkosi kwetu. Tuko kwenye wakati mgumu kuliko
unavyodhani. Vita inayokukabili wewe sasa hivi, huwezi bila hekima ya Mungu. Na
ninakuhakikishia Jack, neno, ‘nampenda Brina’ tu, halitoshi kwa familia yako
inayokupenda na kukujali. Unamuhitaji Mungu. Na huwezi kumsikia Mungu ukiwa umemkasirisha.
Naomba tuache huu mchezo wa furaha ya muda, huku tukikimbia uso wa Mungu tunaye
muhitaji. Mbali na hili la ndoa tu, kwenye huu mji tunamuhitaji Mungu ili atupe
kibali, na uweze kushinda. Wenzako wanakwenda kwa waganga, lakini wewe nilazima
umlilie Mungu na ajidhihirishe haswa. Naomba tutubu tumrudie Mungu.
Nimekuhakikishia mimi nipo hapa, sina ninapokwenda na wala sina nitakayemkubali
isipokuwa wewe. Lakini endapo mama akashindwa kunipokea, sitakuwa na namna
ingine.” Jack akainama.
“Umenielewa
Jack?” Jack akanyanyua kichwa na kumtizama. “Umesema mama akishindwa kuelewa
ndio umesema itakuaje?” Jack akauliza. “Mimi ninajua Mungu hashindwi na
chochote Jack. Kama amefanya kwangu kwa hayo niliyokusimulia, atashindwaje
kwako? Na kama mimi ni mke ambaye Mungu alikusudia uwe na mimi, hili jambo
atalisimamia, mpaka likamilike. Tutaomba pamoja kabla hujakwenda kuzungumza na
wazazi, na mimi sitawapigia simu wazazi mpaka wewe utakapoweka sawa mambo yako.
Usiogope, unapomruhusu Mungu aingilie kati jambo, huwa anayo namna yake,
utashangaa na amani tutakayotembea nayo.” “Kwa hiyo mapenzi ni mpaka wazazi
wakubali?” “Acha hizo Jack. Mpaka ndoa.” Jack akatoa macho.
“Brina!”
“Si tumekubaliana tunamtaka Mungu, na nguvu zake pamoja na hekima zake katika
maisha yetu?” “Daah!” Jack akawa ameshachoka. “Basi hiyo ndio garama ndogo sana
yakulipa ili kumpata Mungu.” “Sio garama ndogo bwana.” “Naomba upige magoti
nikuombee Jack. Acha kulalamika. Hutakufa.” Akapiga magoti. “Lakini Mungu
aliona usiku wa jana nilivyolala vizuri?” Akaendelea kuhoji Jack akilala kama
mtoto mdogo. Sabrina akaanza kucheka.
“Yeye
Mungu si anatuwazia yaliyo mema? Sasa mbona mema yamekuja na wewe unaleta
kipingamizi?” “Mema yapo Jack. Lakini yawe yako. Sio kila jema unakimbilia.
Mimi sio mkeo, Mungu hajakupa bado. Akikukabidhi siku ile kanisani, ruksa.
Utaendelea kula mema tu. Unafikiri mimi ndio sikutaki?” “Mimi naona hunogewi
kama mimi.” “Ningefika mara zote hizo kabla yako?” Jack akacheka sana. “Mimi
mpaka nikawa nashangaa. Kidogo tu, tayari!” “Sio kidogo Jack. Ile hali yakujua
nashikwa na Jack. Mwanaume anayenipenda na aliyenivumilia muda wote huo!
Ukanipokea nilivyo, nini kinanizuia unaponigusa nisifike?” Jack akajisikia
vizuri.
“Basi
nikienda nyumbani nawaambia mwezi ujao nataka kuoa. Siwezi kuendelea kusubiri.
Kama hawana pesa, basi. Lakini nakuoa Brina. Hii raha niliyopata jana na leo,
nataka niimiliki.” “Basi tumwambie Mungu. Tushikane mikono tumwambie Mungu.
Tutubu na kumwambia tunahitajiana sana tena kwa haraka, atusaidie.” Sabrina
akamshika mkono Jack akaanza kuomba. Akatubu kwa ajili yake na Jack. Akaomba
baraka na ulinzi kwao. Akaombea mipango yote waliyonayo. Mpaka anamaliza, Jack
ametulia. “Kwa maombi haya naona kweli dhambi itakaa mbali.” Sabrina akacheka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Hapo ndipo
walipo Jack na Sabrina. Vita ya ndani na Ya nje. Watamkabili vipi Mama Msindai?
Jack ameonjeshwa tu, anataka kujenga mzinga. Ameahidiwa yote ni mpaka
ndoa, huku mama bado hajamuweka sawa.
Nini
Kitaendelea?
Usikose Mazito ya
Mbeleni.
0 Comments:
Post a Comment